Nilijua kimbilio lako ni mdini mwenzako Mohammed Said. Utamuamini vipi mtu anayedai kuwa waarabu hawakuua waafrika wala kuwatesa!
Ili upate balance, nakushauri usome kitabu cha Ali Sultan Issa, kinachoitwa Walk on Two Legs, aliyezaliwa Wete, Pemba mwaka 1932, mwanachama wa ZNP ambae alihamia chama cha Umma. Anazungumzia waafrika waliojiita washirazi ili kujitofautisha na wale walioletwa kama watumwa au wafanyakazi. Anazungumzia watumwa walioletwa kutoka Congo. Anazungumzia mjomba wake aliyerithi mtumwa kutoka kwa babu yake. Aliwajua watu waliokuwa watumwa. Anazungumzia jinsi waarabu wa Pemba walivyozaa na waafrika. Yeye mwenyewe upande wa mama yake asili yao ilikuwa Yemen, upande wa baba Oman. Hata hivyo mama wa bibi yake mzaa mama, ( aliitwa Bibi Ruzuna Binti Tamim, aliyewahi kuwa mke wa Sultan Ali bin Hamoud) alikuwa mzaramo na bibi huyo huyo alikuwa na damu ya wanandi kutoka Kenya. Huyu bwana alikuwa rafiki mkubwa wa Babu na anaelezea kuhusu ushirikiano kati ya chama cha Umma na ASP kuandaa mapinduzi ya Zanzibar. Anaelezea jinsi wao wakommunisti waliwaachia shughuli nzima ASP Youth League kwa sababu wao hawakuwa wengi na serikali iliwahofia zaidi UMMA kuliko ASP. Anaelezea jinsi Yusuf Himidi, Said wa Shoto, Abdullah Said Natepe, Khamis Darweshi, Ramadhan Haji, Pili Khamis, Seif Bakari na Saidi Iddi walivyoongoza uvamizi wa armoury iliyokuwa Ziwani. Hawa walivamia pia Police Barracks zilizokuwa Mtoni. Ukitaka kujua zaidi kuhusu Mapinduzi soma dissertation ya Ph. D ya Ann Lee Grimstad aliyoitetea mwaka 2018 katika Chuo Kikuu cha Florida. Kama nilivyokuambia hapo awali, udini unakupa ujinga. Usiwasikilize wakina Mohammed Said peke yao. Fanya utafiti wako mwenyewe ndio utajua ukweli.
Kwangu mimi sina zaidi ya kuchangia kuliko haya. Una uhuru wa kuamini utakacho.
Amandla....