Abdallah Mwaipaya ulichokifanya Redioni usikirudie tena Kitakugharimu Kiutendaji kwa Rais Samia

Abdallah Mwaipaya ulichokifanya Redioni usikirudie tena Kitakugharimu Kiutendaji kwa Rais Samia

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
DC wa Mwanga Mheshimiwa Abdallah Mwaipaya najua kuwa ulikuwa Radio One na ITV na ulikipenda mno Kipindi chako cha Mazungumzo ya Familia cha kila Jumapili ukiwa na Pacha wako Farhia Middle.

Kwa Mshangao kabisa leo nimekusikia nawe ukipiga Simu ( japo najua uliipiga ya Farhia Middle ) na Kuanza Kuchangia Mada za Masuala ya Mahusiano na mengineyo huku ukijisahau kuwa hivi sasa Wewe ni Mheshimiwa na Maadili hayakuruhusu hivyo.

Labda leo nikusaidie tu DC wa Mwanga Abdallah Mwaipaya kwamba kwa Hadhi yako kwa sasa unachoweza kufanya ni kuwa Msikilizaji wa hicho Kipindi ( ambacho kilikuwa chako na Farhia ) kabla ya Uteuzi wako na kama Mada ikikugusa unaweza kutuma Meseji ya Kusalimia na Kupongeza kwa Kipindi kizuri itatosha sana.

Lakini kwa hiki ulichokifanya leo tena DC mzima tunayetegemea upo busy Kushughulika na Changamoto tena za Watu wa huko Mwanga kupiga Simu Saa 3 Radio One, Kuchekacheka, kupiga Stori na Kuchangia sidhani kama kina Afya kwa Wadhifa huo ulionao sasa.

Ulishakuwa Radio One na ITV na sasa ni Mkuu wa Wilaya hivyo tafadhali achana na ya huku na Jikite na Majukumu yako hayo mapya, makubwa na mazito na kama labda bado unapenda kuendelea Kutangaza basi andika Barua ya Kuachia ngazi kwa Mama ( Rais ) Samia ili akutoe na urejee Radio One katika hicho Kipindi chako uendelee Kubebishana na Rafiki yako Kipenzi wa Redioni Farhia Middle.

Nawajua Watangazaji wengi tu tena waliokuwa Wazuri kukuzidi katika Media zingine ila tokea Wateuliwe hawana muda tena wa kupoteza Kufuatilia Vipindi vyao bali sasa wamejikita zaidi katika Kuwatumikia Wananchi na kuwaletea Maendeleo yao.

Huyo Mtangazaji Farhia Middle ambaye ndiye anapenda na Kukulazimisha sana uwe unachangia katika hicho Kipindi kuwa nae makini kwani atakuponza kama vile Samson alivyoponzwa na Delilah na utakuja Siku moja Kunikumbuka Mimi Mightier wa hapa JamiiForums.

Ni matumaini yangu kuwa utanielewa DC wa Mwanga Abdallah Mwaipaya kwa huu Ushauri wangu, ila kama kuna mahala nimekukwaza kwa huu Uwazi wangu Kwako naomba Radhi sana.
 
Nakiri sikumsikia alipopiga simu lakini kwa maelezo yako sijaona kosa hapo mkuu. Kuna simu huwa zinapigwa kwenye matamasha ya usiku wa saa sita mkuu Tena hivyo visanii vinavyopigiwa simu..vinaweka loudspeaker kwenye mic ili mheshimiwa asikike na walevi walioko pale hulionagi Hilo..au mkubwa siku zote yuko sawa? Vipi mawaziri wanaokata mauno kwenye sherehe?
 
Nyie ndio wale ukipewa ujumbe wa nyumba Kumi unatembea ukiwa umetanua mabega Kama ndege Vita.

Ukiwa Kiongozi haimaanishi unajiondoa kwenye mambo yote ya kijamii, Lazima u socialize na Watu, cheo ni kitu cha kupita tu jifunze Kwa Sabaya.

Hicho kipindi kingekuwa Kina maadhui mabaya yasiofaa kwenye jamii kingekuwa kinaruhusiwa?
 
Mkuu wacha ukuda.

Kuwa serious na kazi haina maana ndio ukunje sura muda wote.

Mwaipaya yuko sahihi kwa alichokifanya so usimchagulie la kufanya.

Maisha ya sasaivi yanataka kujisocialize na kimbuka Mwaipaya sio mtangazaji bali kwa sasa ni mwanasiasa. Siasa haifanyiki bila ya watu ambao hao ndio wanaunda jamii.

Wewe uko serious ila mfumo haujakuona bali Mwaipaya mfumo umemtambua na umeona anafa.

Kuna mambo ambayo ni unethical lakini sio kuongea kwenye radio.

Mwaipaya kama kiongozi wa watu ametumia media kuelimisha jamii kwa nafasi yake, sasa wewe ndugu yangu unateswa na nni baba.

Ukiilewa dunia ya sasa wala hutopata taabu bali ukikomaa kama jiwe la porini utateseka kama unavyoteseka sasa.

Watu sasa hivi wanaangalia weledi wa kazi zaidi kuliko mbwembwe za kutaka kuitwa mkuu na kujitenga na jamii kisa madaraka.

Madaraka yanapita ila jamii haipiti.

Hongera mdogo wangu Mwaipaya, wewe ni kijana mfano mwenye kutenda kazi kwa weledi na hekima kubwa sana.

Kazi iendeleee!
 
Mtu mweusi ana funza kichwani sio bure. Naamn wewe ni mmojawapo mwenye funza tena sio mmoja wengi tu. Kuwa DC hakukufanyi uwe na tabaka katika jamii nyie ndio wale mkiwa kwenye madaraka mnakuwa miungo watu, jinga kabisaa hii..kwan akipiga simu na kuchangia mada shida iko wapi? Kama hajamtusi mtu au haenda kinyume na jamii hakuna shida yyte. Usifikiri wengine ni malimbukeni kama wewe na wenzako
 
Nakiri sikumsikia alipopiga simu lakini kwa maelezo yako sijaona kosa hapo mkuu....Kuna simu huwa zinapigwa kwenye matamasha ya usiku wa saa sita mkuu Tena hivyo visanii vinavyopigiwa simu..vinaweka loudspeaker kwenye mic ili mheshimiwa asikike na walevi walioko pale hulionagi Hilo..au mkubwa siku zote yuko sawa?...vipi mawaziri wanaokata mauno kwenye sherehe?
Hata marehemu JPM alipigia simu kipindi cha clouds 360 (sijui kinaitwa hivyo au la) na akawapa pongezi kwa kuendesha kipindi kizuri kinachoelimisha,sioni ubaya wowote.
 
Bado natafuta kisa la mheshimiwa lakini silioni. Aliye elewa please anisaidie
 
Back
Top Bottom