1963: Rais wa Jamhuri ya Tanganyika, Julius Nyerere akiweka pini katika koti la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. U Thant

Ndugu zangu,
Miaka zaidi ya 30 sasa imepita toka niliposoma Nyaraka za Sykes.

Hivi sasa katika mambo yanayonisikitisha ni kwa Sykes kuzirejesha hizi nyaraka kwenye ''safe,'' kuzifungia na kutoziweka wazi kwa watafiti kuzisoma.

Watafiti wangepewa fursa ya kuzipitia wangeona kuwa kila mzalendo pamoja na wakoloni Waingereza waliohusika katika siasa za kipindi kile wamo ndani ya nyaraka hizi.

MJ Molohan.
Nimemsoma ndani ya Nyaraka za Sykes.

MJ Molohan Mwingereza huyu alikuwa Kamishina wa Kazi nimemkuta katika Nyaraka za Sykes akipambana na Kleist Sykes miaka ya 1930s hadi 1950 anashughulika na watoto wa Kleist katika siasa za wafanyakazi Waafrika.

Kwanza na Abdul katika Dockworkers' Union kisha na Ally katika TAGSA.

Baada ya mgomo ule wa makuli na sheria ya kuundwa kwa vyama vya wafanyakazi kupita Molohan alianza mchakato wa kutafuta watu ambao wangeweza kushika nafasi ya Katibu Mkuu wa Dockworkers’ Union.

Islam Barakat alikuwa Labour Inspector wa kwanza Mwafrika ingawa alikuwa na damu ya Kiarabu na Kiafrika.

Molohan alimwomba Barakati amsaidie kutafuta mtu wa kusika nafasi ya Secretary General wa Dockworkers' Union.

Barakat alipeleka majina mawili.
Jina la Abdul Sykes na la Erika Fiah.

Abdul Sykes, kijana wa mjini miaka 24, mtoto wa mfanyabiashara na mwanasiasa maarufu Dar es Salaam.

Jina lingine lilikuwa la Erika Fiah miaka 53, mwanasiasa mpevu na mtu wa makamo.

Erika Fiah alikuja Tanganyika pamoja na ma crejeshi ya Waingereza kutoka Uganda wakati wa Vita Kuu vya Kwanza.

Baada ya vita alilowea Tanganyika na kuishi Mission Quarters ambako alihariri gazeti lake, Kwetu.

Fiah alikuwa Mwafrika wa kwanza kuanzisha na kumiliki gazeti lake mwenyewe katika Tanganyika.

Mtu wa pili alikuwa Ramadhani Mashado Plantan mtoto wa Chief Mohosh Shangaan kutoka Mozambique alikuyekuwa Tanganyika na Hermann von Wissman akiongoza jeshi la askari mamluki wa Kizulu.

Tanganyika akajulikana kama Affande Plantan mkuu wa Germany Constabulary.

Watoto wake kama walivyokuja kuwa watoto wa Kleist wameacha historia kubwa katika Tanganyika.

Fiah kama wanasiasa wote wa zama zake, alikuwa Mwafrika kwanza na uzalendo ukafuatia.

Vilevile alikuwa mmoja wa wafuasi wa mwanzo wa Karl Marx nchini Tanganyika na gazeti lake Kwetu, lilikuwa maarufu kwa sababu ya ukali na vijembe vyake dhidi ya ukoloni.

Fiah alikuwa mwanasiasa aliyekuwa amepea sana katika wakati wake.

Katika miaka ya 1930 aliwahi kujaribu kuhamasisha tabaka la wafanyakazi na wakulima kuwaunganisha dhidi ya ukoloni, lakini alishindwa kwa kuwa wananchi walikuwa bado hawajaamka kiasi cha kutosha kuweza kuitikia mwito wa kuuhamasisha umma kama tabaka.

Kwa wakati ule Fiah alikuwa na upeo mkubwa wa siasa na alikuwa na uwezo wa kuhamasisha zaidi kuliko kijana mdogo Abdul Sykes.

Vilevile Fiah alikuwa mtu mzima na uzee ni dawa.

Haiwezekani kumlinganisha Fiah na Abdul Sykes aliyekuwa kijana mdogo ambaye Fiah angeweza kuwa mtoto wake.

Kati ya kipindi kile kati ya vita vya kwanza na vya pili ya dunia, Fiah alitumia kalamu yake kudhihirisha bila ya woga matatizo yanayowakabili Waafrika.

Lakini Fiah hakuwa tu adui wa serikali alikuwa pia adui wa Kleist na Waafrika wengine mashuhuri, wengi wa hao wakiwa katika utumishi wa serikali.

Huko nyuma katika mwaka wa 1933 kulikuwako na mgongano baina ya Kleist na Fiah kuhusu uongozi wa African Association.

Kupitia gazeti lake Fiah alimshambulia Kleist akimshutumu kwa kile Fiah alichokiona kuwa tabia yake isiyokuwa ya kizalendo iliyotokana na asili yake ya Kizulu.

Fiah alidai kuwa mambo yanapokuwa mazuri kwa Watanganyika Kleist atajinasibisha na Utanganyika, lakini upepo unapobadilika na kuvuma upande wa Wazulu, mara Kleist anakuwa Mzulu.

Ili kuepuka mgongano Kleist alijiuzulu kama katibu wa African Association na Fiah alichaguliwa kushika nafasi hiyo.

Kalamu ya Fiah ilikuwa haina muhali. Katika rambirambi alizotoa za kijeuri na za dharau juu ya kifo cha Martin Kayamba, Fiah aliomboleza kwa kusema kwamba Waafrika hawakunufaika kwa elimu ya Kayamba wala kwa wadhifa wake kama karani wa kaimu Katibu Mkuu katika serikali ya Waingereza.

Fiah alipingana na Wazungu vilevile.

Mwaka wa 1940 aliandika tahariri iliyowalenga Wazungu waliokuwa wakimpinga kwa kueleza wazi wazi fikra zake na kwa kuchapisha gazetini makala juu ya haki za Waafrika.

Fiah alikuwa mwanaume kweli kweli hata ingawa wakati wa zile harakati za bandarini makuli wakiwa wanakwenda nyumbani kwa Kleist kumfuata mwanae Abdul kwa maandamano na hivyo kumpa hadhi ya uongozi wa harakati zile, kwa hakika Abdul Sykes hakuwa anafikia hadhi wala kiwango cha Fiah ktika siasa za nyakati zile.

Kumfananisha Abdulwahid na Fiah ilikuwa sawa na kufananisha mlima na kichuguu.

Mara kwa mara mawazo ya Erika Fiah kama ilivyotegemewa hayakupokelewa vizuri na serikali katika ya hao waliokuwa serikalini akiwa MJ Molohan.

Ndugu zangu ikiwa kama hamkumjua Fiah huyu ndiye Erika Fiah.

Erika Fiah, Kleist Sykes, Mzee bin Sudi, babu yangu Salum Abdallah kwa kuwataja wachache hawa wote wakifahamika kama ''Wakuja,'' na wenyeji wakiwasema kuwa wanapenda sana kujitia kimbelembele.

Ile ''Wakuja,'' wakiwa na maana kuwa hawana asili ya Tanganyika.

In Shaa Allah darsa litaendelea tutatazama mapambano baina ya Abdul Sykes na Erika Fiah.


Erika Fiah
 
Na uso umevaa kikoi unarusha madongo [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
Janina,
Nakukumbusha tena kuwa jambo lolote ukilitia upole litapendeza.

Ingependeza kama ungeshauri pawepo na subra ijulikane mbona barza imekuwa kimya?

Sasa mtu angesoma mabezo na vicheko vya mbezaji kisha akakusoma wewe unashauri utulivu na kutaka kujua kulikoni angeona tofauti iliyoko baina yenu.

Mtego usingeteguka
Ila kwa zake haraka

Panya kuchungulia kataka
Hapo ndipo mtego ulipofyatuka

Kutoka hawezi macho yamemtoka
Panya masikini kiranga kimemtoka

Mama yake amuuliza kipi kilichokuponza
Ilhali subira nilikufunza?

Nani huyu tena?
Muyaka?
 
"inge" ndio haikuundwa vizuri. Uwezo ndipo ulipoishia, hata baada ya kuelezwa kuwa unaipeleka nchi pabaya, hakuelewa. Ndipo alipopata jina "haambiliki" akakasirika.
 
Kwenye kupigania Uhuru hutosikia majina ya machifu...hawa walikuwa beneti na wakoloni
Ajabu Nyerere alivyopewa nchi Tu..
Akaleta hawa machifu kwenye serikali..


Mang'enya
Fundikira na wengineo

Aliwaleta for strategic reasons sawa na wale Viongozi wa cooperatives kama Kasambala, Bomani, Kahama etc. Machief na hawa viongozi wa ushirika walikuwa na ushawishi na wafuasi wengi seheme walizotoka.

In hindsite, hivi vinavyoitwa VIKOBA sio modified form of COLLECTIVES?
 
Sasa hiyo Shirazi iko Afrika? Eti "Waafrika wanojiita Washirazi", labda ungeandika Waafrika waliochanganya damu na Washirazi (Afro Shirazi, kina Thabit Kombo) Kama vile tunavyowafahamu "Afro Americans".


Nakuona una jitahidi kutaka kuutetea ukweli usioujuwa, ingawa unausoma na kuusikia ukweli kwa wanaoujuwa na wenye ushahidi wa tafiti na wenye mashiko, lakini, bila aibu moyo wako uliojaa chuki za kijinga hautaki kuamini.

Hutoweza kuutetea ukweli kwa uongo wa chuki zako za kujazwa ujinga. Hauna mashiko.
 
Hata China haukufanikiwa ujamaa na ndio maana mpaka leo wanauana sana. Dont judge the book by its cover. Wachina kila walipopata nafasi ya kuutoroka ujamaa walitoroka, mpaka sasa hivi wakipata fursa za kuishi nje ya kwao hawana hamu ya kurudi. Katazame walivojazana US, Canada na Europe. Sasa wameanza kujazana Afrika na Asia nje ya China. Jiulize kama huko ni neema, wakikimbia nini?
 
Utumwa si Zanzibar tu, hata bara ulikuwepo na bado upo. Au huelewi kuwa mpaka leo utumwa upo?
 
Madini mpaka leo "yanachotwa", nini kinazuwia? Mtayala wenyewe?

Kuhusu kilimo kabla ya Uhuru, ukiisoma vizuri historia, wakati tunapata Uhuru Tanganyika ilikuwa namba 1 katika Afrika kuuza mazao nje. Jiulize ilikuwaje miaka 7 tu baadae tukawa omba omba namba moja duniani?
 
Halali na Haramu ni subjective. Halali kwako ni haramu kwa mwengine.


Wewe uhalali wako unaupata kutoka kanisa alilokuanzishia mzungu. Mimi uhalali naupata kutoka kitabu cha Allah.

Hapo sasa.
 
Hilo ni moja tu ya "makosa makubwa", kama ulivyoandika. Tuainishie makosa mengine kwa mtazamo wako, pia tuainishie na Mafanikio yake ni yepi?



Hapo sasa!
 
"inge" ndio haikuundwa vizuri. Uwezo ndipo ulipoishia, hata baada ya kuelezwa kuwa unaipeleka nchi pabaya, hakuelewa. Ndipo alipopata jina "haambiliki" akakasirika.
Humpendi Mwalimu Nyerere kwa kuwa siyo dini yako.

Wewe ni mbaguzi with no shame.

Kama siyo mwalimu ukapata walau elimu ya hiyo ungekuwa flat over.
 
Humpendi Mwalimu Nyerere kwa kuwa siyo dini yako.

Wewe ni mbaguzi with no shame.

Kama siyo mwalimu ukapata walau elimu ya hiyo ungekuwa flat over.
Hayo yako na uliyesema "inge.." ni wewe. Au kabadili kauli yako.

Dini yangu wewe inakuuma nini? Au ndio unapotaka kujifichia huko, kuubadili mjadala kuufanya wa kidini?
 
Ndio maana nimesema waafrika wanaojiita washirazi. Waliochanganya damu ya kiafrika na kishirazi walijiita washirazi sio Afro Shirazi. Hata hao wanaojiita waarabu wengi wao ni waafrika waliochanganya damu ya uarabu na hawajiiti Afro Arabs. Hoja za kubuni kama hiyo ya Afro Shirazi ndio inayonifanya nikuone mpumbavu. Mpumbavu hana tiba. Ni kipaji.

Afro Shirazi Party kiliundwa tarehe 5 Februari mwaka 1957 baada ya vyama vya African Association kuungana na cha Shirazi Association. Thabit Kombo Jecha Al Shiraz alikuwa mwanachama wa Shirazi Association na mwaka 1956 alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wake. Siku zote alitambulika kama mshirazi na sio mafro shirazi. Chama cha Afro Shirazi hakina uhusiano na watu kuchanganya damu.

Ushahidi upi wa kuokoteza? Mimi nahoji kwa sababu huo unaouita ushahidi hauna mashiko. Ndio maana tukiwahoji mnakimbilia kudai tunawachukia.
Ujinga wangu utaondoka mkinielimisha lakini kwa vile mpaka sasa hivi hamjafanikiwa nitabaki kuwa mjinga.

Amandla...
 
Utumwa si Zanzibar tu, hata bara ulikuwepo na bado upo. Au huelewi kuwa mpaka leo utumwa
Nazungumzia Chattel Slavery ambapo mtu na uzao wake ulihesabiwa kuwa bidhaa na ulimilikiwa na binadamu mwenzake. Afrika bado upo Mauritania na Sudan. Labda uniambie Tanzania ni wapi watu wanawamiliki wenzao na uzao wao na wanawauza kama bidhaa nyingine.

Amandla...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…