Absalom Kibanda: Sasa sitaogopa kitu na sina cha kupoteza, nitafichua kila kitu

Anasema alipolazwa hospitalini nchini Afrika Kusini serikali ilimtuma mtu mmoja kwenda kuona maendeleo yake. Uongozi wa hospitali uliamua kumficha ili kunusuru maisha yake.

Serikali ilimtuma mtu! Basi mchawi si anajulikana kwanini asiwe wazitu sasa kulikoni anavyoumauma maneno na mwisho wake watamtambarizia mbali kabla ya kufunguka, ama anataka apate shavu kama la ulimboka?
 
jamani maumivu ya kung'olewa kucha na meno na kutobolewa jicho bila ganzi si mchezo. Anasema sasa ana ujasiri upi? Anajua fika kuwa wahusika wako juu ya sheria wakimtaka wanampata. Hii nchi jamani!!

Sasa si awaani kabla hawajamtaka na kumpata?
 
kumbe alikuwa anaficha?????hili ndilo tatizo la wanahabari wa tanzania.wanaficha habari muhimu.BADILIKENI SASA.

Na kuanika za ovyo na zisizokuwa na manufaa kwetu, mara cjui owoya na nani cjui wafumwa live ujinga mtupu mimi na yule watajifunza nini hapo sasa
 

Ngoja kibanda alipwe nae atamuachia Mungu
 
Ulimboka alisalitiwa na madaktari na yeye akaamua kula chake na kusaliti wengine
 
Jamani aliye record hicho kipindi atusaidiee link please !!!
 
Bwana ABSALOM KIBANDA aliyasema hayo jana wakati anajibu swali na mmoja wa watu waliokuwa wakifuatilia kipindi cha JENERALI ULIMWENGU ON MONDAY kinachorushwa na kituo cha television cha CHANNEL TEN.

Mwananchi huyo alimshambulia yeye na watu wengine kama akina STEPHEN ULIMBOKA kuwa wamekuwa wakiahidi kufunguka na kusema ukweli lakini wanapopewa nafasi ya kusema hawasemi chochote cha maana.

Aidha Bwana KIBANDA alivishukuru vyombo vya dola na hasa jeshi la POLISI, viongozi binafsi wa dola waliostaafu na walioko kazini kwa jinsi ambavyo wako karibu naye kusaiidia kuupata ukweli wa tukio lililomkumba.

Mytake: Binafsi nilifurahishwa na majibu ya Bwana KIBANDA kwani alionesha ukomavu yeye kama Mwandishi wa habari. Hakuna sababu yoyote ya yeye kuanza kulalalmikia vyombo vya dola, watu fulani fulani ama kikundi cha watu wakati hana uhakika wa nani hasa anahusika na tukio hili.

Watu wengine waige mfano wa KIBANDA wa kuheshimu na kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola pindi wanapofikwa na matukio kama haya badala ya kuingiza chuki, siasa na kuepuka kutumiwa na watu kwa ajili ya kujipatia umaarufu katika jamii kisiasa, kijamii na hata kiuchumi.
 
na mtu toka taasisi nyeti ya taifa hili.

Aliambiwa jambo ajiangalie wapi na mtu huyo....

gari limepaki la taasisi moja

Amekubali hali iliyompata kama chachu ya kusimamia anayoyaamini. Hata alipokuwa anasita sasa hatakuwa mwoga.
Anaogopa kutaja jina la hiyo "taasisi nyeti..." anaogopa kutaja huyo aliyeambiwa ajitahadharishe nae, anaogopa kutaja chochote halafu anatuambia kuanzia sasa atakuwa jasiri, ataandika kila kitu. Ridiculous.
 
Ngoja apigwe mwingine kwa unafki huu wa kibanda na ulimboka mptapigwa tu waandishi wa habari
 

Vipi kuhusiana na Kujiondoa Free Media ameongelea?
 

umeiona na kuisikiliza vzr ile video ya lwakatare? Kaisikilize km utaongea haya tena
 

mawazo yako yana mapungufu sana, kama unasema Kibanda ni mwongo tupe ukweli unaoujua wewe.
 
Hivi hawa watu wakishang'olewa meno na kucha na akina Ramadhani Ighondi (read TISS) Pia wanakuwa wameng'olewa AKILI?!

Ni mambo ya ajabu sana akina Harrison Mwakyembe, Dr. Ulimboka na sasa huyu Kibanda wote walitishia Nyau kwamba watasema kila kitu. Lakini walipopewa fursa ya kusema kama huyu Kibanda wote wameishia kusema ETI WANAMUACHIA MUNGU.

Kama Kibanda anafikiri hao wabaya wake wamelala, he is absolutely wrong. Tena kwa matamshi yake hayo ya CH 10 ndiyo amaweka MAISHA YAKE REHANI.
 
Tatizo hawa nao ni awanafi itakuaje mpaka leo amekalia ukweli wakati anajua yeye ni mtu muhimu katika mustakabali wa hali ya mabo na migogoro ya kisiasa inayoendelea nchini mwetu?

MY take: Watanzania tunataka watu wenye dhamira safi na maendeleo ya kweli ya demokrasia ya taifa hili wawe wawazi ili watutoe wasiwasi sisi wananchi kutokana na hofu tunayopandikizwa na wanasiasa kama
mwigulu
 
kubenea alisubiri sana uchunguzi mpaka leo, mtu akijua unajua ukweli atakumaliza kabla hujasema huo ukweli...


You are damn right; na usikute hata ulimboka naye amekuwa contained kwa technique hiyo-hiyo ya kusubirishwa kitu. Kesi ya Ulimboka kwa mfano ndo ipo obvious kabisa kama jua kutoka Mashariki. Somebody got terribly hurt kwenye department ile and that's all you'd need ku-prove involvment. Call them to the parade, mwenye kovu pale mahala ndo huyo aligongwa.... eti intelligence.; stupid fools. Nyerere alikuwa ana-contain political challenge, but he was very careful with the human body. Waseme tu ukweli taifa lijue.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…