Mkuu hii ni akaunti ya akiba ya muda maalum. Ni akaunti ambayo kwa lugha ya kigeni inatwa Fixed Deposit Account. Kwa anayoisemea mdau ni kwamba yeye ameingia mkataba na benki kwa kuweka fedha yake na kisha benki wao wanamlipa riba/interest kwa kila mwezi kwa kipindi chote cha miaka mitatu aliyoingia mkataba.
Baada ya muda huo ukipita/maturity basi atarudishiwa fedha ile aliyoweka mwanzo/ principal amount kwa kuwa alikwisha faidika na riba iliyokuwa inalipwa kila mwezi. Akaunti hii kwa CRDB inaitwa Thamani akaunti.
Kuna akaunti za muda maalum pia ambazo unaweza ukaweka fedha kwa miezi mitatu, miezi sita, tisa na kuendelea. Huwa ni akaunti za muda maalum. Akaunti zote hizi pamoja na hiyo ya juu ya Thamani unaweka kiasi mwanzoni na hutoruhusiwa kukitoa mpaka muda wa mkataba kuisha. Endapo utalazimika kuvunja mkataba kabla ya muda kuisha basi kuna mambo ambayo yatapaswa kufuata/terms and conditions zitahusika.
Kwa wanaume kuna akaunti inaitwa Dhahabu akaunti ambayo inampa fursa mwanaume kujiwekea akiba kila mwezi kwa muda usiopungua miaka mitatu/mkataba ni miaka mitatu. Fedha hizi za kila mwezi zaweza wekwa kwa mteja kuweka fedha taslimu/cash money kila mwezi au akaomba utaratibu wa fedha kuhamishwa kutoka akaunti yake moja ya CRDB bank kwenda kwenye akaunti hii ya dhahabu. Huduma hii inaitwa Standing Order ambapo itasetiwa kwenye mfumo kiasi kwambi kila tarehe fulani ya kila mwezi kiasi fulani cha fedha kitahama kutoka akaunti aliyochagua mteja kwenda akaunti yake ya Akiba ya Dhahabu.
Kwa wanawake wana akaunti inaitwa Malkia akaunti ambayo yenyewe mkataba wake ni mwaka mmoja tu. Na kipindi chote hicho akaunti zote za Malkia na Dhahabu zinapata riba kila mwezi.
Kama una swali waweza uliza mkuu.
Sent using
Jamii Forums mobile app