Abiria wa Tanzania akamatwa Hong Kong na heroin ikiwa ndani ya mashine

Abiria wa Tanzania akamatwa Hong Kong na heroin ikiwa ndani ya mashine

Peak of shame to the country!
Kumbe zile barua za wafungwa ni za kweli bana.
Cha kufanya wajue nani members wa hilo syndicate linalosafirisha mashine toka Tz.
Lakini huwa hatusikii hukumu za hawa watu hata wakishikwa!
 
Mwakyembe si anakesha hapo kiwanjani..sasa huyu kapitia wapi tena?

KIA nayo ni international airport kaka. Wao wanaweka emphasis kwa JNIA, wanaacha milango wazi KIA! Tambarareeee!

Anaweza pia kupanda basi kwenda Mombasa au Nairobi, passport inasema ni Mtanzania, so, madawa yametokea TZ!
 
halafu mwakyembe anatuletea sanaa za kumakamata ras wa kuchonga ili ionekane ccm wanapambana na madawa.Mwakyembe kamkamate idd azan na ridhiwan nyambaf we.

Kwa Tz hii hii ninayoishi mimi hao uliowataja hawawezi kukamatwa labda uje utawala mwingine usiothubutu na kuweza tu bali pia kuchukua hatua kali na kutekeleza kwa vitendo.

Bado tunayo safari ndefu sana.
 
Kwa mara nyingine, maafisa wa Hong Kong katika kiwanja cha ndege wamefanikiwa kukamata dawa za kulevya zilizokuwa zinasafirishwa kutokea Tanzania safari hii zikiwa zimefichwa katikati ya chuma cha mashine.

Dawa hizo aina ya heroin zilikamatwa katika nyakati mbili tofauti kwa jumla zikiwa na kilo 1.5 na thamani ya dola milioni 1.3 za Marekani.

Maafisa hao wanasema kwa kuwa wamekuwa wakifuatilia kwa karibu nyendo za wauza dawa na mbinu za kuficha dawa hizo, walilazimika kukikata chuma cha mashine hiyo ili kuziona.

Adhabu ya kupatikana na dawa za kulevya huko Hong Kong ni faini ya dola milioni 5 za Kimarekani.

Taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti ya Serikali ya nchi hiyo na picha zinazoambatana na taarifa hiyo vimepachikwa hapo chini.

6366947_orig.jpg


8940017_orig.jpg


8668822_orig.jpg

Kifungo cha maisha na faini ya USD 5 million, lakini bado Watanzania hawakomi tu. Hakika sikio la kufa halisikii dawa!!!
 
huyu jamaa nae yani unapeleka spare part hong khong lazima udakwe
 
Kama kakamatwa 15/Agosti, ina maana aliondoka hapa 14/Agosti, siku ambayo Mwakyembe alidamkia JNIA! Bongo boma...
 
Inawezekana Bongo kuna kamtambo kakutengenezea hii kitu!!! Kwa nini asilimia kubwa ya haya madawa yanakamatwa yakitoka huku na sio kuingizwa?
 
Hii machine mbona Kama imechakaa ghafla baada ya kukata hicho Chuma au ilifungwa hapo kwanza kisha kikahamishiwa katika machine nyingine! Tazama kwa umakini hizo picha.
 
Mtu anataka alale maskini amke tajiri haya ndiyo madhara yake.
 
young stunna .mimi kwa mtazamo wangu mwakyembe hausiki kwa hili kwani pale kuna polisi anayelinda na kukagua kwani lazima watakuwa na intel so polisi wapo wapi ilo ndio lingekuwa swali la msingi?
 
Mwakyembe msanii sana, kumbe alivyotuzuga kuvamia hapa Airport alikuwa anataka kumvusha jamaa...
 
Hii machine mbona Kama imechakaa ghafla baada ya kukata hicho Chuma au ilifungwa hapo kwanza kisha kikahamishiwa katika machine nyingine! Tazama kwa umakini hizo picha.

haya ni matukio mawili tofauti. moja ni agosti 2 na nyingine ni jana agosti 15. Kwa vyovyote vile wana mashine zidi ya moja .
 
Hivi ina maana tumekosa biashara nyingine za kufanya kweli?? Mungu abadilishe fikra zetu.
 
Back
Top Bottom