MIMI; Hivi unajua unaibiwa sana kila siku, tena bila kujua?
WEWE; ‘Aaah wapi! Mimi ni mtoto wa mjini, siwezi kuibiwa kizembe, wewe unaongea tuu’
MIMI; Ni kweli wewe ni mtoto wa mjini, Lakini usisahau kwamba; ‘Ndege mjanja hunasa kwenye tundu bovu’ Na inawezekana tundu ulilonasa wewe siyo bovu...