Absalom Kibanda awakosoa vikali CHADEMA, asema "Ukishakula nyama ya mtu huachi", Lema amjibu

Absalom Kibanda awakosoa vikali CHADEMA, asema "Ukishakula nyama ya mtu huachi", Lema amjibu

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Kibanda.JPG


Mwanahabari mkongwe na Mchambuzi wa siasa Absalom Kibanda amekosoa maamuzi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwafukuza uanachama Halima Mdee na wenzake 18.

“Ni kweli Mdee na wenzake 18 walikosea. Msingi wa makosa yao ni kupinga ubabe wa kihistoria wa viongozi wenzao na kudai kwao haki kibabe. Ni kweli pia viongozi wakuu CHADEMA waliwahukumu kabla ya vikao. Kosa la kimaadili limetolewa 'hukumu ya kifo'.

“Huu ni ulaji wa kisiasa. CHADEMA inadai haki yake, akina Mdee wanapigania jasho lao. Orodha inaongezeka, hawakuanza na Davidi Kafulila, Zitto Kabwe, Wilbroad Slaa wala Kitila Mkumbo na hawatamaliza na hawa Wanawake 19. Ukishakula nyama ya mtu huachi,” – Kibanda.

Kumbuka kuwa Kibanda ni mmoja wa waandishi wakongwe waliowahi kufanya kazi kwa ukaribu na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na walikuwa na ukaribu hata nje ya masuala ya kikazi.

Kibanda aliwahi kuwa Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Free Media, wachapishaji wa magazeti ya Tanzania Daima na Sayari ambayo ni mali ya Mbowe, pia Kibanda amewahi kuinia matatizoni mara kadhaa kwa kuikosoa Serikali na kuonekana yupo upande wa CHADEMA, hivyo kwa kauli hiyo ni wazi kuna vitu havipo sawa.

GODBLESS LEMA AMJIBU
Baada ya kauli hiyo, mwanachama mkongwe wa CHADEMA, godbless Lema naye akamjibu kwa kuandika hivi:

"Kama utaendelea KUKAUKIWA nakushauri uende kwa Mwamposa niliambiwa anatoa mafuta ya kuvunja nira ya KUKAUKIWA. Hata hivyo jambo gumu ktk jamii ni pale wazee wenye masharti ya kula wanapo kuwa na njaa kuliko vijana wasio na masharti na diet. Sijui njaa ni nini sasa ?"
 
Kwa hiyo ni haki yao kufoji nyaraka ili mradi kupinga matumizi ya nguvu kudai haki?
Hii nchi ikija kupata maendeleo hata angalau kuwafikia Kenya basi ujue Mungu amekufa.
Nchi ina akili takataka sana.
 
Mbona Kibanda ameandika kwa mihemko sana?

Anaposema; "Ni wazi kuwa viongozi wa Chadema waliwahukumu kabla ya vikao" anamaanisha nini?

Vile vikao vya KK na baadae Baraza Kuu hakuviona?

Ajabu Kibanda anazungumzia haki ya kina Mdee, haki ipi, ya kufoji? au ya mtu kuchomolewa gerezani kimya kimya usiku? Hawa waandishi na njaa zao wanataka tuwe na taifa lisiloheshimu sheria.

Sasa naanza kuamini, kuna kundi la waandishi wa habari [ wakujitegemea na wa vyombo mbalimbali] wamenunuliwa na serikali ili kuichafua Chadema, kwa kuwatetea wale wahuni 19 bungeni.

Yule wa kwanza ameshajulikana yupo humu ndani, huyu Kibanda ni wa pili, tusubiri wa tatu, wanne, .....

Samia na serikali yake ni corrupt, kuwalipa wale wahuni posho na mishahara kule bungeni, na kuwapa posho hawa waandishi njaa kueneza uzushi.Mbowe jitoe kwenye meza ya mazungumzo.
 
Ndiyo mjue kwanini mzungu anaweza kumtawala mtu mweusi kirahisi kuliko kufuga samaki. Jitu linaunga mkono kugushi nyaraka za bunge na mishahara ya kibunge,posho za vikao na linaona Ni kitu sahihi na kutetea. Jinga Sana
Yaani mwandishi wa habari ana support kugushi nyaraka kubwa kama za ubunge. Tanzania tuna kazi hawa eti ndiyo wadai haki wetu !🤔
 
Wadau naomba mnikumbushe kidogo kama hiki kibanda SII kibanda saliti misili ya akina COVID na wasaliti wengine maslahi mamluki waliotumika kukihujumu chadema🤔
 
Kwa hiyo ni haki yao kufoji nyaraka ili mradi kupinga matumizi ya nguvu kudai haki?
Hii nchi ikija kupata maendeleo hata angalau kuwafikia Kenya basi ujue Mungu amekufa.
Nchi ina akili takataka sana.
Kipimo chako cha maendeleo ni Kenya!
 
Kwa hiyo ni haki yao kufoji nyaraka ili mradi kupinga matumizi ya nguvu kudai haki?
Hii nchi ikija kupata maendeleo hata angalau kuwafikia Kenya basi ujue Mungu amekufa.
Nchi ina akili takataka sana.
Forgery is a criminal offence na inahitaji forensic investigation. Hivyo mpaka hapo uchunguzi utakapofanyika kuhusiana na hizo hand writing na kugundulika ni forged then we will be in the good position kusema wamefoji ila kwa wakati huu hatuna evidence za kusema walifoji. Tuwatendee haki pia hao wakina mama!
 
Back
Top Bottom