2024 Africa Cup Of Nations (AFCON) | Special Thread. Mechi ya fainali, FT: Nigeria 1 - 2 Ivory Coast. Ivory coast abeba ubingwa. 11.02. 2024

Yule jamaa ni mtu na nusu, mimi ndo mchezaji wangu bora kutoka africa nayemkubali kwa sasa akifuatiwa na Fundi la mafundi kiboko ya Arsenal Mheshimiwa Mohammed Salah
Umeharibu kuweka mahaba, huyo Salah alifanya nini cha maana? Alipata a clear chance akambwela mpaka mwenzie alipouchukua mpira kiufundi akafunga lile goli la kwanza…

Au ndio ile penalty ambayo hata hivyo kipa aliigusa?
Kwenye mijadala ya miamba iliyofanya vizuri uweke mahaba pembeni.
 
Onana akiwa katika ndege binafsi akielekea Ivory Coast kwenye AFCONView attachment 2872312
Ama kweli upele humuota asiye na kucha. Pesa zote hizo amevaa kama homeless.
Ameichafua hiyo PJ yenyewe kali kinoma.

Unaweza kuvaa mavazi ya gharama ila ukaonekana kituko, taste ya mavazi ni kipaji.
Natamani siku tujadili wachezaji wakali wa fashion...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…