A God can be a mere theory, nothing more

A God can be a mere theory, nothing more

Ok sasa ni time ya mimi kuproof kwamba vitabu vya Mungu vinadanganya.

Nilikuuliza wewe ni wa dini gani but hukujibu hilo. sababu ya kukuliza ni kwamba sitaki nichanganye uongo wa kitabu unachokiamini na kile usichokiamini.

Hope wewe ni Muslim. Aren't you?

Kwanza ungeeleza hivyo vitabu ulivisoma vp hadi ukagundua huo udanganyifu? Kwa sababu kama ulivisoma kama usomavyo gazeti tu hili suala litakuwa gumu sana.
 
Umejitahidi kutafiti vizuri ila utafiti wako unakosa nguvu linapokuja suala la "origin of life". Where did life start.? Naomba jibu bila kuacha mashaka

Hao mkuu hilo haliwezi kuwa swali gumu coz mimi kutojua "origin of life" haiwezi kuproof uwepo wa Mungu. hilo swali litakwenda sawa kama wewe tu utakavyoshindwa kuniambia "origin of God" coz naamini kutokujua kwako huko hakuwezi kumaanisha huyo Mungu hayupo.

Na ukisema tu Mungu hana chanzo nami naweza kukuambia life haina chanzo too. So who can proof then?
 
Zaburi 1:1
Heri mtu Yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki,
. ..............................
WALA KUKETI BARAZANI PA WENYE MIZAHA
 
Mashaxizo Inabidi tuanze kuwaelimisha watu waelewe. Kipindi hiki watu wanaamka tena kwa kasi kubwa sana. Uongo uliowekwa kuhusu uwepo wa mungu kwenye maandiko wanayoyaita matakatifu ni uongo mkubwa.

Ninajiandaa kipesa nitaanzisha midaharo mbalimbali kwenye TV na mafundisho ya kuwaelimisha watu waanze kuamusha consciousness zao.
Ubepari, Umwinyi, Ugaidi, Ukafiri na chuki zimesababishwa na Dini hizi za kikristo, kiislam na kiyahudi.

Ukija na ukweli utaeleweka ila njia yenu ya kusema hiki mara kile ni uongo lakini bila kueleza ukweli hasa ni upi itakuwa ni sawa na bure..tatizo mnataka kulazimisha watu waamini muaminivyo nyinyi na asiyefanya hivyo huonekana uhuru wa mawazo.
 
Last edited by a moderator:


Mkuu Mashaxizo, hapa nakubaliana na wewe na hili mimi niliishalizungumzia hapa;
Psychic Powers: Ni Nguvu za Kufanya Miujiza. Wengi wanazo Bila Kujijua!.


Ila hii hoja yako ya hakuna Mungu, ni kazi ya shetani!.

Mungu yupo ndio The Supreme Being!, Mwanza na Mwisho, Alfa na Omega, ambaye vitu vyote vimeumbwa nae.

Mungu yuko kwenye form ya spirit, God is Power, ndio nguvu inayowezesha kila kitu, ikiwemo uhai 'life force' na ana sifa kuu 4;


  1. Mungu ni omnipotent (all-powerful), Mungu ndio mwenye nguvu kupita nguvu nyingine zozote, ana emetupa sisi binadamu sehemu ya nguvu hizo kupitia 'WillPower'.
  2. Mungu ni omnipresent (in all places at the same time), yaani yuko mahali pote kwa wakati mmoja, ikimanisha Mungu yuko ndani yetu, na yote ambayo Mungu anayetenda anayatenda kutokea ndani yako!.
  3. Mungu ni omniscient (He knows everything), hivyo kila kinachotokea Mungu anakijua, yakitokea majanga, japo yanasababishwa na shetani, Mungu alijua na asipozuia inamaana ame approve, hivyo jambo lolote linalotokea, lilikuwa litokee, liwe zuri au baya ni kazi ya Mungu kwa sababu hata shetani yuko chini ya mamlaka ya Mungu.
  4. Mungu ni omnibenevolent (He only does things that are all good), yaani alipouomba ulimwengu na vyote vilivyomo alidhamiria yute yawe ni mema na mazuri tuu, ila shetani alipoasi, ndie mwenye jukumu la majanga, mateso na maovu yote!.
  5. Mungu alipomuumba binadamu, alimuwekea Uungu ndani yake, lakini pia akampa choice ya utashi wa kuamua au amfuate Mungu kwa kutenda yaliyo mema pekee, au amfuate shetani, kwa kutenda yaliyo maovu!.
  6. Tunaposema kutenda sio lazima matendo, actions, hata kwa kuwaza tuu mawazo maovu ni kumtumikia shetani, au kwa kusema maneno maovu, ni kumtumikia shetani.
  7. Shetani ana mission moja tuu duniani, kuyafanya yale yote yaliyo kinyume na Mungu, na utendani wa shetani ni kama ulivyo utendaji wa Mungu, yaani ile njia Mungu anayoitumia kumpa nguvu mwanadamu, ndio njia hiyo hiyo shetani anaitumia kumpoteza mwanadamu, tofauti pekee kati ya nguvu za Mungu na nguvu za shetani, nguvu za Mungu ni original na ziko ndani ya binadamu tangu siku ile ameumbwa, yaani ziko within, wakati nguvu za shetani ziko nje na ziliingizwa ndani kupitia kula tunda, hivyo ni aquired.
  8. Hivyo chochote kinachotokea duniani ni ama kwa nguvu za Mungu au nguvu za Mwanga, yaani Holly Spirit, ama kwa nguvu za shetani, nguvu za giza powers of the devil, na kuna wakati mwingine nguvu hizi hutumika kutenda mema au miujiza kama chambo, kwa shetani kuji disguise as God ili aweze kupata mavuno makubwa, hivyo kuna wahubiri kibao, wanafanya hadi miujiza kwa kutumia jina Mungu, lakini sii wa Mungu bali ni tricks za shetani. Majo ya kazi kubwa ya shetani ni kuwaaminisha binadamu kuwa hakuna Mungu kama anachofanya mtoa mada hii, anamtumikia shetani kwa kujua au bila kujijua, namna pekee ya kumsaidi ni maombi ili afunguliwe toka kwenye giza alimo aone mwanga.
  9. Tofauti pekee kati ya wema wa Mungu, na wema wa shetani, au miujiza ya Mungu na miujiza ya shetani ni conditionalities, kwa vile nguvu za Mungu ni original na kila mtu amepewa, miujiza ya Mungu au wema wa Mungu hutokea au huweza kufanyika naturally unconditional bila kuwekewa masharti yoyote, kwa Miujiza ya Mungu kutokea, unapaswa kuamini tuu. Lakini miujiza ya shetani au wema wa shetani ni conditiona una masharti lazima uyafuate!, ili itendeke au ataambiwa fanya hiki au kile!. Hivyo kuna wengi wanamtumikia shetani bila kujijua wakidhani wanamtumikia Mungu!.
  10. Ili uweze kujijua unamtumikia nani, au huko unakosali ni kanisa la Mungu au la shetani, kwanza ni wewe mwenyewe kutake your own initiative kutaka kumjua Mungu wa kweli, na hili unaweza kulifaniisha kwa kusoma vitabu vya dini kumjua Mungu kisha jifikirie kile kinachofanyika kwenye dhehebu lako ndicho Mungu alichofundisha?. Muulize Mungu aliyeko ndani yako kuwa hiki ni sawa?!, utaisikia sauti ikikuambia ukweli halisi!.

Jumapili njema.

Pasco

...........
Haya mambo ya kumezeshwa kwenye nyumba za ibada! Mi kila siku huwa nasikia miujiza miujiza, mbona wanaoponywa si watu tunaowafahamu........? Ukisoma kitabu, "his excellency head of the state", utapata japo picha kidogo juu ya fumbo la dini! Ni wazi binadamu ndo tumemuumba mungu and not the other way around🔴
 
Unaona sasa hapo ndiyo umeeleweka. Lakini kabla ya kujadili hili suala ningependa kujua kuwa wewe kama wewe hizo sifa za Mungu umezipata wapi

Hahahahaaaaa! i like the way you think.

Hizo sifa hata sikupenda kukutajia but uliniambia nitaje kwa mtazamo wangu. ok hizo nimetoa kupitia Imani ya kiisla na Ukiristo na hiyo ndio sababu nazikataa hizo dini kwamba sio za kweli hizo sifa zinapingana na kile kilichoelezwa na matabu yao.
 
Ukija na ukweli utaeleweka ila njia yenu ya kusema hiki mara kile ni uongo lakini bila kueleza ukweli hasa ni upi itakuwa ni sawa na bure..tatizo mnataka kulazimisha watu waamini muaminivyo nyinyi na asiyefanya hivyo huonekana uhuru wa mawazo.
Ndugu nadhani unachanganya vitu hapa. Hapa tunaonesha jinsi gani maandiko yenu yanavyojichanganya kuhusu uwepo wa mungu wenu. Sasa kulingana na hayo na mungu wenu kutojitetea ni sawa na yule mungu wa kichaga aliyevunjwa.

Mungu gani ashindwe na shetani?, mungu gani ahukumu watu wake? mungu gani apende wazungu tu? mungu gani huyu?
Ni lazima tuutafute ukweli. Na pale utakapoanza kuutafuta ukweli nuru itakuangazia.
 
We unaamini hii dunia na vilivyomo vimetokea wapi?
Na unaamini Ulimwengu (Universe) umetokea wapi?

Katika ule moto wa mwisho wako watu ambao Watakua ndio KUNI ya wengine, yaani bottom of lile shimo ndio wataanza wao, ambao wewe ni mmoja wao.

Then kule juu mwisho mwisho kwenye Moshi unapoishia ishia ndio tutakaa sisi believers ikitokea tukaingia kule kwa bahati mbaya (Mungu apishie mbali).
.............
Kuna theories nyingi zinazojaribu kujibu maswali yako na moja ya theories hizo ni dhana ya Mungu na Uungu, lakini hakuna theory hata moja inayojitosheleza (ikiwemo na dhana ya kuwa ulimwengu na kilichomo kimeumbwa na Mungu).
 
Hahahahaaaaa! i like the way you think.

Hizo sifa hata sikupenda kukutajia but uliniambia nitaje kwa mtazamo wangu. ok hizo nimetoa kupitia Imani ya kiisla na Ukiristo na hiyo ndio sababu nazikataa hizo dini kwamba sio za kweli hizo sifa zinapingana na kile kilichoelezwa na matabu yao.

Kwanza kabisa mie nilikwambia utoe vigezo vya kutambua dini sahihi, ila wewe ukaleta sifa za Mungu na ndiyo maana nilikuuliza hivyo ni vigezo vya kutambua dini ya kweli au ni sifa za mungu?

Sasa je,hizo sifa za Mungu unazikubali kuwa ni za kweli ili tuweze kuchambua dini sahihi yenye kutokana na Mungu wa kweli. Lakini kama itakuwa huzikubali hizo basi itakuwa haina hapa kujadili suala hilo.
 
Jee unamanisha dini/zote zinazomuamini Mungu/miungu ni za kweli? ikiwa jibu ni ndio, inawezekana vipi ukizingatia hayo makundi yanaamini Miungu tofauti?

Ikiwa jibu ni sio. Ni ipi dini ya kweli?

Sasa mkuu elimu ya kimapokeo ni ipi na ya kimamboleo ni ipi?

Ok, Nimefanikiwa kuyaona maswali yako.

Kwanza Amua kweli katika Moyo wako kutaka kumjua MUNGU wa kweli.

Anza kufikiri kuhusu Dunia, Nyota zisizo kuwa na Idadi, JUA, Mbala mwezi, Bahari yenye mawimbi makubwa, Milima mirefu, Misitu minene, Species mbalimbali za wanyama wa kupendeza,Ndege wengi wa aina mbalimbali wa kupendeza,Majangwa, Mawingu, Mabonde makubwa, mito, Maporomoko ya maji, Matetemeko ya Ardhi, Volcanic eruption, Hurricanes, Vimbunga alafu jiulize swali moja NI NANI ALIYEVIFANYA VYOTE HIVYO?? najua hutopata jibu. (kama utakuwa umeweka elimu yako ya Darasani pembeni)

Jaribu kuzunguka Duniani kama uberikiwa kupata kipato kitakacho kuwezesha kusafiri..., Jaribu kutembelea sehemu mbalimbali Duniani Anzia Israel, Nenda Italy,China,Russia,SA,Thailand,Canada Bila kusahau nchi za Uarabuni kama Pakistani, Irani, Iraq, Kazakistan, Libya, Egypt nenda Australia, Cuba, Denmark n.k at least tembelea robo tatu ya nchi sehemu mbalimbali za Duniani.

KUMBUKA tembelea sehemu hizo ukiwa na nia ya kutaka kumjua MUNGU MWENYEZI, Utaona watu wengi maelfu kwa maelfu wakifanya Ibada mbalimbali kwa dini tofauti tofauti tembelea sehemu zao za Ibada.

Then kaa chini jiulize wewe ni nani na una nini cha ziada kuzidi watu wote mamia kwa maelfu utakao waona wakifanya ibada kumwomba MUNGU MKUU WA VIUMBE VYOTE ULIMWENGUNI.

Jitengenezee IMANI (kumbuka imani huja kwa kuamini na kuwa na uhakika na jambo unalolitarajia) Anza kuuambia MOYO wako ''nataka kumjua na kumfahamu MWENYEZI MUNGU MKUU, MKAMILIFU, MUUMBA MBINGU NA ULIMWENGU NA VITU VYOTE VINAVYOKAA NDANI YAKE'' jaribu kujiambia hivyo mara kwa mara na kwa muda mwingi.

Iset akili yako kutaka kumjua MWENYEZI MUNGU kumbuka hapo umeshajishusha na kujiondoa uthamani wako ambao ulifikiri mwanzoni unao., Utaanza kuona mambo madogo madogo tuu yakikudhihirishia uwepo wa MWENYEZI MUNGU ambayo naamini kwako Yatakuwa ni makubwa sana.

Kumbuka hutoweza kumwona MWENYEZI MUNGU (kama akili zako umeziset ivyo) kwani hakuna kiumbe chini ya JUA kinachoweza kumtazama MWENYEZI MUNGU kutokana na UKUU na UTUKUFU alionao.

MWENYEZI MUNGU NI MKUU NA MTUKUFU NA UKUU WAKE HAKUNA ANAYEWEZA KUUELEZEA.
 
Ok, Nimefanikiwa kuyaona maswali yako.

Kwanza Amua kweli katika Moyo wako kutaka kumjua MUNGU wa kweli.

Anza kufikiri kuhusu Dunia, Nyota zisizo kuwa na Idadi, JUA, Mbala mwezi, Bahari yenye mawimbi makubwa, Milima mirefu, Misitu minene, Species mbalimbali za wanyama wa kupendeza,Ndege wengi wa aina mbalimbali wa kupendeza,Majangwa, Mawingu, Mabonde makubwa, mito, Maporomoko ya maji, Matetemeko ya Ardhi, Volcanic eruption, Hurricanes, Vimbunga alafu jiulize swali moja NI NANI ALIYEVIFANYA VYOTE HIVYO?? najua hutopata jibu. (kama utakuwa umeweka elimu yako ya Darasani pembeni)

Jaribu kuzunguka Duniani kama uberikiwa kupata kipato kitakacho kuwezesha kusafiri..., Jaribu kutembelea sehemu mbalimbali Duniani Anzia Israel, Nenda Italy,China,Russia,SA,Thailand,Canada Bila kusahau nchi za Uarabuni kama Pakistani, Irani, Iraq, Kazakistan, Libya, Egypt nenda Australia, Cuba, Denmark n.k at least tembelea robo tatu ya nchi sehemu mbalimbali za Duniani.

KUMBUKA tembelea sehemu hizo ukiwa na nia ya kutaka kumjua MUNGU MWENYEZI, Utaona watu wengi maelfu kwa maelfu wakifanya Ibada mbalimbali kwa dini tofauti tofauti tembelea sehemu zao za Ibada.

Then kaa chini jiulize wewe ni nani na una nini cha ziada kuzidi watu wote mamia kwa maelfu utakao waona wakifanya ibada kumwomba MUNGU MKUU WA VIUMBE VYOTE ULIMWENGUNI.

Jitengenezee IMANI (kumbuka imani huja kwa kuamini na kuwa na uhakika na jambo unalolitarajia) Anza kuuambia MOYO wako ''nataka kumjua na kumfahamu MWENYEZI MUNGU MKUU, MKAMILIFU, MUUMBA MBINGU NA ULIMWENGU NA VITU VYOTE VINAVYOKAA NDANI YAKE'' jaribu kujiambia hivyo mara kwa mara na kwa muda mwingi.

Iset akili yako kutaka kumjua MWENYEZI MUNGU kumbuka hapo umeshajishusha na kujiondoa uthamani wako ambao ulifikiri mwanzoni unao., Utaanza kuona mambo madogo madogo tuu yakikudhihirishia uwepo wa MWENYEZI MUNGU ambayo naamini kwako Yatakuwa ni makubwa sana.

Kumbuka hutoweza kumwona MWENYEZI MUNGU (kama akili zako umeziset ivyo) kwani hakuna kiumbe chini ya JUA kinachoweza kumtazama MWENYEZI MUNGU kutokana na UKUU na UTUKUFU alionao.

MWENYEZI MUNGU NI MKUU NA MTUKUFU NA UKUU WAKE HAKUNA ANAYEWEZA KUUELEZEA.

Wewe ni dini gani?
 
mkuu ninachofurahi ni kuwa angalau asilimia tisini ya maswali yako yanaufumbuzi kupitia neno lake ila kama ukiamua kujifunza kwa unyenyekevu.

Wewe sio wa kwanza hata paul wakati akiitwa sauli alikuwa anaua watumishi akidhani anafanya kazi ya Mungu kumbe alijichanganya.

Mfalme NEBUKADNEZA alikuwa na akili nyingi pengine kuliko mtu yeyote anayeishi duniani kwa sasa. Lakini wakati ulipofika pamoja na miungu yake yote. alikubali na kukili Hakuna kama Mungu wa Israel.

Ninachoomba ukweli huu uuelewe mapema kabla haujachelewa na moyo wako kuziba kabisa uwezekano wa kupokea ukweli.
natanguliza shukurani. kwa huo utangulizi wangu

...........

Hata leo tunaambiwa Wazungu wanaakili sana kuliko sisi Weusi, na watu kama wewe kuamini hivyo! Kwahiyo siwezi kushangaa kuwa umeaminishwa na kuamini kuwa Nebuchadnezzar alikuwa na akili kuliko binadamu yoyote aliyepata kuishi! Upande mwingine, tunaambiwa Suleiman alikuwa na akili, hekima na busara kuliko binadamu yoyote!!! Haya mambo ya Mungu na Uungu, they only exist in your own mind, and those who make their living by preaching! Lazima wazidi kukuogopesha.......though uoga huo usaidia kuwepo kwa Amani.......... Ila uwezi kunidanganya kuwa there is life after death na kwamba kuna supernatural powers🔴
 
Ndugu nadhani unachanganya vitu hapa. Hapa tunaonesha jinsi gani maandiko yenu yanavyojichanganya kuhusu uwepo wa mungu wenu. Sasa kulingana na hayo na mungu wenu kutojitetea ni sawa na yule mungu wa kichaga aliyevunjwa.

Mungu gani ashindwe na shetani?, mungu gani ahukumu watu wake? mungu gani apende wazungu tu? mungu gani huyu?
Ni lazima tuutafute ukweli. Na pale utakapoanza kuutafuta ukweli nuru itakuangazia.

Ujue unapolikuta tukio la mtoto mdogo akimpiga mtu mzima ambaye ana nguvu zake vizuri tu lakini yule mtu mzima akawa harudishi mashambulizi kwa yule mtoto, basi unaweza ukalieleza tukio hilo kuwa huyo mtu mzima kapigwa na mtoto,lakini kiuhalisia hatuwezi kusema kwamba yule mtoto mdogo ana ubavu kumzidi yule mtu mzima ndiyo maana akampiga bali tutatakakujua ni kipi kilichofanya hadi yule mtu mzima akamuachia mtoto ampige.


Maana ya mfano wangu huo ni kwamba mambo mnayoyaeleza nyie ni kuwa mnayatizama mambo kwa kiasi cha kulitamaza tukio tu lakini hamtaki kujua uhalisia.
 
Kulingana na comment yako nimeonelea nikuulize kunakitu nataka kucoment.

Mimi ni mkatoliki.

Imani yangu ni kwamba naamini juu ya Kufa, kufufuka na Kurudi Kwa Yesu kuja kutuchukua.

And most important to MYSELF I believe in TRUE LOVE, Upendo wa kweli ambao Bwana Yesu alituachia. .

Karibu kwa Comments.


 
Ujue unapolikuta tukio la mtoto mdogo akimpiga mtu mzima ambaye ana nguvu zake vizuri tu lakini yule mtu mzima akawa harudishi mashambulizi kwa yule mtoto, basi unaweza ukalieleza tukio hilo kuwa huyo mtu mzima kapigwa na mtoto,lakini kiuhalisia hatuwezi kusema kwamba yule mtoto mdogo ana ubavu kumzidi yule mtu mzima ndiyo maana akampiga bali tutatakakujua ni kipi kilichofanya hadi yule mtu mzima akamuachia mtoto ampige.


Maana ya mfano wangu huo ni kwamba mambo mnayoyaeleza nyie ni kuwa mnayatizama mambo kwa kiasi cha kulitamaza tukio tu lakini hamtaki kujua uhalisia.
Unaongeleaje kuhusu mungu wa wachaga aliyevunjwa. je huyo mungu wa wachaga na mungu wa waisrael anatofauti gani? au yule mungu wa ibrahimu na mungu huyu wa wachaga anatofauti gani?

Au mwanamalundi na yesu wanautofauti gani?
 
...........

Hata leo tunaambiwa Wazungu wanaakili sana kuliko sisi Weusi, na watu kama wewe kuamini hivyo! Kwahiyo siwezi kushangaa kuwa umeaminishwa na kuamini kuwa Nebuchadnezzar alikuwa na akili kuliko binadamu yoyote aliyepata kuishi! Upande mwingine, tunaambiwa Suleiman alikuwa na akili, hekima na busara kuliko binadamu yoyote!!! Haya mambo ya Mungu na Uungu, they only exist in your own mind, and those who make their living by preaching! Lazima wazidi kukuogopesha.......though uoga huo usaidia kuwepo kwa Amani.......... Ila uwezi kunidanganya kuwa there is life after death na kwamba kuna supernatural powers

Ivi Mkuu kwani hakuna watu walio kuzidi akili wewe... naamini wapo tena wengi tuuu na wamekuzidi kwa kiwango kikubwa tuuu...! Sioni kutokuamini kwako juu ya Mfalme Sueiman.

Your point is too low, Jaribu kugusia swala jingine labda.
 
Mimi ni mkatoliki.

Imani yangu ni kwamba naamini juu ya Kufa, kufufuka na Kurudi Kwa Yesu kuja kutuchukua.

And most important to MYSELF I believe in TRUE LOVE, Upendo wa kweli ambao Bwana Yesu alituachia. .

Karibu kwa Comments.



Kwa nini wakatoliki huwa wanamumbea mtu aliye kufa kuwa atolewe tohalani?
 
Ivi Mkuu kwani hakuna watu walio kuzidi akili wewe... naamini wapo tena wengi tuuu na wamekuzidi kwa kiwango kikubwa tuuu...! Sioni kutokuamini kwako juu ya Mfalme Sueiman.

Your point is too low, Jaribu kugusia swala jingine labda.
Point sio kumzidi yeye point ni kwamba anaakili kuliko watu wote duniani. Huu ni ujinga uliopitiliza
 
Back
Top Bottom