zilindeni mali zenu kwa kutoa sadaka hii ni secret code matajiri wa wanafanya,niliwahi kufanya kazi kwenye moja ya familia za kitajiri hapa Tz.jamaa wanatoa sana sadaka makampuni yao yana watu wasipungua 10k ,lakini wanaweza watembezea pesa na mazaga kibao kipindi cha mfungo,bado watu baki nje huko.
Sadaka toeni kwa wahitaji sio unapeleka kunua maji kwa wachungaji,December hii peleka kalamu,daftari ,unga charity center kuna malaika kibao pale hawana dhambi na baraka /dua/maombi yao yanafika haraka.
Saidia wazazi wako,kuna ndugu yetu alipatwa na maruhani/mapepo/majini hyo siku tuliambiwa ndugu wote tukutane ili kujua anasaidiwa vipi yle mashetani yakawa yanampa kila mmoja changamoto zake .kila mtu alikili ni kweli anazo hizo shida ingawa hatukuwa tunaambizana Majini yale yalimtaka awe mganga so tukasema ngoja tuone kweli yaliyomo yamo
ikafika kwangu moja ya mambo niliambiwa kuwa mimi sipendi kutoa sadaka kiufupi nina mkono wa birika ,madude yale yakasema mama yako humpi fungu lolote kutoa kwenye kipato chako nikawambia nina ishi nae kwa hyo anapata huduma zote kama watu wangu wengine,ila nikaambiwa lazima nitenge fungu la kwake ili vimeo vyangu vikawe sawa na kweli kipindi hicho nilikua na vimeo kinoa
Pili niliambiwa laima niwe msiri kwenye mambo yangu ,ukweli nilipata kazi part time sehemu ila iliishia kwenye mkataba hata kazi sikuwahi kufanya na yule mwenye ile kazi alikua ananihusudu sana ila sasa hata simu nikimpigia hapokei ,nadhani nilitangaza kwa watu nimepata part time job kwa hyo itaniongeza niboost salary yangu kwa kuwa na kazi 2
Mavitu yake yakaniambia kuna mtu niliambiwa kwa code usichangamane nae ana roho flani hivi ukimshirikisha mambo hutoboi na kweli hyo jamaa nilikuaga nashare mambo mengi ,baadaae kuna mambo yalitokea nikajua kumbe jamaa alikuaga ananichoma kwa maboss kidogo nipoteze tonge
Nadhani kwenye suala la utafutaji kuna vita kubwa sana tena unaweza chukulia rahisi lakini watu wanachoma sana mitaji ,kazini unaanza vizuri na hivi kazi za kibongo ni uchawa na kurogana ,utapiga kazi hata Vitz hununui na kipindi hicho wewe ndio mtu potential watu wanakufunika tu mtu flani wa maneno na kujikosha kwa maboss anapepea tu anabadili mandinga kudadeki