2022 Haya ndio makabila yanaongoza kwa maendeleo

2022 Haya ndio makabila yanaongoza kwa maendeleo

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925
Zingatio 1: Simo katika kabila lolote kwenye hii orodha, sina mgongano wa kimaslahi wa kunifanya kupendelea ama kuchukia makabila niliyotaja.

zingatio 2: kuwa ndani ya haya makabila haimaanishi watu wote wa kabila hilo wafanikiwa, hata idadi ya wenye mafanikio makubwa ndani ya haya makabila bado ni ndogo, usibweteke kujidanganya umefanikiwa kisa umo ndani ya haya makabila, Tafuta chako!!

Muhimu 3: kama kabila halipo haimaanishi halina watu waliofanikiwa, kuna watu wa makabila ambayo hayamo humu wana mafanikio makubwa kuzidi watu kibao wa makabila yaliyowekwa hapa.

Muhimu 4: hakuna muhuri wa kudumu wa umasikini ama maendeleo kwenye haya makabila, kuna kupanda na kushuka, kuna makabila yalikuwa chini zamani ila kwa sasa yanakuja kwa spidi ya radi, mengine yameshuka.

1. Wachaga -

🎯Biashara
🎯Elimu
🎯Siasa
🎯Kubebana
🎯Kuendeleza kwao

Kibiashara kabila hili wapo katika nafasi nzuri, wamekuwa pioneers wakubwa katika kuanzisha na kuziendeleza biashara kibao, mifano ya biashara maarufu kuna kampuni ya ndege za Precision Airways, Hamidu city sehemu ya makazi yenye nyumba elf 2 za kisasa, hotel kali za Arusha / Dar, n.k. Icon kubwa katika kabila hili ni Marehemu Mzee Reginald Mengi, aliweza kuingia ndani ya orodha ya top 10 ya matajiri wa hapa nchini akiwa ni mtanzania pekee mwenye asili ya makabila ya hapa kwetu, kwenye elimu nako hakuwa nyuma, alikuwa muhasibu wa kwanza nchini kuthibitishwa na bodi ya wahasibu na wakaguzi wa hesabu za fedha (CPA), aliweza kutumikia sehemu mbali mbali zilizompa mishahara minono lakini aliamua kugeukia ujasiriamali uliompa utajiri mkubwa.

Kielimu wamejitosheleza, mkoa wanaotokea unaongoza kwa kuwa na shule nyingi tangu zamani hadi sasa, kupata elimu ni kitu rahisi, maofisini katika kila watumishi 10 imeshazoeleka kumkuta mchaga walau mmoja na hii idadi imepunguzwa sana, miaka ya nyuma maofisin kulijaa wachaga na makabila machache yasiyozidi matatu yaliyokuwa na wasomi hususan wahaya. sikuhizi hali ni tofauti, elimu imesambaa kwenye makabila mengi na mbaya zaidi wasomi ni wengi kuzidi ajira kiasi kwamba nafasi 1 inagombaniwa na watu 500, pia wizara ndio inasimamia zoezi la ajira sio kama zamani kila shirika / taasisi ilijisiamia kwenye kuajiri, bosi akiwa mchaga anarundika ndugu zake. Uzuri ni kwamba wachaga hawategemei ajira pekee, huwa kuna mlango mwengine wa kufanya biashara, inakuwa rahisi kwao kuanza biashara maana wana utamaduni wa kubebana kwa kuchangiana mitaji na kwavile kunakuwa na ndugu wanaofanya biashara huwa inakuwa rahisi kushikwa mkono kupewa ramani, ushauri na connections za biashara.

Kisiasa wapo active na sijaona wa kuwakaraibia, vyama vikuu vya upinzani vilivhowahi kuleta upinzani mkali kuanzia Tlp, Nccr na Chadema vimeanzia huko kwao, wamo pia kwenye chama kikuu cha ccm na influence yao ya political power si haba.

Kubebana na kusaidiana ni silaha kubwa sana katika maendeleo yao, mmoja akitoboa anasaidia wengine.

Hawasahau kuendeleza walikotoka, wanajenga na kuboresha makwao huko kwenye asili yao, hata ikitokea misiba au wakirudi kusalimia huwa hapati shida kwenye makazi. Kuna nyumba ya Marehemu mzee Mengi aliijenga kwao ni mfano wa mansion za kisasa.

kila mwisho wa mwaka kabila zima huwa wanarudi makwao kwa pamoja, ni utamaduni wa kipekee, kukutana huku husaidia ndugu waliotawanyika kukutana, ndugu kuchangiana mitaji, ndugu na majirani kujuliana hali, kupanga mikakati, kutambulisha watoto kwa ndugu, n.k. kurudi inakuwa rahisi maana makazi ya vijijini wanayaboresha.

mkoa wao ni wa pili kwa kiwango kidogo cha umasikini...

Niishie hapa maana ntaanza kuonekana nawapendelea lakini kila nilichoorodhesha hapa ni facts.

Wakinga -

🎯Biashara
🎯Kubebana

Kama ilivyo kwa wachaga, nao hawa kubebana na kusaidiana ni silaha kubwa sana katika maendeleo yao, idadi yao ni ndogo hawavuki milioni lakini wanabebana sana pengine kuzidi hata wachaga.

Hawa shabaha yao kuu ya mafanukio wameilenga sehemu moja kwenye biashara, kwenye elimu bado wanajikongoja lakini main focus wameweka kwenye biashara na kiukweli biashara zimebadili maisha yao.

Nchini China katika jiji la Ghuangzhou wakinga ndio watanzania waliojazana zaidi mpaka wana mitaa yao, ni jiji kubwa la kibiashara lenye viwanda vingi na kuna bandari kubwa ya kusafirisha mizigo, wakinga wa huko huwa wanashughulika na kutafuta bidhaa nzuri viwandani kisha wanasafirisha kwa meli ziwafikie ndugu zao wa huku, hata ikitokea kuna bidhaa kama kiatu kinauzwa sana hapa nchini basi kitasafirishwa kwa ndege kiwafikie ndugu zao wa huko wakipeleka kwa wachina watengeneze vingi na kuvisafirisha haraka vifike hapa kwetu wapige pesa, wana kampuni maarufu ya kusafirisha bidhaa kutoka China hadi hapa kwetu inaitwa Mapembelo Cargo, hilo neno Mapembelo ni salamu yao ya kilugha.

Silaha yao kubwa ni kuuza kwa bei ndogo, ndugu zao wa huko China wanahusika sana hapa kwa kupeana connection za machimbo ya huko China yenye bei za chini, kampuni ya kusfirisha bidhaa zao nayo inapunguza gharama, pia na wao hawanaga tamaa za faida kubwa nayo hii inasaidia sana gharama kuwa ndogo. hii mbinu ya kuuza kwa bei ndogo ndio iliwafanya hata wapemba na wachaga kupungua pale Kariakoo, ni ngumu kushindana na mtu anaeuza bidhaa hio hio au yenye ubora zaidi kwa bei chee, ni ngumu sana!

Mwamko wa biashara kwa wakinga wengi ulianza miaka ya 2000 lakini ndani ya muda mfupi maendeleo yao ni mithiri ya spidi ya radi.

Masoko waliyoteka ni soko la kuu la Kariakoo pamoja na mikoa ya nyanda za juu kusini. Kwa Dar wamejaa kwenye soko la Kariakoo ambalo ni soko mama na kubwa kuzidi yote nchini, wafanyabiashara wengi wenye maduka Dar, mikoani na wale wa nchi za Malawi, Zambia, Congo, Rwanda na Burundi wanajumua mizigo yao katika soko hili. Kariakoo si ajabu kwenye maduka 10 kuyakuta 6 yana wakinga, soko hili hapo zamani walijaa wachaga na wapemba hapa lakini kwa sasa hali ni tofauti, wakinga wamejazana na ndio wanaongoza kwa uwakilishi. Pia wanamiliki maghorofa mengi hapo Kariakoo.

Ukiachana na kariakoo, wameweza kuuteka kibiashara ukanda wa nyanda za juu kusini kwenye miji mikubwa ya mikoa ya Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe, Ruvuma..

wenye chuki na wivu wa maendeleo hawakosekani, waliwahi kusambaza uchungu wao kwa wachaga kwa kuwaita ni majambazi na matapeli, hivi sasa wamehamia kwa wakinga kuwaita ni wachawi, yani kuna watu hawafurahii hata kidogo maendeleo ya wengine, naweza kusema hayo mambo hata kama yapo ni kwa wachache waliofanya maamuzi yao binafsi, na hata kama ingekuwa uchawi unategemewa basi kwanini waganga walioshika huu uchawi hali zao ni duni ? Kwanini makabila yanayosifika kwa uchawi hali zao ni duni, wanashindwaje kutumia matunguli yao waroge biashara ziwape maendeleo ?

Wapemba -

🎯Biashara
🎯Kubebana

Hawa nao kubebana na kusaidiana ni silaha kubwa sana katika maendeleo yao, kwa mara nyingine tunaona jinsi umoja ulivyo na nguvu

Kwenye swala la elimu huko Pemba wapo chini sana ni mkoa unashika namba ya mwisho miaka nenda rudi lakini kwenye biashara wapo mbali sana, mafanikio waliyonayo ni kuzidi hata ya wasomi wengi wanaopokea mishahara mirefu, connection walizonazo na ndugu zao waliojazana nchi za nje nyingi zinawabeba pia.

Wahaya -

🎯Elimu

katika swala la akili za darasani ni kama walizidishiwa 😂, mkoani kwao mazingira ya elimu yapo chini lakini bado wanafaulu, ilifikia kipindi serikali iliongeza alama za ufaulu kwa mkoa wa kagera maana watu walikuwa wanafaulu kama vile wanakunywa maji.

Elimu inawabeba na inawapa sifa za kuajiriwa sehemu nyingi,

Maofisini katika kila watumishi 10 si ajabu utamkuta mhaya angalau mmoja na hii idadi imepunguzwa sana, miaka ya nyuma ilishazoeleka maofisin kujaa wahaya na makabila machache yaliyokuwa na wasomi kama wachaga. Sikuhizi uwanja umebadilika kwasababu elimu imesambaa kuna shule nyingi za serikali + private, tuisheni, upatikanaji rahisi wa vitabu, ufaulu umekuwa mkubwa, n.k. hali hii imefanya kuwe na wasomi kibao karibu kila kabila, maofisini hata wamasai wapo. pia kwa sasa wizara ndio inasimamia zoezi la ajira sio kama zamani bosi wa shirika unamkuta ni mhaya au mchaga anarundika wenzake. ubaya ni kwamba wahaya wengi hawana mlango wa pili (plan b), wana uwezo mkubwa darasani wa kuwafanya wapate sifa za kujirika (zamani ilikuwa ni uhakika wa ajira) lakini sasa nje yah apo kujiongeza hata kwenye biashara ni wazito.

Kubebana bado wapo kiwango cha chini, naweza kusema kubebana kupo sana makabila ya kibiashara kwenye kuchangiana mitaji lakini huku kwengine sio kivile.

Wasukuma -

🎯Elimu

Wasukuma ndio kabila lenye watu wengi kwenye hii nchi, wapo takribani milioni 12, idadi yao ni kubwa sana na ilibidi iwabebe lakini tatizo lao kubwa ni kwamba wana ushirikiano mdogo, laiti wasukuma wangekuwa na muungano hakuna kabila lingewafikia hata nusu ya maenddeleo yao.

Any way kwa wasukuma bado idadi yao kubwa inawabeba, katika hii idadi kuna koo zimeelimika na kuliweka kabila kwenye ramani,

Pia hujishughulisha na shughuli za uchumbaji mdogo wa dhahabu na kilimo japo ni kiwango cha kawaida.

Kuzaliana kwa sana kumekuwa ni tatizo kubwa.
 
Wachaga - Yes, kibiashara hawa jamaa ni wamejaa pia kwenye elimu tangu zamani mkoa wao ndio unaongoza kwa kuwa na shule nyingi, ni kabila la pili kwa wingi, utamaduni wao wa kubebana umekuwa ni moja kati ya silaha yao kuu, Marehemu mzee Mengi aliwahi huwa tajiri pekee mwenye asili ya Tanzania aliekuwemo kwenye orodha ya matajiri 10 wa Tanzania.. Kabila hili lina utofauti wa kipekee katika maendeleo kwa kufanya mandeleo vijijini kwao hasa katika ujenzi na uboreshaji wa makazi, wana utamaduni wa kipekee wa kurudi vijijini kwa pamoja ikifika krismas, huko hutambulisha watoto kwa ndugu zao, kupanga mipango, kuchangiana mitaji, kudumisha mila na desturi za kichaga, n.k.

Wakinga - hawa wamejikita zaidi kwenye biashara, hata wakiajiriwa si ajabu kuizacha ajira wakishapata mtaji. na wamefanikiwa kupindua meza, soko kuu la kimataifa la Kariakoo ndio wanaongoza kwa kabila la wafanyabiashara wengi, zamani soko hilo lilijaa wachaga na wapemba lakini kwa sasa wakinga wamepindua meza kwa kuongeza ushindani wa kuuza vitu kwa faida ndogo na bei ndogo. Nje ya Dar sehemu walizokamata kwa sana ni mikoa ya nyanda za juu kusini Mbeya, Songwe, Iiringa, Njombe, Iringa. Kwa idadi yao ndogo wasiyozidi hata watu laki 6 haya wanayofanya ni makubwa/ wameyakamata vilivyo.

Wapemba - Kwenye swala la elimu huko Pemba wapo chini sana ni mkoa unashika namba ya mwisho miaka nenda rudi lakini kwenye biashara wapo mbali sana na kuwa na mafanikio kuzidi hata ya wasomi wengi wanaopokea mishahara ya milioni. Huko kigamboni wamejazana tele.

Wahaya - Ok, sasa tunakuja kwenye makabila ya wasomi, wasomi wanaotegemea mishahara, kiukweli katika swala la akili za darasani hawa jamaa wapo juu, mkoani kwao mazingira ya elimu yapo chini lakini bado wanatoboa kielimu.

Tatizo linapokuja kwa mhaya ni kwamba zama zimebadilika, hio elimu siku hizi imesambaa mno karibu kila kabila siku hizi kuna wahitimu wa vyuo katika fani mbali mbali wenye sifa za kuajiriwa, sio kama zamani tena! sikuhizi wizara ya utumishi ndio inasimamia zoezi la ajira sio kama zamani kwamba bosi wa shirika au taasisi unamkuta ni mhaya au mchaga anajaza wenzake, Mambo yamebadilika!! Kwa mchaga ana mlango wa pili wa biashara lakini hapa kwa mhaya unakuta narudi kwao huko kijijini akikosa ajira.

Wasukuma - Hawa ndio wanaongoza kwa kuwa na watu wengi hii nchi, wapo takribani milioni 12, idadi yao ya kuwa wengi ilibidi iwabebe lakini sijui hata inakuwaje wapo chini huku, any way kwa wasukuma nao kwa vile idadi ni kubwa nao wamo wamo kwenye elimu, kwenye biashara za migodi namo wapo sana sana kama wachimbaji wanaojitegemea.
Wasukuma/nyamwezi ni 15m population.
 
Heshima kwa wachaga.

Mimi sio mchaga lakini huwa nikifika kwenye hii miji midogo midogo inayoibukia kwenye fursa, moja ya kigezo ninachotumia kwenye kubaini uwepo wa fursa za kibiashara ni uwepo wa wachaga.

Kama mji wa kibiashara hauna wachaga, hapo napaangalia mara mbili mbili.
 
Wachaga - Yes, kibiashara hawa jamaa ni wamejaa pia kwenye elimu tangu zamani mkoa wao ndio unaongoza kwa kuwa na shule nyingi, ni kabila la pili kwa wingi, utamaduni wao wa kubebana umekuwa ni moja kati ya silaha yao kuu, Marehemu mzee Mengi aliwahi huwa tajiri pekee mwenye asili ya Tanzania aliekuwemo kwenye orodha ya matajiri 10 wa Tanzania.. Kabila hili lina utofauti wa kipekee katika maendeleo kwa kufanya mandeleo vijijini kwao hasa katika ujenzi na uboreshaji wa makazi, wana utamaduni wa kipekee wa kurudi vijijini kwa pamoja ikifika krismas, huko hutambulisha watoto kwa ndugu zao, kupanga mipango, kuchangiana mitaji, kudumisha mila na desturi za kichaga, n.k.

Wakinga - hawa wamejikita zaidi kwenye biashara, hata wakiajiriwa si ajabu kuizacha ajira wakishapata mtaji. na wamefanikiwa kupindua meza, soko kuu la kimataifa la Kariakoo ndio wanaongoza kwa kabila la wafanyabiashara wengi, zamani soko hilo lilijaa wachaga na wapemba lakini kwa sasa wakinga wamepindua meza kwa kuongeza ushindani wa kuuza vitu kwa faida ndogo na bei ndogo. Nje ya Dar sehemu walizokamata kwa sana ni mikoa ya nyanda za juu kusini Mbeya, Songwe, Iiringa, Njombe, Iringa. Kwa idadi yao ndogo wasiyozidi hata watu laki 6 haya wanayofanya ni makubwa/ wameyakamata vilivyo.

Wapemba - Kwenye swala la elimu huko Pemba wapo chini sana ni mkoa unashika namba ya mwisho miaka nenda rudi lakini kwenye biashara wapo mbali sana na kuwa na mafanikio kuzidi hata ya wasomi wengi wanaopokea mishahara ya milioni. Huko kigamboni wamejazana tele.

Wahaya - Ok, sasa tunakuja kwenye makabila ya wasomi, wasomi wanaotegemea mishahara, kiukweli katika swala la akili za darasani hawa jamaa wapo juu, mkoani kwao mazingira ya elimu yapo chini lakini bado wanatoboa kielimu.

Tatizo linapokuja kwa mhaya ni kwamba zama zimebadilika, hio elimu siku hizi imesambaa mno karibu kila kabila siku hizi kuna wahitimu wa vyuo katika fani mbali mbali wenye sifa za kuajiriwa, sio kama zamani tena! sikuhizi wizara ya utumishi ndio inasimamia zoezi la ajira sio kama zamani kwamba bosi wa shirika au taasisi unamkuta ni mhaya au mchaga anajaza wenzake, Mambo yamebadilika!! Kwa mchaga ana mlango wa pili wa biashara lakini hapa kwa mhaya unakuta narudi kwao huko kijijini akikosa ajira.

Wasukuma - Hawa ndio wanaongoza kwa kuwa na watu wengi hii nchi, wapo takribani milioni 12, idadi yao ya kuwa wengi ilibidi iwabebe lakini sijui hata inakuwaje wapo chini huku, any way kwa wasukuma nao kwa vile idadi ni kubwa nao wamo wamo kwenye elimu, kwenye biashara za migodi namo wapo sana sana kama wachimbaji wanaojitegemea.
wamakonde na wangoni watakuj kuanzisha vita mda c mref
 
Wachaga - Yes, kibiashara hawa jamaa ni wamejaa pia kwenye elimu tangu zamani mkoa wao ndio unaongoza kwa kuwa na shule nyingi, ni kabila la pili kwa wingi, utamaduni wao wa kubebana umekuwa ni moja kati ya silaha yao kuu, Marehemu mzee Mengi aliwahi huwa tajiri pekee mwenye asili ya Tanzania aliekuwemo kwenye orodha ya matajiri 10 wa Tanzania.. Kabila hili lina utofauti wa kipekee katika maendeleo kwa kufanya mandeleo vijijini kwao hasa katika ujenzi na uboreshaji wa makazi, wana utamaduni wa kipekee wa kurudi vijijini kwa pamoja ikifika krismas, huko hutambulisha watoto kwa ndugu zao, kupanga mipango, kuchangiana mitaji, kudumisha mila na desturi za kichaga, n.k.

Wakinga - hawa wamejikita zaidi kwenye biashara, hata wakiajiriwa si ajabu kuizacha ajira wakishapata mtaji. na wamefanikiwa kupindua meza, soko kuu la kimataifa la Kariakoo ndio wanaongoza kwa kabila la wafanyabiashara wengi, zamani soko hilo lilijaa wachaga na wapemba lakini kwa sasa wakinga wamepindua meza kwa kuongeza ushindani wa kuuza vitu kwa faida ndogo na bei ndogo. Nje ya Dar sehemu walizokamata kwa sana ni mikoa ya nyanda za juu kusini Mbeya, Songwe, Iiringa, Njombe, Iringa. Kwa idadi yao ndogo wasiyozidi hata watu laki 6 haya wanayofanya ni makubwa/ wameyakamata vilivyo.

Wapemba - Kwenye swala la elimu huko Pemba wapo chini sana ni mkoa unashika namba ya mwisho miaka nenda rudi lakini kwenye biashara wapo mbali sana na kuwa na mafanikio kuzidi hata ya wasomi wengi wanaopokea mishahara ya milioni. Huko kigamboni wamejazana tele.

Wahaya - Ok, sasa tunakuja kwenye makabila ya wasomi, wasomi wanaotegemea mishahara, kiukweli katika swala la akili za darasani hawa jamaa wapo juu, mkoani kwao mazingira ya elimu yapo chini lakini bado wanatoboa kielimu.

Tatizo linapokuja kwa mhaya ni kwamba zama zimebadilika, hio elimu siku hizi imesambaa mno karibu kila kabila siku hizi kuna wahitimu wa vyuo katika fani mbali mbali wenye sifa za kuajiriwa, sio kama zamani tena! sikuhizi wizara ya utumishi ndio inasimamia zoezi la ajira sio kama zamani kwamba bosi wa shirika au taasisi unamkuta ni mhaya au mchaga anajaza wenzake, Mambo yamebadilika!! Kwa mchaga ana mlango wa pili wa biashara lakini hapa kwa mhaya unakuta narudi kwao huko kijijini akikosa ajira.

Wasukuma - Hawa ndio wanaongoza kwa kuwa na watu wengi hii nchi, wapo takribani milioni 12, idadi yao ya kuwa wengi ilibidi iwabebe lakini sijui hata inakuwaje wapo chini huku, any way kwa wasukuma nao kwa vile idadi ni kubwa nao wamo wamo kwenye elimu, kwenye biashara za migodi namo wapo sana sana kama wachimbaji wanaojitegemea.
Ukiniambia kabila lenye mafanikio Kanda ya ziwa ntakuambia wakurya, wahaya na wasukuma hawamfikii mkurya
 
Wachaga - Yes, kibiashara hawa jamaa ni wamejaa na ndio iliowapa mafanikio makubwa, lakini pia kielimu wapo juu maana mkoa wao unaongozea kwa kuwa na shule nyingi tangu zamani hivyo kuwafanya wapate fursa za ajira na vyeo, utamaduni wao wa kubebana umekuwa ni moja kati ya silaha yao kuu kuwaweka hii nafasi ya juu, hata Marehemu mzee Mengi alisoma mpaka nje kwa kubebwa na akawa muhasibu wa kwanza nchini (cpa) ila hakuishia hapo akawa mfanyabiashara mkubwa aliebeba wengine, alikuwa ni tajiri haswa kiasi kwamba aliweza kuwa mtanzania wa asili aliekuwemo kwenye orodha ya matajiri 10 wa Tanzania..

Kabila hili lina utofauti wa kipekee katika maendelea, hawaishii kuwa na maendeleo ugenini pekee bali hufanya mandeleo mpaka vijijini kwao hasa katika ujenzi na uboreshaji wa makazi, pia wana utamaduni wa kurudi makwao huko vijijini kwa pamoja kila mwisho wa mwaka, kurudi hukukwa pamoja hutoa fursa kuinuana kwa kuchangiana mitaji, kupanga mipango ya pamoja, kutambulisha watoto kwa ndugu zao, kudumisha mila na desturi za kichaga, n.k.

Wakinga - hawa wamejikita zaidi kwenye biashara, hata wakiajiriwa si ajabu kuizacha ajira wakishapata mtaji. na wamefanikiwa kupindua meza, soko kuu la kimataifa la Kariakoo ndio wanaongoza kwa kabila la wafanyabiashara wengi, zamani soko hilo lilijaa wachaga na wapemba lakini kwa sasa wakinga wamepindua meza kwa kuongeza ushindani wa kuuza vitu kwa faida ndogo na bei ndogo. Nje ya Dar sehemu walizokamata kwa sana ni mikoa ya nyanda za juu kusini Mbeya, Songwe, Iiringa, Njombe, Iringa. Kwa idadi yao ndogo wasiyozidi hata watu laki 6 haya wanayofanya ni makubwa/ wameyakamata vilivyo.

Wapemba - Kwenye swala la elimu huko Pemba wapo chini sana ni mkoa unashika namba ya mwisho miaka nenda rudi lakini kwenye biashara wapo mbali sana na kuwa na mafanikio kuzidi hata ya wasomi wengi wanaopokea mishahara ya milioni. Huko kigamboni wamejazana tele.

Wahaya - Ok, sasa tunakuja kwenye makabila ya wasomi, wasomi wanaotegemea mishahara, kiukweli katika swala la akili za darasani hawa jamaa wapo juu, mkoani kwao mazingira ya elimu yapo chini lakini bado wanatoboa kielimu.

Tatizo linapokuja kwa mhaya ni kwamba zama zimebadilika, hio elimu siku hizi imesambaa mno karibu kila kabila siku hizi kuna wahitimu wa vyuo katika fani mbali mbali wenye sifa za kuajiriwa, sio kama zamani tena! sikuhizi wizara ya utumishi ndio inasimamia zoezi la ajira sio kama zamani kwamba bosi wa shirika au taasisi unamkuta ni mhaya au mchaga anajaza wenzake, Mambo yamebadilika!! Kwa mchaga ana mlango wa pili wa biashara lakini hapa kwa mhaya unakuta narudi kwao huko kijijini akikosa ajira.

Wasukuma - Hawa ndio wanaongoza kwa kuwa na watu wengi hii nchi, wapo takribani milioni 12, idadi yao ya kuwa wengi ilibidi iwabebe lakini sijui hata inakuwaje wapo chini huku, any way kwa wasukuma nao kwa vile idadi ni kubwa nao wamo wamo kwenye elimu, kwenye biashara za migodi namo wapo sana sana kama wachimbaji wanaojitegemea.
Unajitekenya ili ucheke siyo? Ondoa huu upupu wako uliojaa hisia na uwongo. No research no right to speak. Huu utafiti umeufanya wapi. Wachaga mnapenda sana makuu peleka hizi sifa za uwongo na kijinga Kenya siyo hapa kwetu
 
Haya ndio makabila yenye wsomi wengi na yaliyoogopwa sana na Mwalimu nyerere.

1. Wachagga.
2. Wanyakyusa.
3.wahaya.

Wakinga.
Wapare.
Wahaya.....

Hawa ndio wanao fuata.

"Lakini kazi Moja ya makabila iliyobaki ni kutambika unataka kutambika?????
KARNE ya 21 Unamzungumzia ukabira".
JULIUS NYERERE.
 
Haya ndio makabila yenye wsomi wengi na yaliyoogopwa sana na Mwalimu nyerere.

1. Wachagga.
2. Wanyakyusa.
3.wahaya.

Wakinga.
Wapare.
Wahaya.....

Hawa ndio wanao fuata.

"Lakini kazi Moja ya makabila iliyobaki ni kutambika unataka kutambika?????
KARNE ya 21 Unamzungumzia ukabira".
JULIUS NYERERE.
Zama zimebadilika, zamani makabila machache yalikuwa na wasomi, kwa sasa karibu kila kabila kuna wasomi wa fani mbali mbali.

Kwa sasa game limebadilika, waanyabiashara ndio wameshikilia usukani
 
Unajitekenya ili ucheke siyo? Ondoa huu upupu wako uliojaa hisia na uwongo. No research no right to speak. Huu utafiti umeufanya wapi. Wachaga mnapenda sana makuu peleka hizi sifa za uwongo na kijinga Kenya siyo hapa kwetu
Ni kipi nimedanganya hapa ?

1. Mkoa wanaotoka wachaga hauongozi kwa shule nyingi ?
2. Mengi hakuwa tajiri pekee list ya top 10 mwenye asili ya Tz?
3. Wachaga sio kabila pekee wanalorudi pamoja kila mwisho wa mwaka?
4. Wachaga sio kabila linaloongoza kwa kuendeleza makwao ?
 
Sasa wasukuma wanamaendeleo gani
Wewe kabila lako lina maendeleo gani, au kuuza duka la rejareja naww unakuwa mfanyabiashara mkubwa, acha kushindana na msukuma kenge wewe, wakitoka wahindi na waarabu wanaofuata kwa ukwasi hapa Tanzania ila hawana kelele za kipimbi hakuna kabila lingine bali ni wasukuma.
 
Back
Top Bottom