Miaka ya hivi karibuni, matumizi ya dawa za uzazi wa mpango (Vidonge na Sindano) yameongezeka sana, hali inayozua wasiwasi wa usalama wake miongoni mwa watumiaji.
Baadhi wameonesha wasiwasi wao kuwa dawa hizi husababisha kupata watoto wa kiume wenye homoni nyingi za kike, au hata kupata watoto wa kike wenye kiasi kikubwa cha homoni za kike hivyo kuwafanya wakomae mapema kabla ya umri sahihi.
Mathalani, mdau mmoja wa JamiiForums.com amekiri kuwahi kusikia kuwa matumizi ya muda mrefu ya dawa hizi yanaweza kusababisha mama kupata binti ambaye akifikisha umri wa miaka 8 matiti yake yanaweza kuwa makubwa, yaliyolala.
Ukweli kuhusu athari za dawa hizi ukoje?