Abiria wa Pugu anafuata nini kwenye SGR kama sio upigaji

Abiria wa Pugu anafuata nini kwenye SGR kama sio upigaji

anza kuzoea tu daladala mkuu kwenda pugu, cas either ulipe nauli ya dar moro then hata ukishuka pugu sawa tu utajua mwenyewe, cas maoni yangu yashapokelewa huko TRC na majibu yamekuja ndio watafanya hivyo cas washaona changamoto iliopo. Bye mkuu rudi barabarani tu kadandie magari ya pugu
station ya pugu ilikuwa ya kushusha ng'ombe, wakati wa mkoloni pugu ikuwa msituni na iliwekwa pale pia kwa shughuli za kijeshi, kwa sasa haina maana tena, funga hiyo station fullstop
 
watanzania (baadhi) wajinga sana wanajifanya watalaamu na professional wa kila kitu, kwani Pugu hakuna station ya treni? na kwa nini iljengwa kama haina maana? low iq folks, emotions zimewajaa badala ya logic, sgr ina treni aina mbali mbali kuna ya kawaida ambayo itasimama kila kituo na kuna express ambayo itasimama vituo vikubwa tu, kipi ambacho hamuelewi hapo? nchi haiendeshwi kwa personal interest bali interest za wote, huko Pugu kuna watu wanaishi pia …
We kwenda zako huko! Kuwa na station sio lazima ipakie abiria anaetoka Dar na kwenda Dar! Matumizi mabaya ya raslimali.
 
Dawa ni kila kituo kuweka geti litakalofunguka na abiria kuweza kupita baada ya kuwa amescan tiketi yake. Hiyo itasaidia kuzuia hao wote wababaishaji, kama unalipa nauli ya kuishia Pugu halafu ukaendelea mpaka Moro, ukifika kule manake geti litakataa kukurusu kupita maana tiketi yako ilikuwa ya kuishia Pugu. Matumizi ya teknolojia ndio suluhisho hapo, hakuna hata haj ya walinzi ndani ya mabehewa
 
We kwenda zako huko! Kuwa na station sio lazima ipakie abiria anaetoka Dar na kwenda Dar! Matumizi mabaya ya raslimali.

siyo lazima ndiyo kama mambo yote siyo lazima, hata treni ya umeme inayokwenda 160 km/ h siyo lazima pia, ajabu unaongelea matumizi mabaya ya rasilimali kivipi? kutakuwa na treni ya ya express pia ambayo haitasimama vituo vidogo na kutakuwa na treni nyingine ambayo itasimama kila kituo kilichojengwa kwani watu wa Pugu na kwingineko ni walipa kodi pia …
 
station kujengwa pugu ilikua ni makosa, ila ndo ishajengwa, msijari mtakua mnalipia nauli ya morogoro kwenda hapo pugu kwenu😊

ni makosa kivipi? isitoshe kama ni hivyo kwa nini wa morogiro wasilipie nauli ya dodoma pia kwani treni ya dodoma kusimama morogiro ni makosa pia kwa logic yako …
 
Naskia SGR wanapakia abiria hadi wa buku alafu wanapitiliza hadi dodoma

Juzi hapa kulikuwa na malalamiko abiria wa Doodma wale original na wa moro wanakosa tiketi wanaona online treni imejaa kumbe mmewapa nafasi watu wa pugu na abira wa karibu kwa bei kitonga na hao kitonga ni wahuni wanaopitiliza hadi Morogoro, Dodoma kwa elfu moj hivi hamuoni aibu?

Huu mradi msipikuwa makini mtauuwa mapema tu maana naona hii ni michezo ya wafanyakazi

Ukienda abood pale hakuna nauli ya mlandizi wala nauli ya Chalinze ukipanda gari ya mro kama nuali ni sh 13000 utalipia hiyp hiyo 13000 hakuna masihara

Ukipanda tilisho,kilimanjaro,bm za arusha kama unashukia Tanga au himo wao haiwahusu utalipa 45000 ile ile ya Arusha wanafanya hivyo kuepuka upigaji wa wafanyakazi na abiria wasio waaminifu sasa nyie sgr hamjifunzi kwa wenzenu?

Abiria wa pugu si apande daladala za gongo la mboto pugu kwenye sgr anafuata nini

Serikali sijui inafeli wapi ,hao wahuni ni kuwapa kesi ya uhujumu uchumi na wakija kwenye plea bargain unawapiga milioni 100 ili watoke...wakiwafanyia watu 10 huo upuuzi utaisha.
 
watanzania (baadhi) wajinga sana wanajifanya watalaamu na professional wa kila kitu, kwani Pugu hakuna station ya treni? na kwa nini iljengwa kama haina maana? low iq folks, emotions zimewajaa badala ya logic, sgr ina treni aina mbali mbali kuna ya kawaida ambayo itasimama kila kituo na kuna express ambayo itasimama vituo vikubwa tu, kipi ambacho hamuelewi hapo? nchi haiendeshwi kwa personal interest bali interest za wote, huko Pugu kuna watu wanaishi pia …
Huna akili
 
Ajabu kabisa nimejaribu hapa ni kweli ukikata tiketi ya pugu, siti inakuwa close maana yake mtu akitaka hiyo siti kwenda dom atakosa
Hili sasa ni tatizo la hao watu wa software, ilitakiwa hiyo seat iwe released baada ya abiria huyo kushuka pugu ili abira wa hapo hapo pugu aweze kuninunua tena hiyo seat.
Kwa mtindo huo mtu akiwa na laki anaweza hujumu behewa zima kwa kukata tu tiketi za pugu.
 
Huna akili

wewe mwenye akili nijibu kama ukipenda kwa nini kuna wamejenga station ya treni hapo kwa kutumia mabilioni ya fedha ? na siyo wao tu hata mkoloni pia alipojenga reli aliweka station miji midogo pia ni kwa nini unafikiri au wote hawana akili isipokuwa wewe tu ? maisha siyo kuangalia matakwa yako tu bali ya kila mmoja wetu pia …
 
Wanashindwa kuwa wabunifu. Watengeneza mabehewa ya Abiria wa njiani.

Na kwa treni inayoanzia Dar na kituo cha kwanza kiwe Ruvu siyo Pugu.

Shida tumejaza watu wasiofikira katika hizi Taasisi.
Wewe unafikiri behewa ni kama gari la mabox? Sio haraka hivyo, sema wasitishe huduma kwa vituo vya karibu mpaka hapo baadae watakapopata behewa nyingi zaidi.
 
Back
Top Bottom