Kutokana na ushauri wa kuvaa barakoa kama njia mojawapo ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya kirusi cha korona wengi wetu wanafanya makosa yafuatayo ya uvaaji wake.
1) Barakoa kufunika tu mdomo. Uwezekano wa kuambukizwa kupitia pua ni mkubwa ukivuta hewa yenye virusi. Hii ni pamoja na...
Ni wazi sasa barakoa za vitambaa ndio 'habari ya mjini'. Sasa niwaulize wataalamu wetu wa afya, hizi barakoa zina uwezo wa kuzuia hivi virusi? Kama jibu ni hapana, sasa kwanini hamjachukua nafasi yetu badala yake mmeacha tu wananchi wazivae?
Au tunavaa barakoa ili iweje?
Kupanga ni kuchagua, kwasasa traffic polisi wabaki wachache barabarani wahamie kwenye kuzuia vifo vinavyotokana na COVID-19. Taifa lihamishie nguvu zake kwenye CORONA pia kwa kuwapeleka Polisi wengi sehemu zenye mikusanyiko mikubwa Kama stand, masokoni, bank, nk ili kuhimiza kunawa mikono...
Habari iwe kwenu wakuu!
Leo nilikuwa nimepanda gari kwenda kazini (huwa napanda magari 2 hadi kufika kazini) cha kushangaza kwenye gari la kwanza mpaka nashuka nilihesabu watu wasio na barakoa wakafika 15 na kuna wakati gari ilikuwa na jumla ya watu 28 huku watu 15 wakiwa hawana barakoa...
Bei ya jumla ya Sukari ni Tsh 2800/= kwa kilo moja, hii ni kwa DSM, lakini katika hali ya kushangaza serikali inawataka wafanyabiashara wa reja reja waiuze kwa Tsh 2600/= kwa kilo moja, hili jambo halitawezekana hata kwa mtutu wa bunduki, hivi sasa sukari madukani imefichwa na wafanyabiashara...
Na WAMJW- DSM .
Serikali kupitia Wizara ya Afya, imetoa wito kwa wananchi kuteketeza Barakoa zao vizuri baada ya kumaliza matumizi yake kisha kuitupa sehemu salama ili kuepusha kusambaa kwa magonjwa ya mlipuko hususan ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona. .
Wito...
Nchini singapore ni kosa mtu kutoka bila kuvaa barakoa/ mask ! endapo hili litakiukwa mtu atalipishwa faini ya $300 na akirudia atalipishwa $1,000
Czech republic na slovakia ni nchi nyingine ambazo zimepitisha sheria ya kila mtu lazima avae barakoa ili kupambana na ugomnjwa huu wa COVID19...
Waziri wa viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa amesema bei ya barakoa zinazotengenezwa hapa nchini hazitakiwi kuzidi Tsh. 1,500.
Yoyote atakayekwenda kinyume na agizo hili hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Chanzo: Clouds tv!
Salaam wakuu,
Huu Ugonjwa wa Corona umekuja na mengi ikiwemo kuvaa Barakoa kuziba mdomo na Pua ili ili majimaji ya Korona yasikupate au hata kama na wewe una Corona usiweke kuambukiza wengine pale unapo piga chafya.
Ila mimi nikiivaa naona ni Mateso makubwa. Wenzangu mnawezaje kuvaa Barakoa...
China imkamata barakoa milioni 89 za barakoa zilizotengenezwa chini ya kiwango. Hitaji la barakoa limeongezeka baada ya mataifa mengi duniani kuzihitaji ili kupambana na #CoronaVirus
Nchi kadhaa zimerudisha barakoa hizo za kutumiwa na wahudumu wa afya na watu walioko katika hatari ya kupata...
Taarifa kutoka Morogoro zinadokeza kwamba Mbunge wa Chadema Mh Devota Minja amekamatwa na jeshi la polisi kwa Amri haramu ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro , kwa kosa la kufuata muongozo wa kuzuia Corona wa shirika la Afya la dunia ( WHO ) na kugawa Barakoa bora kabisa za viwango vya N 95 kwa...
Wanasiasa mnatuangusha. Tulitegemea hata chama kimoja kijitokeze kugawa bure barakoa kwa nchi nzima Kama ambavyo mmekuwa mkifanya kipindi Cha uchaguzi, ambapo huwa man uwezo wa kugawa tisheti, kofia, kanga na vitu vingine vingi nchi nzima.
Huu ndo wakati wenu tunawaomba mjitokeze.
Mwandishi wa habari nguli mh Pascal Mayalla amewataka wataalamu wa Kemia kuja hadharani na kutuchambulia faida na hasara za kupiga fumigation mitaani na kwenye vyombo vya usafiri kama kuna tija kwenye mapambano dhidi ya Corona.
Kadhari watuelimishe juu ya ubora wa barakoa kama zinaweza...
Wahenga walishasema tangu zamani kwamba kutoa ni moyo , na wala si utajiri , huyu Devota Minja yeye ameamua kutoa barakoa ili kuwaokoa wananchi dhidi ya vifo vya corona.
Lakini inafahamika kwamba Tajiri Mohamed Abood yeye miaka yote anatoa Magari ya kubebea maiti kupeleka makaburini kuzika ...
MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA MATUMIZI YA BARAKOA
Uvaaji wa barakoa au “mask” ni moja ya njia za kujikinga na maambukizi ya magonjwa mbalimbali ya kuambukiza. Katika kudhibiti kusambaa kwa Virusi vya #Corona
Barakoa inapaswa kuvaliwa endapo unakohoa au kupiga chafya, mtu wa karibu yako ana dalili...
Mengi yamesemwa kuhusiana na hizi barakoa na hadi sasa hivi kuna baadhi ya watu hawajazielewa vizuri.
Kuna wanaodai zile za kutengenezwa mtaani hazifai kabisa lakini kuna kundi la watu wengine wanadai hata hivyo zinasaidia kuliko kuacha kabisa kuvaa.
Nilichokishuhudia leo kwa jirani yangu...
Nashauri katika kupambana na ugonjwa corona, viongozi wakuu wa kitaifa kwa maana ya Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, wawe wanavaa barakoa kila wanapojitokeza hadharani iwe ni katika mikutano na waandishi wa habari ingawa mikutano hii nayo inapaswa kuepekuwa au waendapo kusali katika nyumba...
Tatizo kubwa hapa nchini ni kwamba pale inapotokea janga, mlipuko wa ugonjwa basi wafanya biashara hutumia nafasi hiyo kujinufaisha. Kuna vifaa kama hand sanitizer, medical face masks vimekuwa katika uhitaji mkubwa sana kwa ajili ya kujikinga na virusi vya corona.
Serikali kupitia waziri wa...
TAARIFA YA WAZIRI KIVULI WA AFYA, MAENDELEO, YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO KWA VYOMBO VYA HABARI
Kumekuwepo na sintofahamu kubwa miongoni mwa Watanzania juu ya ufahamu wa aina gani sahihi ya barakoa (mask) wanazopaswa kuvaa pale wanapokuwa katika shughuli zao za kila siku ili kujikinga...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.