8/02/2015: Yanga vs Mtibwa match preview and live coverage

Yangaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
Ngasaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Mikia mvae miwani msione GERE!!!
 
Jukwaa limedorola kama nini! Mikia mko wapi jamani? Njooni huku tuchati. Tumewanyima raha tangu Jumatano, Jumamosi na Jumapili, poleni sana, hiyo ndiyo Young Africans Sports Club, bingwa wa kihistoria, wengine wasindikizaji tu kama kenge katika msafara wa mamba.
 

Mikia haiwezi kujitokeza humu hasa ukizingatia timu ya wananchi imefanya mambo makubwa leo!!!! Ahsante uncle Ngassa kwa kuitimua mikia humu jakwaani.
 
mikelele miiingi,laleni basi mtashangilia na kesho

Wewe sepa tu, wala usiendelee kuchunguliachungulia hapa jukwaani, wiki hii imekuwa shubiri kwenu. Huu ni mwanzo tu, leo limetengenezwa gap la point 8 kati yetu na ninyi. Sijui mtalifutaje hili gap, mikia nywiiiiiii!
 
Kwa niaba ya wana Yanga wote, tunatoa pole kwa mikia mliokuja Taifa kujiandaa kuishangilia Mtibwa sugar, na kuizomea Yanga.

Tunatoa pole kwa mikia ya hapa jukwaani,waliokuwa wanatubeza toka jana, kuhusu Mtibwa, ila wameshuhudia kiama.

Tunatoa pole kwa mikia ambao bundle wananunua wenyewe, lakini ni Yanga ndio wanawaamuru jinsi ya kuitumia na kuingia jukwaa hili.

Tunatoa pole ya dhati kwa yeyote aliyenuna siku ya leo, kwa ushindi wa Yanga, pole kwa wewe unayechungulia tu nyuzi za game ya leo.

Tulianza na Mungu tutamaliza na Mungu.
 
Goooooool! Ngasa Anaongeza La Tatu hapa, ala kumbe gemu ishaisha.
 

Amina. Mkuu Bantu lady imetosha, tuishie hapa.
 
Last edited by a moderator:
Nachukua fursa hii kuwapongeza yanga kwa dhati kwa ushindi waliopata katika mechi mbili zilizopita.Wote tunajua ligi ni ngumu na bado tofauti ya point sio ya kutabiri bingwa....Hii ni changamoto kwa timu yangu ya Simba kuona ni kipi kinachoweza kufanyika ili katika mechi zijazo performance iwe afueni....Otherwise mpira ni upendo,furaha,Amani Makoye Matale Bantu lady Masuke Amavubi grafani11 sembo
 
Last edited by a moderator:

Asante sana Mkuu.
 

Ahsantee mkuu Freeland, niulizie nimeona sehemu eti Masuke ni Yanga. Ila usinitaje mimi nimesoma tu sehemu... simooo
 
Last edited by a moderator:
Kikosi cha yanga leo; 1. Barthez, 2.Twite, 3.Edward charles, 4.Rajabu zahir, 5.cannavaro, 6. Telela, 7.msuva, 8.Niyonzima, 9.Sherman, 10. Tambwe, 11. coutinho. SUB-Ngassa, javu, tegete, mrwanda, alphonce(kipa)
Huyu golikipa Alphonce katokea wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…