4 Fortuner VS Discovery 4 tuagize kutoka Africa ya Kusini au Singapore?

Ukitaka kuagiza, agiza popote, kodi ya TRA haiangalii nchi inayotoka, kodi ni ile ile isipokua tu kama unaagiza South Africa na unataka unafuu wa kodi basi gari lazima iwe brand new, hapo kodi itakua kidogo sana. Kwa maana nyingine hutalipa import duty kwa sababu ya mikataba ya SADC. Gari iwe mpya zero kilomita.

Nizungumzie Toyota Fortuner isiyozidi miaka 3, hapa CIF haipungui dollar 💰 40,000 sawa na tzs 100m hivi, jumla na kodi yake na makorokoro mengine andaa +- 120m hivi.

Matengenezo, gari za Toyota zinajulikana na kuaminika ulimwengu kote kwa kuwa na roho ya paka, kudumu muda mrefu na gharama kidogo za matengenezo.

Binafsi, I would Prefer Toyota Fortuner.

Tathmini na utafiti wa consumers report Duniani kote, Magari ya Land Rover kwenye category ya Reliability hua yanashika mkia.
 
Singapore gari zao hua wanakua na tabia ya kubadili baadhi ya vitu na kuweka vyenye damage au visivyokuwa na ubora.
Ukitaka uenjoy zaidi, nenda Sauzi mwenyewe uikague gari na kuridhika nayo. Kingine hakuna freight cost kama ambavyo ipo kama ukiagiza kutoka Singapore. Kingine na cha mwisho, fortuner ina muonekano mzuri sana na pia upate engine either ya 1GD-FTV 2.8L au 2GD-FTV 2.4L. utaenjoy sana maisha. Ina perfomance nzuri na mwendo sio wa kitoto
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…