ACACIA Mining PLC set to close loss-making mine as Tanzania export row deepens

ACACIA Mining PLC set to close loss-making mine as Tanzania export row deepens

Madhara yake ni yepi, kama Acacia ina wana hisa world wide? Hatua stahiki ni mahakamani.
 
So wanataka kutuambia kua ule mchanga (makapi) ndio ulikua wanautegemea kwa kutafuta faida ya kila siku??
Kama ndivyo je dhahabu inayopatikana nayo wanaifanyia nini??
Wafunge tu waondoke wezi hawa, washatuibia sana

Bahati mbaya Tanzania kila mtu mjuaji hata ambaye hana uelewa wowote. Uzalishaji wa dhahabu wa mgodi wa Bulyanhulu 60% ni gold bar. Iliyobakia 40% ni concentrate. Mgodi tangu uanze, the highest profit ambayo umewahi kutengeneza si zaidi ya 20% (hiyo ni bila ya kuondoa gharama za uwekezaji). Kama faida ni 20% (achilia mbali kipindi hiki ambapo wanasema hautengenezi faida), halafu ukazuia kuuza 40% ambayo ni concentrate, hiyo faida itapatikana vipi?

Ni very layman thinking kuita concentrate ni makapi. Kama mtu hajui ni afadhali asichangie, asome na kuuliza ili kujenga uelewa.

Kwa wasioelewa, hakuna mgodi ambao ni mgumu kuuendesha na kuujenga kama wa underground. Bulyanhulu ndiyo mgodi pekee wa underground. Acacia wakiondoka leo, wakiamua kuufunga mgodi wa Bulyanhulu, itakuwa vigumu sana kuipata kampuni nyingine itakayochimba dhahabu katika mgodi huo ambao kwa sasa nadhani utakuwa upo kwenye kina karibia cha kilometer 2. Hakuna hata mchimbaji mdogo atakayeweza kuingia chini huko kuchimba na akatoka hai. Joto lililopo ambali huo linatosha kukua mara moja. Lakini pia bila ya hewa ya kutosha kupelekwa huko chini, hakuna anayeweza kuishi.

Migodi mingi ya kina hicho, katika baadhi ya nchi inafungwa siyo kwa sababu ya kwisha kwa dhahabu bali ni kutokana na gharama kuwa kubwa za kupoza hewa na upelekaji wa hewa. Sisi tupo karibu ya Ikweta, temperature gradient kadiri unavyoshuka chini ni juu sana, ndiyo maana ukichimba shimo refu kiasi, hata kama ungali kwenye udongo, unaona mwongezeko wa joto.

Uamuzi wa kipuuzi hautalisaidia Taifa letu. Hata kama mgodi huu hautengenezi faida lakini siyo kwamba hauna faida kwa Taifa. Kumbukeni una wafanyakazi wengi sana ambao wanalipa kodi, wanachangia kiwango kikubwa kwenye mifuko ya jamii na wanategemeza familia na wategemezi, wanachangia mzunguko wa fedha, kuna contractors na suppliers wanaolipa kodi na wana waajiriwa wanaolipa kodi pia. Dhahabu inayozalishwa inalipiwa mrabaha wa 4% on production (na kwa migodi inayotengeneza faida, hii 4% huwa ni karibia 15-20% ya net profit). Ukiweza kuwafanya watu wako wengi wakaajiriwa, hata kama waajiriwa hawalipi kodi, bado mapato ya serikali yatapaa, na maisha ya watu wako yatakuwa mazuri. Siyo kodi ya serikali ndiyo inayoboresha maisha ya watu bali ni ajira.

Ujinga wetu wengi tunafikiria madini yanachukuliwa tu kutoka ardhini bila ya kujua kuna kazi ngumu sana ya kuweza kuyatoa.

Miaka ya nyuma, tulitaafisha migodi yote toka kwa makampuni, tukawapa STAMICO wachimbe. STAMICO haikuweza kuendesha uchimbaji hata wa mgodi mmoja achilia mbali kufanya utafiti. Leo hata tukiyafukuza makampuni ya kigeni yote, hatutaweza kuendesha uchimbaji katika mgodi hata mmoja mkubwa kwa sababu hatuna uwezo wa kugharamia kikamilifu ili kuweza kupata faida.

Uendeshaji wa uchimbaji madini ni aghali sana, unahitaji organization ya hali ya juu sana, ndiyo maana hata katika mataifa haya makubwa, makampuni ya uchimbaji siyo mengi. Duniani kote, ukienda utakuta makampuni ya uchimbaji madini ni haya haya - Barrick, Anglo, BHP, Newmont, Kinross, Placedome, etc. Wenzetu Ghana walijaribu lakini baadaye walinyosha mikono kuwa hawawezi.
 
hiyo ni report yakwenu sasahivi tuna report mpya inayoonesya data mpya zaidi kwa kuambiwa kuna madini zaidi...

swali lingine hizo report unazo ziandika wewe umezifanyia uchunguzi wewe au hao acacia? na nizamwaka gani bro?
 
hiyo ni report yakwenu sasahivi tuna report mpya inayoonesya data mpya zaidi kwa kuambiwa kuna madini zaidi...

swali lingine hizo report unazo ziandika wewe umezifanyia uchunguzi wewe au hao acacia? na nizamwaka gani bro?

Mgodi wa Bulyanhulu, utafiti wake umefanyika kwa miaka mingi kuanzia miaka ya 1970. STAMICO walifanya wakaishiwa pesa na utaalam. Wakafuata Placedome, wakaja Sutton Resources na baadaye Barrick. Utafiti ndiyo unaowezesha mgodi kuanza kujengwa. Mgodi siyo shamba la mahindi au maharage ambalo mazao yake huweza kubadilika kufuatana na msimu au hali ya hewa. Taarifa zilizopatikana kabla ya kuujenga mgodi ni hizo hizo mpaka leo, na ndiyo zinazoongoza uchimbaji na uchenjuaji.

Taarifa hizo hupatikana baada ya kazi ya muda mrefu iliyohusisha watu wengi wenye ujuzi mbalimbali. Sisi ndiyo tuliofanya utafiti. Nilikuwepo pia miaka ya mwanzo ya uzalishaji. Baadaye niliondoka na kuendelea na kazi hizo hizo ndani na nje ya Tanzania mpaka leo. Alichoandika Mruma na wenzake hakipo katika Ulimwengu huu labda kama ni ugunduzi mpya. Na kama ni ugunduzi mpya basi ungekuwa kwa mgodi mpya siyo huu ambao taarifa zake zinafahamika sana.
 
Kwani sisi huwa tunaeleweka basi Mkuu. Ni kushabikia tu vitu kama majuha. Tunashabikia report ya kuwananga ACACIA wakati huohuo hatusomi tafiti nyingine zilizofanywa huko nyuma zinazoonyesha kwamba hatuwezi kumudu uwekezaji wa smelter nchini. Halafu hawa watu wanayoyafanya yote yalipewa baraka zote za serikali hiyohiyo inayolialia leo. Upuuzi mtupu. Binafsi nataka kuona independent analysis ya hasara tunayoambiwa tumeingizwa na hawa ACACIA kabla sija comment zaidi.
Mkuu uko sahihi kabisa, kuna comments ukisoma humu unabaki unashangaa, yaani ni aibu. Nimechukua kipande kidogo cha document ya ACACIA kinachoonyesha nchi zinazotuma makinikia zao kwenye smelter moja tu kwani ukiijenga peke yako na kutegemea migodi miwili tu itakua hasara na migodi itafungwa kabla hela yako haijarudi. Yaani mtu anasema wafukuzwe tu kama ni rahisi kiasi hicho.
upload_2017-5-28_19-37-36.png
 
Bottom line...tuna mashaka na tungependa a fair deal.

Nawasubiri wale waliosema tutashitakiwa na kulipa pesa waje
 
Sielewi mengi kuhusu kemia na utafiti. Pia naweza kuwaza ya kwamba kampuni labda liko tayari kudanganya.
Lakini naona mashaka kuhusu taarifa ya maprofesa. Kama kweli asilimia ya dhahabu ni mara kumi jinsi ilivyotangazwa na kampuni - basi kweli Tanzania ingekuwa kiongozi duniani kwa uzalishaji wa dhahabu. (Sasa Tz inatoa tani 40 za dhahabu kwa mwaka, China mkubwa duniani karibu tani 400/mwaka). Hata wakiweza kuficha dhahabu hapa TZ na kuipeleka nje - soko hili si kubwa vile ya kwamba inaweza kufichwa kwenye soko la dunia. Tofauti ingeonekana - lakini hakuna taarifa ya vyanzo visivyojulikana! na ni soko linalotazamiwa sana na wenye hisa na wawekezaji wanaoshindana kati yao.
(hapa tofauti na soko la almasi ambako inajulikana kuna vyanzo visivyoweza kutajwa "blood diamonds")

Hii inanipa mashaka kuhusu taarifa ya uchunguzi wa makontena. Waongeze wengine wa nje kuthebitisha au kupinga!
 
May 27, 2017 | The Telegraph

Mgodi wa Bulyanhulu huenda ukafungwa kufuatia mfululizo wa hasara baada ya Serikali kusitisha usafirishwaji wa mchanga kwenda nje.

Zuio usafirishaji wa mchanga wa madini kwenda nje ya nchi, lilipelekea bei ya hisa za Kampuni ya ACACIA kutetereka kwenye Soko la Hisa la Uingereza (LSE) na Dar es Salaam (DSE).



=======
Acacia Mining is preparing to close a loss-making mine after a row over exports with the Tanzanian government escalated.

Shares in the FTSE 250 gold miner plunged nearly 40pc last week after a report by the Tanzanian government accused it of under-representing the amount of gold in the concentrate it exports, potentially depriving the country of millions in royalties.

The government said that Acacia’s gold output was 10 times greater than it claimed – a level that would “make it third-biggest gold miner in the world”, the company said.

The findings, published with great fanfare on national TV, mean an export ban on gold concentrate imposed at the start of March is likely to continue indefinitely. Acacia is still able to ship out gold bars, which make up 70pc of its output, but estimates that it is losing $1m (£780,000) in revenue every day.

The company, which is dependent on its three mines in Tanzania, has been stockpiling gold concentrate in the hope of a quick end to the dispute. But it is now preparing to close Bulyanhulu mine to stem mounting losses.

Acacia is dependent on three mines in Tanzania
Around 45pc of Bulyanhulu’s output is gold concentrate, and the losses from stockpiling production cannot be offset by sales of gold bars.

Acacia’s Buzwagi and North Mara mines will remain operational for now.

Some observers suggest that Tanzania’s president, John Magufuli, is trying to force Acacia to fund a new gold-smelting industry, but experts say the country’s output is too small for this to be economically viable.

Acacia is petitioning the government to allow a third party to assess its output.

“We need to defend ourselves,” said a person close to the situation. “The numbers are not believable. We are not guilty of a multi-billion dollar fraud.”

A second government committee is looking at gold concentrate production in Tanzania dating back 15 years - roughly the time-span that Acacia, formerly African Barrick, has been operating there. As Acacia is by far the largest miner in the country, it is thought to be the focus of the probe.
Hii inapaswa kuwa African movement against wanyonyaji. Tuburuzane mahakamani tu ili Dunia ijue Africa inabadilika now
 
Sakata la mchanga wenye dhahabu la Acacia Mining Plc mambo bado mabichi-thejury is still out!
 
Mpaka wanataka kufungu mgodi, kweli wameshikwa! JPM endelea kukomaa soon utaona uzalishaji wa dhahabu unaongezeka
 
Mgodi wa Bulyanhulu, utafiti wake umefanyika kwa miaka mingi kuanzia miaka ya 1970. STAMICO walifanya wakaishiwa pesa na utaalam. Wakafuata Placedome, wakaja Sutton Resources na baadaye Barrick. Utafiti ndiyo unaowezesha mgodi kuanza kujengwa. Mgodi siyo shamba la mahindi au maharage ambalo mazao yake huweza kubadilika kufuatana na msimu au hali ya hewa. Taarifa zilizopatikana kabla ya kuujenga mgodi ni hizo hizo mpaka leo, na ndiyo zinazoongoza uchimbaji na uchenjuaji.

Taarifa hizo hupatikana baada ya kazi ya muda mrefu iliyohusisha watu wengi wenye ujuzi mbalimbali. Sisi ndiyo tuliofanya utafiti. Nilikuwepo pia miaka ya mwanzo ya uzalishaji. Baadaye niliondoka na kuendelea na kazi hizo hizo ndani na nje ya Tanzania mpaka leo. Alichoandika Mruma na wenzake hakipo katika Ulimwengu huu labda kama ni ugunduzi mpya. Na kama ni ugunduzi mpya basi ungekuwa kwa mgodi mpya siyo huu ambao taarifa zake zinafahamika sana.
 
Watu wameiba tangu wakiwa Barric Gold tunakuja kulialia wakiitwa Acacia na all days mliambiwa hawa wanaiba mkajifanya viburi,wako wapi wabunge walioshabikia?
At that time Magufuli alikua Mbuge na hata siku moja hakuwahi kutoa hoja kupinga issue za barrick


siasa siasani
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Tumeibiwa sana, tena sana ila wasiwasi wangu ni hii report kutoaksi ukweli, Sisi kama wachumi tulitaka Report ya ukweli ili tuichambue na kutoa majibu sahihi kwa maendeleo ya taifa leo.
Najua kwa mtu aliyesoma au anayefanya Biashara anajua kitu kinaitwa Operating Cost.

Ili tujue tunaibiwa Kiasi gani, inabidi tujue Price of minerals(gold, Copper, Silver..) in Tanzania sio huko Uk, the Operation cost mpaka unapata hayo Makanikia ndio tujue faida. halafu tukokotoe hiyo faida(Tax,....) tuone tunaibiwa shilingi ngapi. Sio kutumia Selling price ya soko la dunia eti ndicho tunachoibiwa as if huyo investor anaokota hayo madini juu ya arthi kama mchanga wa bahari.

Narudia tena tumeibiwa sana na simutetei huyo mwekezaji wala sina hisa naye ila ukweli ni kwamba kuna process ndefu ili upate madini(Running Cost).
  1. Exploration
  2. Surveing
  3. excavating
  4. Drilling of rock
  5. ...
  6. ...
  7. ...
  8. Manpower
  9. Machineries
  10. Theft
  11. Processing
  12. transportation
  13. Sinking Cost
  14. Marketing & marketing
  15. Interest from Banks
  16. Consultation
  17. Insurance .......................
Hayo ni baadhi ya mambo ambayo tulihitaji yawepo kwenye report pamoja na Mkataba wenyewe ili wachambuzi tuliyibobea tuyafanyie kazi halafu tutoe ushauri nini kifanyike, ila kama ndio riport inasema kilichomo kwenye makanikia tu hiyo itakua report ya kujinyakulia umarufu wa kisiasa ambao ndio iliyotufikisha hapa tulipo. Bila kusahau hadi leo watanzania wanamsifia Nyerere kwa Maamuzi ya kutoruhusu uchimbaji madini miaka hiyo eti kwa kisingizio cha kuibiwa maamuzi ambayo ni ya juha kwelikweli. poor administration system kwani mwenye nyumba lini akajua kujenga gorofa ila anajiri wasomi(Engerneer) kumjengea kutokana na usimamizi mzuri na haibiwi.

Tatizo hapa ni mkataba! mkataba! mkataba! mkataba! Mibovu sio Makanikia. na magufuli ni sehemu ya tatizo kwani alichangia hata juzi kupitisha mikataba ya gas kwa hati ya dharura. "The problem cannot be Solved by the same person who created it"
 
Nadhani hili ndilo lililokuwa linatafutwa kwa muda mrefu. Lengo limetimia, sasa tuwe tayari kwa mapambano ya kisheria.
 
Sielewi mengi kuhusu kemia na utafiti. Pia naweza kuwaza ya kwamba kampuni labda liko tayari kudanganya.
Lakini naona mashaka kuhusu taarifa ya maprofesa. Kama kweli asilimia ya dhahabu ni mara kumi jinsi ilivyotangazwa na kampuni - basi kweli Tanzania ingekuwa kiongozi duniani kwa uzalishaji wa dhahabu. (Sasa Tz inatoa tani 40 za dhahabu kwa mwaka, China mkubwa duniani karibu tani 400/mwaka). Hata wakiweza kuficha dhahabu hapa TZ na kuipeleka nje - soko hili si kubwa vile ya kwamba inaweza kufichwa kwenye soko la dunia. Tofauti ingeonekana - lakini hakuna taarifa ya vyanzo visivyojulikana! na ni soko linalotazamiwa sana na wenye hisa na wawekezaji wanaoshindana kati yao.
(hapa tofauti na soko la almasi ambako inajulikana kuna vyanzo visivyoweza kutajwa "blood diamonds")

Hii inanipa mashaka kuhusu taarifa ya uchunguzi wa makontena. Waongeze wengine wa nje kuthebitisha au kupinga!
Inawezekana kiwango cha madini hayo kwenye huu mgodi isiwe kama makisio ya findigs yanavyoonesha kutokana na utafiti wa serikali but i keep an open mind kutokana na baadhi ya maswala yaliyogundulika yanayoonesha kwamba kunaweza kuwa na mwanya wa ku temper na mchanga huo.
Kwa mfano kama TMAA walikua wanachukua sample kwenda kupima kiwango cha madini harafu hawaweki seal kwenye makontena kuna uwezekano mchanga huo ulikua unapakuliwa kiasi na kushindilia madini au mabaki mengine ya madini bila TMAA kujua.

Kuna mambo mengi sana ambayo yana maswali yasiyo na majibu kwa upande wangu ila ninachoamini ni kwamba tutafikia mwafaka mzuri tu. Sio vibaya pale kunapokua na shaka tujiridhishe maana hata mikataba yetu ina viashiria vya personal interest so let the Gvt do the work
 
All in all in bad english, why in London there is profit not in Tanzania, why the ban has affected ashashia more than any other coy operating in Tanzania?. Is the ashashia ready to tell us the total revenue generated per year and the amount paid as Mrahaba from thirty percent from ore?. Can we get information of what is extracted from the end-smelters for the pas five years.?. If the Tanzania operation is insignificnat why the Presdintail probe has caused fall of its shares?. They tell us the way forward looking for the independent valuer/auditr to measure the mchange wont solve problems. We are hitting the pot carrying the snake,
 
Back
Top Bottom