uchaguzi

Uchaguzi Tanzania
Uchaguzi hasa wa viongozi katika nchi ni utaratibu (mchakato) rasmi unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria kuwawezesha wananchi kufanya maamuzi kwa njia ya kuwapigia kura kuwachagua watu ambao wanawataka kuwaongoza kwa kipindi maalum.

Uchaguzi ni utaratibu wa kawaida wa demokrasia wa kuwapata wawakilishi wa kisiasa ambao umekuwa ukitumika tangu karne ya 17. Kuna aina tatu za msingi za uchaguzi zinazotumiwa kuwapata viongozi kulingana na mfumo unaotumiwa na nchi husika.

Aina hizo ni uchaguzi wa Rais, Uchaguzi wa Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria na Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Vyama vya Siasa kwa upande wao navyo huendesha chaguzi ambazo zinajulikana kwa jina la “Chaguzi wa Msingi” zinazotumika kuwachagua wateuliwa wa vyama katika aina za uchaguzi ambazo zimetajwa hapo juu.

Endapo Tume haitaridhika kabla ya kutangaza matokeo ya uchaguzi kwamba kulikuwa na kutokufuatwa kwa taratibu, matumizi mabaya au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi au pale ambapo kura za wagombea waliopata kura za juu imelingana, Tume itasimamisha au kufuta uchaguzi au sehemu yoyote ya uchaguzi na itatangaza siku nyengine ya kurudiwa kwa uchaguzi huo.
  1. Stephano Mgendanyi

    LGE2024 Mbunge Ghati Chomete: CCM Imejipanga Vizuri, Lazima Itashinda kwa Kishindo Uchaguzi Serikali za Mitaa

    MBUNGE GHATI CHOMETE: CCM IMEJIPANGA VIZURI, LAZIMA ITASHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara Mhe. Ghati Zephania Chomete, tarehe 26 Novemba 2024 ahitimisha kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kuwaombea kura wagombea wa CCM Wilaya ya Musoma...
  2. Waufukweni

    LGE2024 Tundu Lissu: Walitufanyia mizengwe ili tususie Uchaguzi

    Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara Tundu Lissu, akielezea hali waliyokutana nayo wakati wa kuapisha mawakala wa chama hicho wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Tarafa ya Ikungi, wilayani Ikungi mkoa wa Singida, leo Novemba 26, 2024.
  3. Bams

    LGE2024 Uchaguzi wa Serikali Za Mitaa, Hakuna Kiongozi hata mmoja wa Serikali aliyewahi kutoa karipio Juu ya Uovu Uliokuwa Ukitendeka

    Nchi yetu ya ajabu sana, iliyojaliwa kuwa na viongozi wa ajabu pia, viongozi wanaobariki maovu alimradi maovu hayo yawe ni dhuluma ya kuwanufaisha CCM. Fikiria, waziri Mchemgerwa ndiye mwenye jukumu la kutengeneza kanuni za uchaguzi, akatengeneza kanuni za hovyo kabisa, ikiwemo ile ya kifungo...
  4. R

    Pre GE2025 Uchaguzi ni mchakato, kama kujiandikisha, kuteuliwa, na kuapishwa kumekuwa na "madudu" sahau kuwa kesho kuna haki yoyote itatendeka kwa wapinzani

    Tumeona ukiukwaji mkubwa katika kujiandikisha, kuenguliwa wapinzani, /kuteuliwa. kuwekewa mapingamizi ya uongo na kweli, kuapishwa wamekataliwa, sasa UPINZANI mnadhani kesho ndiyo CCM watatenda haki?
  5. Tlaatlaah

    LGE2024 Nawatakia wana JF wote uchaguzi wa amani, Kesho

    Kwa wale wote tutakao shiriki uchaguzi muhimu mno na wa maana sana wa serikali za mitaa, Nawatakia nyote matumizi sahihi uhuru na haki ya kikatiba, kwa kuchagua viongozi makini na watakao saidia kuchochea mageuzi na maendeleo katika mtaa au kijiji unachoishi. Hongera kwa uchaguzi wa...
  6. Waufukweni

    LGE2024 Polisi Songwe wafanya doria kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

    Saa chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji kesho Jumatano tarehe 27 Novemba, 2024 Jeshi la Polisi mkoa wa Songwe mapema leo Novemba 26, 2024 limefanya doria za magari na miguu katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Songwe ikiwemo mji wa Tunduma wilaya ya...
  7. Waufukweni

    LGE2024 Wananchi wa Lupembe wako tayari kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa

    Wananchi wa jimbo la Lupembe wameeleza utayari wao kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika leo Novemba 27, 2024 Nchi nzima huku wakiweka wazi Matarajio yao kwa viongozi wapya watakaochaguliwa Wananchi hao akiwemo Fikiria Vicent Kisogole, Salvina Barton Mpolo na Martina Isdol...
  8. Mindyou

    LGE2024 Tundu Lissu anazungumza kuhitimisha kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Ikungi Singida

    Wakuu. Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu anazungumza muda huu huko mkoani Singida kuhitimisha kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Fuatilia uzi huu kujua nini kinaendelea Tundu Lissu amesema kuwa mara ya mwisho Tanzania kufanya Uchaguzi ilikuwa nwaka 2014 kwani mwaka 2019...
  9. Waufukweni

    LGE2024 Dkt. Philip Mpango awahimiza Wananchi kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amewahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi katika kushiriki zoezi la uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika kesho tarehe 27 Novemba 2024. Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akizungumza na abiria...
  10. Mindyou

    LGE2024 Mkuu wa mkoa wa Dodoma: Atakeyevuruga Uchaguzi Dodoma atachukuliwa hatua

    Wakuu, Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema kuwa hatua zitachukuliwa dhidi ya mwananchi yeyote atakayeonesha viashiria vya uvunjifu wa amani kuelekea uchaguzi wa serikali za Mitaa utakaofanyika kesho Novemba 27, 2024 nchini. "Siku ya kesho ya kupiga kura kila mtu atunze amani...
  11. T

    LGE2024 CHADEMA wanashiriki uchaguzi wakitegemea nini? Hatutaki malalamiko

    Msije baadaye mkasema mmedhulumiwa kura au kura zimeibwa. Mnapoingia uwanjani ni kuwa mmekubaliana na sheria na taratibu za mchezo. Hakuna excuses za kipuuzi. Ni kupambana na kukubaliana na matokeo. Hakutakuwa na excuses ni mapambano. Mshindi apatikane. Maana hamchelewi kusema mlinyanyaswa...
  12. Waufukweni

    LGE2024 Dorothy Semu amuonya Mtendaji wa Kijiji kutoipendelea CCM Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

    Kiongozi wa ACT Wazalendo, Dorothy Semu, amemuonya mtendaji wa Kijiji cha Angalia kutopendelea Chama cha Mapinduzi (CCM) wajibu wake nikutumikia wananchi sio ubaguzi wa itikadi katika uchaguzi. Kauli hiyo ameitoa baada ya mtendaji huyo kuzuia mikutano ya chama hicho kutumia maeneo ya Umma, Semu...
  13. Political Jurist

    LGE2024 Shemsa asisitiza umuhimu wa Uchaguzi katika maendeleo

    Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Simiyu Ndg.Shemsa Mohamed ameendelea na ziara yake yenye jina la Siku Saba za Moto ambapo tarehe 25 Novemba, 2024 aliweka kambi katika Jimbo la Kisesa akitembelea Kata ya Bomani ,Kata ya Isengwa na Mwasengela. Ndg.Shemsa amekutana na kuzungumza na...
  14. Waufukweni

    LGE2024 CCM hatutegemei dola, tutawashughulikia watakao vuruga Uchaguzi

    Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma kimesema kimejipanga kwa njia zote kuhakikisha kinalinda amani kabla ya Uchaguzi na baada ya Uchaguzi ikiwemo kuwadhibiti wale wote wenye nia mbaya (ovu) ya kutaka kuvuruga Uchaguzi kwa kuanzisha Vurugu. "Asitokee mtu yeyote au kundi kupanga njama za kutaka...
  15. G

    LGE2024 Sielewi lengo la CHADEMA kushiriki uchaguzi huu

    Inajulikana wazi kuwa CCM hawawawezi CHADEMA katika sanduku la kura, hivyo imeweka nguvu kubwa kwenye figisu na dhulma. CCM tayari wameonesha taa nyekundu ktk hatua za mwanzo kwa kuwaengua wagombea wa chadema 16,0000, na baada ya rufaa wagombea 5,000 tu ndiyo wamerejeshwa. Pia viongozi wa...
  16. Mzee Mwanakijiji

    Pre GE2025 Wazo Jipya: Sema Mambo 3 CHADEMA wafanye sasa kwa Uchaguzi Mkuu 2025

    Ukiniuliza mimi ntasema mambo yangu matatu; siyo mageni sana lakini naamini yanaweza kuisadia CHADEMA kujiandaa na uchaguzi mkuu mwakani. Na wewe kama unayakwako yaweke labda katika wastani yatapatikana mambo matatu makubwa. 1. Itangaze mapema kama msimamo wa chama kuwa wagombea wote wa ubunge...
  17. The Watchman

    LGE2024 Chalamila: Kwa atakayetishia usalama siku ya uchaguzi tutamnyakua na hatokuwa salama

    Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila akizungumza jijini Dar es salaam kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa mnamo mwezi Novemba 27, 2024 amesema hali ya usalama mkoa wa Dar es salaam ipo vizuri na mtu yeyote atakayejaribu kuharibu amani iliyo siku ya uchaguzi hatoachwa salama na...
  18. Roving Journalist

    LGE2024 Dkt. Doto Biteko ahimiza Watanzania kupiga Kura Novemba 27, 2024 asema ni Haki ya Kikatiba

    Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amewahimiza Watanzania kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024. Dkt. Biteko ametoa rai hiyo leo Novemba 25,2024 akiwa mkoani Geita ambapo amesema uchaguzi huo ni muhimu hususan kwa ukuzaji wa demokrasia...
  19. Papaa Mobimba

    LGE2024 ACT Wazalendo Tunduru: Kuna vijana wamepangwa kupiga kura za mapema, tunawaonya...

    Mwenyekiti wa ACT Wazalendo wa Jimbo la Tunduru Kaskazini mkoani Ruvuma, Yasin Mohamed Mawila, ametoa onyo kali dhidi ya jaribio lolote la udanganyifu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024. Akizungumza Jumapili, Novemba 24, 2024, kwenye mkutano wa kampeni...
  20. Waufukweni

    LGE2024 Mussa Zungu ajitosa kampeni za Mtaa kwa Mtaa, awaombea Kura Wagombea CCM, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

    Mussa Azzan Zungu, ambaye ni Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, ameendelea na kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Kata ya Upanga Magharibi, jijini Dar es Salaam. Amengia kuogea na wananchi mtaa kwa mtaa na nyumba kwa nyumba, Zungu amewanadi wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika...
Back
Top Bottom