Abby Chams: Sijawahi kula miguu ya kuku wala firigisi, wala sijawahi kusikia sehemu inaitwa Mburahati

Another fool, unafikiri dar tu ndo kuna ushuani? Ushamba mzigo,
Pumbavu kenge wewe mporipori,
Huko maporini kwenu ni makazi yaliyochangamka, narudia hakuna mfano wa Oysterbay, Masaki, Msasani wala Mikocheni, mpaka kesho hata Mbweni ni majengo tu makubwa lakini haitafikia thamani ya kiwanja wala nyumba za hayo maeneo.
Narudia tena hakuna ushuani mikoani na hataikaa itokee,
 
Hata Mimi sijawahi kula miguu ya kuku na firigisi.
 
Mie nikiona mchuzi au soup ina miguu ya kuku baasss hapo hata hamu ya kula inaniisha. Hivyo ikitokea nimeletewa kuku wa kienyeji ameshatengenezwa kukiwa na miguu ya kuku na kichwa natoa.
Yaani hata ile sight basi mimi inani disturb.
Ila firigisi napiga fresh
 
sahihi mimi nilianza kula matembele nikiwa mkubwa kabisa.
Kigogo nimekuja kukujua nina watoto.
Temeke sijui mbagala nimefika nikiwa mkubwa kabisa chuo sijui.
Jamani kuna watu maisha yalikuwa ni wilaya ya kinondoni tu, tukienda wilaya nyingine ni Upanga.
Nini ajabu sasa ?
Lazima kwani kupajua Mburahati? Hapajui ndio!
lazima kula miguu ya kuku?hajawahi kula ndio!
 
Mie nipo zanzibar miaka telee na kina sehemu naziskia tu pasi na kuzijua.
Sehemu nyengine ndio naziskia hivi ukubwani na huwa nauuliza hio iko wapi Unguja au Pemba, ipo mjini au shamba!
Inategemea na maisha uliokulia mkuu. Wengine wanakuwa wanajua njia ya kwenda skuli na kurudi tu
 
Wewe sasa ndo umesema.
 
Ni mfano tu, Mtu anayeishi mbagala, sio rahaisi kuifahamu Kimara Bonyokwa, au kuifahamu Kilungule.

Huyo binti yuko sahihi, kuna maeneo sio rahisi kuyafahamu kama huyatembelei au katika cycle yako hakuna mwenye interest nayo.
 
Miguu ya kuku na kichwa huwa napenda, bahati mbaya kabisa huwa hapa home akiandaliwa vinakatwa na kutupwa pia naona noma kusema nitengee miguu ya kuku au kichwa. Bahati mbaya nyingine ni kuwa siwezi kununua ile ya uswazi, hitimisho najikuta sijala miaka mingi
 
Upanga imekuwa wilaya lini?
 
Sahihi kabisa mkuu, naona hiyo management yake imejikita zaidi kwenye kudeal na kipaji Chake atoe Muziki mzuri tu basi, na Wala hawajali kabisa mahusiano na audience yake yako vipi.

Muziki ni Zaid ya kipaji, mashabiki wana sehemu kubwa sana ya kuukuza Muziki wako hasa kwa bongo hapa, hivyo ni muhimu sana kujua behavior patterns pamoja na akili zao zikoje hili ujue namna ya kuishi nao.

Na namna nzuri ya kuishi au kuteka mashabiki ni kujifananisha na wao hata kama ni kiongo uongo, na sio kujitofautisha na wao.

Sasa wewe huwezi leo hii ukaropoka eti wewe hujawahi kula ugali na Wala kwenu hampikagi ugali, halafu utegemee positive reactions kutoka kwa watanzania wakati zaidi ya 96% wamekuzwa na huo huo ugali ambao wewe unaona si chakula Cha kula mtu.

Huyu Binti washauri wake wanapaswa kumjenga kwenye suala Zima la public relation, na wasikae tu kujustify majibu yake ya ajabu ajabu mara sijui kakulia masaki, yeye sio celebrity wa kwanza kukulia masaki walikuwepo akina king crazy Gk walikulia Oysterbay sijui Upanga lakini walijua kuishi vizuri na adhira ya bongo.
 
Upanga imekuwa wilaya lini?
Sehemu ikiwa ndani ya wilaya nyingine inaitwa jina la wilaya hiyo au jina la sehemu husika?
suala lilikuwa, ni kutaja eneo lililopo ndani ya wilaya tofauti na nilipozoea kufika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…