A day in the Buddhist college

A day in the Buddhist college

Unawezaje kugundua nguvu zako zipoje?
Nataka niwe na teleporting abilities.

Nilikuwa nina uwezo wa kutabiri hatari Neema au chochote, lakini pia niliporudi Tanzania kuna siku nilienda kanisani na wakati naenda kukaa siti za mbele nilikuwa na kitu kama vibration wakati nawapita watu
Lakini pia nimeshasimulia sana hapa JF matukio mengi ya kuibiwa nk na waliofanya hivyo ikala kwao
 
Daaah!! hii ni thread ya kwanza ambayo nimesoma kila comment mwanzo mwisho...kiukweli nimebaki njia panda tuu maana sielewi elewi vinavyoongelewa,sometime nakuwa kama napata kinowledge flani hivi lakini sijui ni knowledge ipi,halafu nashangaa navutiwa kuendelea kusoma vitu ambavyo hata sivielewi...may be something happens nafsini mwangu..
mkuu mshana jr hivi mazingaombwe yapo category gani?? nipo interested sana na hii kitu,natamani nijue namna ya kufanya mazingaombwe.

Sio wewe tu ukishaanza kujifunza Buddhism unaanza kuona vitu katika mwanga tofauti na hivyo kukuvutia zaidi na zaidi kuendelea kujifunza
Binafsi baada ya Buddhism nilisoma conficious, Taoism Krishna consciousness na kidogo satanism
 
Last edited by a moderator:
Ubuddha kama dini ni mfumo wa maisha. Lakini ubuddha hasa ni kuishi kwa mwenendo na mwongozo wa 'Buddha'...

Buddha ni mwalimu na kiongozi wa namna/mafundisho/njia ya Buddha--Aliyepata kuishi wakati fulani na mahala fulani nyuma huko India. Buddha ni mtu aliyetaamulika na kufanya chachu ya kueneza na kusambaza uhalisia wa 'taamuli' katika mtu.

Mafundisho ya Buddha ni ndiyo yanafanya 'Dhamapada' -- njia ya Buddha, kwamba katika kila mtu kuna mpango timamu, kamili na wenye kheri lakini huwa hukadirika katika mtu 'mwenye wongofu' ama mwenye kuishi kadiri ya kufuta njia ya kati kati kuelekea 'wongofu kamili'.

Ndivyo basi ndivyo gurudumu la spoku nane la dhama ni kadiri idhihirishayo njia ya Buddha ilipatwa kufundishwa na mwenyewe Buddha, mwenyekheri sana, kama mwongozo kuelekea 'wokovu' ulikokatika ama ujao na mtu aliyetaamulika.

Kinyume na wokovu ni basi hali yote ya mtu kuwa katika ulimwengu usiokuwa na nuru ya 'kibuddha' kusema kwamba, Mtu aliyekatika hali isiyo ya kutaamulika ni mtu mwenyekuishi katika ulimwengu wa masumbuko na kuathiriwa na kweli athimu ya 'Dhuka' -- adha nne za kuonwa kwa jicho la mali sana -- ambazo ni asili ya masumbuko yote, kutoridhisha kwa maisha ya muda hapa duniani: (i) kuishi ni safari isiyo na kinga ya adha zote za jasho, maradhi, uzee nk... (ii) Chanzo cha taabu zote kuwa ni mshikamano na muambatano wa hisia za fahamu ya mtu na mali/amari za dunia / ulimwengu na mambo yake. (iii) Kwamba muda ndiyo adui ama mwamuzi asiye epukwa kuhakikisha marefu ya mambo ya mtu na hata uhai wake, japo hata mauti si mwisho wa safari ya mtu kwa kuwa kuzaliwa tena na tena kwa mtu humtupa yeye kurudi katika yale yale kila awapo hapa duniani kwa sura hii ama ile, hapa ama kule (iv) Kwamba namna pekee ya kumkomboa mtu ni pasi kuifuata njia ya mali sana ya Buddha--Gurudumu la kufanyikia namna nane ili kumpeleka mtu katika 'Taamuli' ... kuishi namna ya kati, (kuwa na nidhamu ya kati/sahihi), kutizama yote namna ya kati, kauli ya katikati/sahihi, dhamira sahihi/kati, vitendo sahihi, jitihada sahihi, utiaaji akili sahihi, uweka ufahamu katika pahala sahihi...

Ndivyo basi Buddha alisisitiza katika kila mtu kuna 'buddha' ndani yake... na katika kila kilichofanyika na kuchukua sura kina 'dhama' ndani yake. Ni dhama pekee inayoweza kutibu maradhi ya mtu kujaribu moja hata jingine lakini kamwe asijekupata ridhiko la ndani hasa na maisha yake...

Na zaidi Buddha alifundisha maisha ya kudumu katika miditisha kama njia ya mtu kuongeza umakini juu ya yote yanayotawala akili yake na kumfunga na mengine yote ayapayo maana ama utambuzi kuhusu mapenzi yake ama hatima yake katika 'uzima' wote...

Miditisha katika mtu hukua na kumea na kumuongoza yeye katika ukombozi kamili wa 'nafsi' ili kuishia katika 'uto-nafsi' ulio ni 'Buddha' kamili. Safari ambayo huweza kuchukua mtu jitihada ya isho moja hata jingine mpaka siku yake kuamka na kuifikia 'moksha', ukombozi mbali ya mwili, akili na hisia fahamu. Katika Ubuddha hufundishwa kwamba nafsi ya mtu na viumbe vyote hujidhirisha kwa namna ya mizunguruko inayofanyika kwa kuzaliwa na kufa na huku 'nafsi' ikiwa ni kiungo chenye kudumisha ukweli wa maisha katika sura iliyofichika lakini ikawa dhahiri kwa buddha ama msafiri wa njia ya kibuddha mwenye kudumu katika maelekezo ya vitendo vya ufunguo ndani 'utiaaji akili sahihi' na pia 'uweka ufahamu katika pahala sahihi'...

Unaweza kujifunza mengi kuhusu Ubuddha kama namna ya visomo fananishi vya dini, lakini dini ni zao la utamaduni na azma ya watu wakiwa kama jamii yenye taasisi zenye kutawala mashauri juu ya miongozo ya stawi zao husika. Ualimu wa Kibuddha na tamaduni za kibuddha ni matokeo mifumo ijayo na taasisi--na kama ilivyokuwa juu ya taasisi yeyote, kusudi hasa huwa ni kueneza sura ya ustawi ama ustaarabu kwa nguvu za fikra na hisia juu ya jambo lake na basi kutafuta kujenga ama kudumisha ushawishi wake katika maisha ya watu.

Ubuddha ni dini ambayo misingi yake yapitiliza dhana na mapokeo ya 'mtu' na 'mungu' ama 'nafsi' na 'mungu'...

Katika mafundisho ya ubuddha nafsi hukanushwa, na mungu vile vile... lakini hapo hapo hujakuwa dhahiri kuwa mwenye kufuata maelekezo ya nidhamu ya kuutafuta wokovu, kukombolewa na 'dhuka'--mtu huja kuijua nafsi yake na kuimaliza; hujua yote ambayo mtu angeliweza kudhani ni 'tawala' ya kimungu lakini hatafungamana la lolote ila kuridhika kuwa mmoja na kweli inayopitiliza yote yaliyodhahirika, naam, ni kama kusema, hata kuacha mungu kuwa mungu kwa maana kwamba kila kitu tayari ni yote mtu awezayo kudhania ni 'mkono' wa mungu na mashauri mengine yote yenye kuambatana na hilo.

Ubuddha kama imani isiyojihusisha na fikra adilifu za mashauri ya 'mungu' katika ulimwengu wa leo utatuletea kung'amua na kuelewa vizuri ukweli na mashauri juu ya 'Meritokrasia'.

Dini kama Ukristo na Uislamu, zinatuletea kung'amua ukweli na mashauri zaidi juu ya 'Tekinokrasia'...

Ila ufundi wa mambo ya muingiliano wa mwili, akili na hisia--Maarifa ya Yoga na nidhamu za vitendo na upeo wa kutambua/kung'amua, utatulea ukweli na mashauri zaidi kuhusu 'Usanisi'--jinsi ambavyo 'umungu' na 'uzima' vyachakata kama moja katika kila kitu kilichofanyika, kilichodhahiri ama kisicho dhahiri.

Nuru ya Ufahamu katika mtu ndiyo msingi wa kheri yote.

Na ndivyo Buddha alifundisha, ni kheri kila mtu kuja kuwa nuru kwa yeye mwenyewe...

Asante kwa ufafanuzi wa kina mose
 
Last edited by a moderator:
Kama maswali yameisha nitaendelea na sehemu ya pili

A NIGHT INSIDE BUDDHIST COLLEGE
Binadamu ni mtu anayependa uhuru na ukimchunga atatafuta mbinu ya kuwa huru
Ndani ya kile chuo tulichungwa sana na kama ikitokea umekamatwa umetoroka adhabu yake ilikuwa ni kufukuzwa chuo moja kwa moja
Hatukurusiwa kuvaa nguo zetu za nyumbani kila kitu kilikabidhiwa na kufungiwa store siku tulipowasili na tukapewa hayo manguo ambayo ndio ilikuwa 24/7 tunayavaa popote tulipokuwa (tulikuwa na pair mbili)
Chuo kilikuwa kilometer moja kufika mjini na nusu kilometer kufika barabara kuu
Chuo kilizungushiwa ukuta wa matofali na fence ya umeme na security lights lakini pia mijibwa mikali yenye roho mbaya sana
Wanachuo walilala floor ya chini na ya pili na mamaster floor ya tatu kwahiyo kama ungetaka kutoroka usiku ilibidi ufanye yafuatayo
- utaimu mijibwa ikiwa haiko upande wa mabweninini
- mtu akusaidie kuzima umeme kwenye fence
- ufanikiwe kuruka ukuta wa mita tatu bila kishindo na bila kuyastua makubwa huko yaliko
-ufanikiwe kuvuka security lights bila kuonekana na mamaster ghorofa ya tatu
-kisha utambae kwenye majani umbali wa nusu km mpaka kufika barabara kuu ndio unakuwa salama
Ukikaribia barabara kuu unavua manguo ya kibuddha ndani una T-shirt na jeans na kapelo na raba (nguo hizi zilikuwa zinafichwa mbali sana)
Unaingia mjini unafanya yako halafu wakati wa kurejea hali ni ileile, yani ilikuwa ukirudi bwenini salama unamshukuru Mungu na kujiapiza kuwa hutotoroka tena
 
Mshaha Kama nataka kufanya chi peke yake is it possible mzee???
 
Nilikuwa nina uwezo wa kutabiri hatari Neema au chochote, lakini pia niliporudi Tanzania kuna siku nilienda kanisani na wakati naenda kukaa siti za mbele nilikuwa na kitu kama vibration wakati nawapita watu
Lakini pia nimeshasimulia sana hapa JF matukio mengi ya kuibiwa nk na waliofanya hivyo ikala kwao

Nadhani hujajua jinsi ya kutumia kipaji chako vizuri.
Ningeshakuwa milionea fulani hivi.
 
Sio wewe tu ukishaanza kujifunza Buddhism unaanza kuona vitu katika mwanga tofauti na hivyo kukuvutia zaidi na zaidi kuendelea kujifunza
Binafsi baada ya Buddhism nilisoma conficious, Taoism Krishna consciousness na kidogo satanism

Duh! mshana jr unatisha your full of knowledge endelea kutujuza binafsi navutiwa sana, confucius niliwahi kuipitia kdg napenda hekima iliyoko huko
 
Last edited by a moderator:
Unaposema Vital power, ni nini hasa???
Ni kozi ya muda gani???
Mbimbinho chi gong ni nguvu inayotoka tumboni/ kitovuni, wale waimbaji wazuri hutumia koo na tumbo kutoa sauti zao na zina tofauti
Kuna connection kubwa sana kati ya mind na chi gong, ukijifunza tai chi movement zake ni za taratibu mno lakini lakini zilizobeba uzito mkubwa
Angalia mapigo mawili ya tai chi na karate/kung fu/judo
Ukipanga tofali 3 ukampa mtu wa karate/judo au kung fu azivunje atavunja zote tatu lakini ukimpa mtu wa tai chi avunje atakuuliza unataka avunje ipi au ngapi na atafanya hivyo
 
Last edited by a moderator:
Nadhani hujajua jinsi ya kutumia kipaji chako vizuri.
Ningeshakuwa milionea fulani hivi.

Hapana umilionea ni sort of craving....! Nautaka sana lakini si kwa njia hii
 
Ukimaanisha?
I mean, using your super powers kujua fursa, raising capital, getting customers etc

Yeah ni sahihi but kwa Tanzania yetu hii, unaishia kuitwa mwanga mchawi Freemason n the like japo mwisho wa siku uamuzi ni wako binafsi
Lakini kimsingi nanufaika sana na niliyojifunza
 
Mkuu mshana jr nadhani tutakuwa marafiki wazuri!!!,

Unaweza kunipa msaada wa namna ya kujitunza na kuishi kwenye chi!!,

Nayo inasaidia kuamsha zile sense 3 ambazo ziko dormant!!?

Je kuna side effects??!.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mshana jr nadhani tutakuwa marafiki wazuri!!!,

Unaweza kunipa msaada wa namna ya kujitunza na kuishi kwenye chi!!,

Nayo inasaidia kuamsha zile sense 3 ambazo ziko dormant!!?

Je kuna side effects??!.
neo1 niwe tu mkweli, chi hata mimi mwenyewe sijatosheka nayo ni unique thing ambayo inapatikana sehemu ndogo ya dunia Nakushauri usiache kuingia Google lakini pia hebu tafuta CD za mwanamama Enya na zingine zote za Tai chi utakapokwama mahali nicheki 24/7

Kuhusu hizo senses nyingine ni ishu ya meditation na kujisomea, lakini changamoto tuliyo nayo kwenye meditation ni kukosa muda wa ku practice na kuwa wasemaji sana
Tunaandika mambo so deep mpaka tunawachanganya watu
Ni lazima kuwe na Essex za meditation na kustick katika hizo kabla ya kwenda mbele zaidi
Hii ishu haina side effects kwakuwa haidhuru mwili wala kuharibu akili
 
Last edited by a moderator:
Imekusaidia nini?
sikiliza.. wewe umeyabeba maroho yafuatayo:- taekwondo spirits, dojo spirits, tai chi spirits nk.
matokeo yake utayaona very soon.
We, haukujiuliza ile namna ya nidhamu ya hali ya juu maanayake nini ?

Nakwambia kama ungemwabudu Mungu wa Kweli kwa namna ya nidhamu ile....
ungeiambia Kambi ya Lipumba hamia CCM, na ingekuwa....

Una point sana mkuu
 
Watu wanaabudu sanamu (China,India) lakin bado Mungu wetu amewabariki wao kuliko sisi ngozi nyeusi tunaojifanya tunaijua sana dini (kuna wanaomlilia Mungu na wanaojitoa mhanga kwa ajili ya Mungu)! Mambo ya dini wakati mwingine ni kizungumkuti.

Ni wewe tu hujui kuzifata protocol za Mungu, wao wanazifata kweli kwa kuitolea ibada na sadaka, mbona mi nimebarikiwa
 
Back
Top Bottom