A - Town Gangsters walioitikisa Arusha kwa matukio ya uhalifu

Mojaa alikuwa anajificha kwenye upolisi jamiii [emoji28], polisi wanalinda wahuni siku zote. Sio wa kuwaamini
 
Mawala alikua na watoto wawili na rundo la madem,fununu aliuawa shauri ya kugombea vitalu vya uwindaji,alikua anamiliki vitalu vya kutosha na wazungu flani
 
Wewe unaijua chuga kindakindaki,fred jebi si alichomwa kisu
 
Mojaa alikuwa anajificha kwenye upolisi jamiii [emoji28], polisi wanalinda wahuni siku zote. Sio wa kuwaamini
Mojaa ni police kidole hana jingine,siku hizi yeye anapewa kazi ya kuleta wahuni kwenye kesi za kubomoa nyumba zilizo tolewa hukumu mahakamani,kuvunja au kutoa wamiliki ndani ya nyumba
 
Mkuu wao wa kanisa tiba wa lile lililopo mnazi mmoja hapo daslamu ?
 
Mojaa ni police kidole hana jingine,siku hizi yeye anapewa kazi ya kuleta wahuni kwenye kesi za kubomoa nyumba zilizo tolewa hukumu mahakamani,kuvunja au kutoa wamiliki ndani ya nyumba
Mwaka juzi nadhani, alienda kuleta vurugu kwa watu kwa kigezo cha upolisi (mtaa wa jaluo chini pembeni ya mtoni). Wakamkata panga sema hakufa
 
Hao vibaka tu ,ndo mana Jombi alikua anasubiri waibe aende akawaibie au la wampe mgao.
Jombi ndio jambazi toka mbeya tanzania yote toka 80s mpaka akafa aliyetikisa.
hao walisakwa na rais mmakonde,
JOMBI alipigiwa akaombwa aache mambo yake atulie
akabugi akaenda huko huko Arusha akapiga tukio na tatizo aliua wazungu kadhaa akaiba madini wakamkamatia manyara huko maporini katika kutoroka.pale ndo akafungwa.
 
We una matatizo binafsi na Arusha teh teh, miaka ya 90's kimsingi hakukuwa na tofauti sana ya Arusha na Dar kwa maana ya town things. Kwa kukusaidia tu Dar pia kulikuwa na majambazi na walisumbua sana. Kuhusu usela mavi Dar upo sana kuliko Arusha... sema hauuoni kwa sababu unapita maeneo yenye neema. Kingine mtu alikuwa anatoa profile ya uhalifu we ukaleta mashindano.
 
Sema watu wanazidiana level, unataka kushindanisha majambazi kwa matukio, Jombi kwao Mbeya na wewe kama kwenu Mbeya inabidi tukuelewe
 
Eugene in mdogo wake Batlida Burian,alikuwa ni Jambazi
 
Sema watu wanazidiana level, unataka kushindanisha majambazi kwa matukio, Jombi kwao Mbeya na wewe kama kwenu Mbeya inabidi tukuelewe
ndio nakwambia hao wotw hapo juu kwa jombi walikua watoto chekechea,ndio nikakwambia badae alikua hata anawapora hao uliowataja na mwisho wakaacha kuiba akaingia front ndio tukio lililommaliza.
 
Miaka ya 80 kuna jambazi aliitwa Nyau, katika mazindiko yake alilishwa moyo wa paka. Akikurukia shingoni alikaba na kurarua kama paka. Huyu jamabazi aliteleza mikononi kwa PGO kama nyoka anavyoteleza mikononi mwa mwanadamu.

Alikua na hirizi hiyo akiivaa risasi zilikua zinapita bila kumdhuru. Alikinukisha Dar na kwenda kujificha Tanga vijijini huko kwa wakwe zake.

Aliuzwa na mke wake, mke wake alikula dili na wajomba kuwa akiwasaidia kumkamata yeye hatakua na hatia. Aliwaambia akiwa amevaa hirizi yake hamuwezi kumkamata.

Basi bwana alikaa ndani muda wote, kuna siku mke wake alimwambia si aende nje akapate fresh air, jamaa alitaka kuvaa hirizi mkewe alimwambia unavaa ya nini si unaemda hapo tu. Kumbe nje wajomba wamezunguka nyumba usawa wa vichaka.

Nyau alikamatwa kizembe sana bila hirizi yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…