A day in the Buddhist college

A day in the Buddhist college

Mkuu kama hutojali toa darasa dogo kuhusu meditation,maana walimu wamekuwa wengi mpaka tumechanganyikiwa.

Mbaya walimu wenyewe ni wa theory tu,hawajasomea wala kupractice sana.

Nimeshakutag kule kwenye ile post fuatalia tafadhali
 
Mkuu mshana jr Kama utabalikiwa tunaomba uendelee na somo

Sante 😉
 
Last edited by a moderator:
Sijaambulia kitu kaka,uzi nimeupitia kama vile sijaridhika.

Rudia tu naona wadau wameshaongezeka.

Yeah hata mimi nimegundua kuwa hauwezi kujibu swali lako, subiri kesho nitafanya hivyo mambo yaliingiliana kidogo
 
Kwakweli kilichotufanya tutoroke si kingine bali ni starehe na ile ego ya mienendo ya kibinadamu ya kutaka kwenda kinyume na mazoea
Sehemu maarufu tuliyokuwa tunaenda ilikuwa inaitwa Sambhonani, club ya weusi na iliyokuwa na kila aina ya vurugu na nyingine ilikuwa inaitwa Zithobeni hii ilikuwa kama km 6 hivi kutoka mjini bronkohorspruit, huko walikuwa wanakaa weusi tupu
Tuliogopeka mno na Jamii ya wazulu kwakuwa chuo chetu kilichukuliwa kama sehemu ya kufundisha uchawi ushirikina na mambo ya kishetani
Hii yote ilitokana na vile tulivyokuwa tunavaa (kanzu nyeusi) na hizo nguo za kichina pichani, ibada za kuabudu sanamu, chanting, kunyoa vipara muda wote na mambo mengine mengi tuu
Kwahiyo ilikuwa tukiwa kwenye hizo bar tuliogopeka mno
Siku moja tukiwa club ikatokea vurugu kubwa hasa, na kabla hatujaweza kuchomoka police wakawa washatake cover mlango mkuu na hapo maana yake kila atakayekamatwa ni selo.
Nitaendelea......
 
Kwakweli kilichotufanya tutoroke si kingine bali ni starehe na ile ego ya mienendo ya kibinadamu ya kutaka kwenda kinyume na mazoea
Sehemu maarufu tuliyokuwa tunaenda ilikuwa inaitwa Sambhonani, club ya weusi na iliyokuwa na kila aina ya vurugu na nyingine ilikuwa inaitwa Zithobeni hii ilikuwa kama km 6 hivi kutoka mjini bronkohorspruit, huko walikuwa wanakaa weusi tupu
Tuliogopeka mno na Jamii ya wazulu kwakuwa chuo chetu kilichukuliwa kama sehemu ya kufundisha uchawi ushirikina na mambo ya kishetani
Hii yote ilitokana na vile tulivyokuwa tunavaa (kanzu nyeusi) na hizo nguo za kichina pichani, ibada za kuabudu sanamu, chanting, kunyoa vipara muda wote na mambo mengine mengi tuu
Kwahiyo ilikuwa tukiwa kwenye hizo bar tuliogopeka mno
Siku moja tukiwa club ikatokea vurugu kubwa hasa, na kabla hatujaweza kuchomoka police wakawa washatake cover mlango mkuu na hapo maana yake kila atakayekamatwa ni selo.
Nitaendelea......

saa ngapi au kesho tenants?
 
saa ngapi au kesho tenants?

Kwenda selo haikuwa ishu sana ishu ni kwamba hatukuwahi na documents zozote kama passport nk kwakuwa kila kitu kilikuwa kinashikiliwa na uongozi wa chuo
Hivyo ikabidi kila mtu afe kivyake asikamatwe, jamaa yetu mmoja walivamia choo akajifanya ni mhudumu wa choo, akalivagaa sink na kinyesi chake mzungu akamuacha wawili waliruka ukuta lakini walikatwa vibaya sana na vioo vile vinavyochomekwa juu ya ukuta lakini wakasalimika, mimi niliingia kwenye pipa la maji lililokuwa na Maji nusu....imagine baridi ya South halafu uzame kwenye pipa la maji baridi
Hali ilipotulia tuliondoka salama lakini nikiwa natetemeka hasa kwa baridi na mwenzangu akiwa ananuka kinyesi tupu, wale wenzetu wawili walifika mapema na wanaingia salama bwenini nasisi pia vilevile, tuliwatibia usiku ule ili damu ikate asubuhi wawe parade bila mabandage..ni kitu kigumu mno lakini walihimili
 
Visa vya kutoroka vilikuwa vingi na kwakweli viliwapoteza ndugu zetu kadhaa, Charles yeye alipigwa na waabudu shetani mpaka wakamuua tena mtaani, Omolo yeye alikuwa disco Pretoria akatongoza demu wa mtu, jamaa wakamsubiri alipoenda kukisaidia wakampiga huko vibaya sana alikuja kufariki baadae, kapinga yeye alikufa miaka ya karibuni lakini yeye habari yake ni ndefu ikimhusisha mwanamke wa kizulu aliyekuwa anaishi naye
Kwa kufupi wanawake wa kizulu hawana staha na sehemu zao za siri ubaguzi umewaathiri mno, kwao kumvulia yeyote chupi sio ishu ndio maana mauaji ya mapenzi na magonjwa yapo kwa kiwango cha juu mno south
Mbaya zaidi wanapenda sana wageni hivyo mara kwa mara kunakuwa na migongano kati ya wageni na wenyeji kuhusiana na swala la mapenzi
 
Visa vya kutoroka vilikuwa vingi na kwakweli viliwapoteza ndugu zetu kadhaa, Charles yeye alipigwa na waabudu shetani mpaka wakamuua tena mtaani, Omolo yeye alikuwa disco Pretoria akatongoza demu wa mtu, jamaa wakamsubiri alipoenda kukisaidia wakampiga huko vibaya sana alikuja kufariki baadae, kapinga yeye alikufa miaka ya karibuni lakini yeye habari yake ni ndefu ikimhusisha mwanamke wa kizulu aliyekuwa anaishi naye
Kwa kufupi wanawake wa kizulu hawana staha na sehemu zao za siri ubaguzi umewaathiri mno, kwao kumvulia yeyote chupi sio ishu ndio maana mauaji ya mapenzi na magonjwa yapo kwa kiwango cha juu mno south
Mbaya zaidi wanapenda sana wageni hivyo mara kwa mara kunakuwa na migongano kati ya wageni na wenyeji kuhusiana na swala la mapenzi

duh !hatare kk
 
duh !hatare kk

Dah!Nimeipenda sana hii kitu.

Nilinusurika kifo mara nne
Naweza kukiri kwamba meditation, martial arts na mazingira ya chuo yalinijengea uwezo fulani wa nguvu fulani, nguvu zenye uwezo wa kukuepusha au kujua hatari ijayo
Leo hii ningekuwa marehemu niliyeoza siku nyingi sana lakini kw namna ya ajabu kabisa nikakikwepa kifo mara nne
mara ya kwanza kwanza kwenye chumba fulani mtaani self container nilitorokea dirisha la bafuni/chooni..wakati jamaa, wakivunja mlango ili waingie wanimalize
Mara ya pili ilikuwa ni kama kilometer tatu tu kutoka chuoni wakaniotea niliwazidi maarifa nikatoka nduki mbio ambazo nafikiri nilimzidi Bolt
Mara ya tatu ilikuwa sumu kwenye pombe, nikategesha chupa mdomoni kama sekunde tano, nikaishusha mezani nikasepa

Mara ya nne ilikuwa na mambo mengi sana
Nilitoka chuoni saa nne usiku nikiwa na bastola( nilikuja kununua silaha) na hii yote ilikuwa kwa ajili ya kujilinda, nikafika mpaka Sambonani kwaito likiwa ndio kwanza linakolea
Mtu niliyemfuata akanipa signal kuwa pale hapakuwa penyewe wale wagomvi wangu walikuwepo kwahiyo tukachukua tax kwenda Zithobeni km kama tano hivi toka pale mjini
Tukafika kwenye bar moja kubwa na ukumbi wa disco, sasa ukifika pale unakabidhi silaha mlangoni kisha unasachiwa ndio unaruhusiwa kuindia ndani, mimi silaha niliichomeka chini y kitovu na nikanuia jamaa wasiione kweli haikuonekana nikaingia
Tukiwa tunakunywa kwenye dimlights za ukumbini nikawaona wabaya wangu meza kama ya nne hivi, palepale yakanicheza, lakini wakati huohuo mmoja wao akaenda chooni
Nilikaa tayari kwa lolote, nikiwa nawaangalia jamaa niliona mmoja ananyanyua chupa, na umeme ukakatika nilimrukia mtu wangu tukaanguka chini, kilichofuatia ni kishindo cha chupa ukutani nilisikia upepo wakati inapita juu ya kichwa changu
 
Nilinusurika kifo mara nne
Naweza kukiri kwamba meditation, martial arts na mazingira ya chuo yalinijengea uwezo fulani wa nguvu fulani, nguvu zenye uwezo wa kukuepusha au kujua hatari ijayo
Leo hii ningekuwa marehemu niliyeoza siku nyingi sana lakini kw namna ya ajabu kabisa nikakikwepa kifo mara nne
mara ya kwanza kwanza kwenye chumba fulani mtaani self container nilitorokea dirisha la bafuni/chooni..wakati jamaa, wakivunja mlango ili waingie wanimalize
Mara ya pili ilikuwa ni kama kilometer tatu tu kutoka chuoni wakaniotea niliwazidi maarifa nikatoka nduki mbio ambazo nafikiri nilimzidi Bolt
Mara ya tatu ilikuwa sumu kwenye pombe, nikategesha chupa mdomoni kama sekunde tano, nikaishusha mezani nikasepa

Mara ya nne ilikuwa na mambo mengi sana
Nilitoka chuoni saa nne usiku nikiwa na bastola( nilikuja kununua silaha) na hii yote ilikuwa kwa ajili ya kujilinda, nikafika mpaka Sambonani kwaito likiwa ndio kwanza linakolea
Mtu niliyemfuata akanipa signal kuwa pale hapakuwa penyewe wale wagomvi wangu walikuwepo kwahiyo tukachukua tax kwenda Zithobeni km kama tano hivi toka pale mjini

Why ulikua unawindwa mkuu?
 
Why ulikua unawindwa mkuu?

.....niliponyanyuka pale chini silaha nikiwa nayo mkononi nilikimbia upande wa chooni huku watu wakigongana na kupiga kelele sana
Ndani ya dakika kumi nilikuwa nimesharuka ukuta niko mtaani kuku defender zenye mijibwa na polisi zikiwa zimeshatake cover pale ukumbini
Nilikimbia mtaa kwa mtaa lakini kwa nyuma umbali wa kilometer moja nilipopata tax iliyonipeleka Zithobeni B, pale ilikuwa ni A naumbali wake ilikuwa kama km 3 hv
Nilifika kule salama lakini nikakuta bar ha uswazi hasa yenye virugu zote
Pale nikampata kijana ambaye nilimnunulia bangi na pombe ya kienyeji kama gongo halafu nikamwomba anitafutie usafiri wa kwenda chuoni hiyo sasa ilikuwa saa saba usiku
Kila dereva aliyetajiwa chuo chetu aligoma kwenda palikuwa panaogopeka mno
Ilipofika saa nane usiku kilikuja kigari nissan dutsun mbele kikiwa na watu wawili lakini kwenye canopy kuko tupu
Yule kijana alienda akaongea nao cha ajabu wakakubali wakati ni kama wamekuja kwenye starehe tena kwa rand kumi tu mpaka chuoni
Nikapanda kwenye canopy kigari kikaondoshwa kwa kasi ya ajabu, mmh nikashtuka ...kunchungulia kwenye kioo nyuma ya cabin ni wale vijana wapambe wa wale wabaya wangu, nikajua nimekwisha
Tunaondoka Zithobeni B kuelekea A lakini tulipokaribia A ghafla mwelekeo ukabadilika kuelekea highway..nikajua leo ama zangu ama zao
Ile kutaka tu kuingia high way ikawa unakuja semi trailer ambapo ilibidi jamaa asimame ghafla la sivyo rungeishia palepale
Kitendo cha kusimama ghafla ndio kilinipa mwanya wa kufungua mlango wa canopy na kuruka,
 
Back
Top Bottom