Account gani ya bank itatunza pesa zangu mpaka 2020 bila ku-draw??

Account gani ya bank itatunza pesa zangu mpaka 2020 bila ku-draw??

Mkuu hii ni akaunti ya akiba ya muda maalum. Ni akaunti ambayo kwa lugha ya kigeni inatwa Fixed Deposit Account. Kwa anayoisemea mdau ni kwamba yeye ameingia mkataba na benki kwa kuweka fedha yake na kisha benki wao wanamlipa riba/interest kwa kila mwezi kwa kipindi chote cha miaka mitatu aliyoingia mkataba.

Baada ya muda huo ukipita/maturity basi atarudishiwa fedha ile aliyoweka mwanzo/ principal amount kwa kuwa alikwisha faidika na riba iliyokuwa inalipwa kila mwezi. Akaunti hii kwa CRDB inaitwa Thamani akaunti.

Kuna akaunti za muda maalum pia ambazo unaweza ukaweka fedha kwa miezi mitatu, miezi sita, tisa na kuendelea. Huwa ni akaunti za muda maalum. Akaunti zote hizi pamoja na hiyo ya juu ya Thamani unaweka kiasi mwanzoni na hutoruhusiwa kukitoa mpaka muda wa mkataba kuisha. Endapo utalazimika kuvunja mkataba kabla ya muda kuisha basi kuna mambo ambayo yatapaswa kufuata/terms and conditions zitahusika.

Kwa wanaume kuna akaunti inaitwa Dhahabu akaunti ambayo inampa fursa mwanaume kujiwekea akiba kila mwezi kwa muda usiopungua miaka mitatu/mkataba ni miaka mitatu. Fedha hizi za kila mwezi zaweza wekwa kwa mteja kuweka fedha taslimu/cash money kila mwezi au akaomba utaratibu wa fedha kuhamishwa kutoka akaunti yake moja ya CRDB bank kwenda kwenye akaunti hii ya dhahabu. Huduma hii inaitwa Standing Order ambapo itasetiwa kwenye mfumo kiasi kwambi kila tarehe fulani ya kila mwezi kiasi fulani cha fedha kitahama kutoka akaunti aliyochagua mteja kwenda akaunti yake ya Akiba ya Dhahabu.

Kwa wanawake wana akaunti inaitwa Malkia akaunti ambayo yenyewe mkataba wake ni mwaka mmoja tu. Na kipindi chote hicho akaunti zote za Malkia na Dhahabu zinapata riba kila mwezi.
Kama una swali waweza uliza mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kwa hii Dhahabu account naweza kuweka hakiba kuazia kiwango gani cha fedha kwa mwezi tafadhali.
 
Mkuu kwa hii Dhahabu account naweza kuweka hakiba kuazia kiwango gani cha fedha kwa mwezi tafadhali.
Laki moja kiongozi unapofungua kama kianzio lakini waweza weka kuanzia 50000 kwa mwezi kama kiwango cha chini.
 
Ni wazo zuri kuweka fedha benki kwa kipindi fulani au muda mrefu hasa kwa wale ambao kwa muda fulani wanakuwa hawajabuni biashara au kutokuwa tayari kupambana na risk. Kinachofanyika benki ni wewe kuwapatia fedha zako na wao kuzifanyia biashara kwa niaba yako na baadaye mnagawana faida kama sio hasara,cha muhimu hapo ni kubuni biashara. Fedha haitakiwi kukaa benki muda mrefu inatakiwa kuingia na kutoka.Ikikaa benki maana yake tumeshindwa kuifanyia kazi na mwisho wa siku tunapata gawio dogo ambalo sisi tunaliona ni gawio kubwa.
Somo zuri sana hili.
 
Unajua kuna watu wanatafuta sifa !! Tunaomba u attach mkataba huo hapa tuone. Otherwise ni uongo ulokomaa
Mkuu sio kila kitu mtu anapaswa thibitisha kwa kuweka nyaraka zake huku kwenye mtandao. Kumbuka pindi mtu aingiapo mkataba wa aina hii anapewa kielelezo ambacho ndicho kinacho mtambulisha yeye kwa benki husika. Hapa tunazungumzia FDR Receipt.

Ametoa option ya wewe kutembelea tawi la karibu la benki tajwa na kupewa maelekezo sahihi. Pia tukumbuke pia benki hizi zina website na huko wameeleza akaunti zote na features zake, je hili umeshindwa?. By the way hii akaunti ilipoanzishwa ilikuwa na riba ya faida ya 13% kwa mwaka, baadaye ikashuka kulingana na mahitaji ya fedha.

So sio kila kitu tunapaswa kubisha, tujifunze kutafuta taarifa na njia za utafutaji pia ni nyungi. Benki zote zina tovuti na wanaeleza in a nut shell akaunti zao. Ukiweza kufika tawi la karibu la benki unayotaka pia ni vyema.
 
Huyo aliewekeza 50,000,000 nakupata kila mwezi 500,000 inamaana kwa mwezi anapata riba ya 1% ya kiwango alichowekeza. Je itakuaje mimi kapuku ninaedunduliza mpaka nikapata 1,000,000 kwa riba ya 1% ni sh.10,000. Tafakari, chukua hatua, Songa mbele...! Kumbuka Benki zetu hazijawahi kuwa rafiki kwetu sisi hata siku moja na huwa ninaamini sio lengo lao. Anza kitu.
 
Huyo aliewekeza 50,000,000 nakupata kila mwezi 500,000 inamaana kwa mwezi anapata riba ya 1% ya kiwango alichowekeza. Je itakuaje mimi kapuku ninaedunduliza mpaka nikapata 1,000,000 kwa riba ya 1% ni sh.10,000. Tafakari, chukua hatua, Songa mbele...! Kumbuka Benki zetu hazijawahi kuwa rafiki kwetu sisi hata siku moja na huwa ninaamini sio lengo lao. Anza kitu.
Watu wanatakiwa waelewe nini maana ya benki;na wao wanapata wapi fedha za kujilipa mishahara
 
Huyo aliewekeza 50,000,000 nakupata kila mwezi 500,000 inamaana kwa mwezi anapata riba ya 1% ya kiwango alichowekeza. Je itakuaje mimi kapuku ninaedunduliza mpaka nikapata 1,000,000 kwa riba ya 1% ni sh.10,000. Tafakari, chukua hatua, Songa mbele...! Kumbuka Benki zetu hazijawahi kuwa rafiki kwetu sisi hata siku moja na huwa ninaamini sio lengo lao. Anza kitu.
Ni sawa kabisa bro. Lkn ukumbuke pia kwmba taasis za kifedha km benk biashara ndio kibaumbele...km unataka pesa za mteremko nenda kwny vikund vya "pesa za mfuko wa Rais" au zile za manispaa zinazotoka hazina kuu ya Taifa!
 
Hii ndo jinc ya kutenez profit, au kuna njia nyngne kw taasis za kfedha kujitenezea faida??
Wanaonufaika ni bank na si mteja,watu wakikataa kupeleka fedha bank,bank zote zinakufa na watumishi wote wa bank wanakosa ajira.
 
Wanaonufaika ni bank na si mteja,watu wakikataa kupeleka fedha bank,bank zote zinakufa na watumishi wote wa bank wanakosa ajira.
Banking ni biashara. Bila mtaj huwez kufungua yako. Ukiwa na upungufu wa ukwasi huruhusiw ku-operate!
Bottom line: kuna uhutaj wa banking services kwny jamii ztu, thereof: huo uhitaji unakua ni fursa kwa karne hii na zjazo. So u cant fight its presence. Join it
 
Banking ni biashara. Bila mtaj huwez kufungua yako. Ukiwa na upungufu wa ukwasi huruhusiw ku-operate!
Bottom line: kuna uhutaj wa banking services kwny jamii ztu, thereof: huo uhitaji unakua ni fursa kwa karne hii na zjazo. So u cant fight its presence. Join it
Uko sawa,kutokana na kuyumba kwa uchumi kuna baadhi ya bank ziko kwenye mchakato wa kufilisika na wateja wao waliwekeza fedha huko,mwisho wa siku wale wateja wanashindwa kupata fedha zao kwa wakati.mfano inatokea unataka utoe M.10,wanakuambia utoe M.5;Kwahali hiyo fedha haitakiwi kukaa bank inatakiwa kupita tu iende kuzalisha;ingawa itaathiri malengo ya bank.Ndio maana bank zinapambana kushawishi wateja kwa kigezo cha riba kwa wale watakaoweka fedha bank kwa muda mrefu bila kuzitumia
 
Mimi nimedeposit milion 50 CRDB kwa mkataba wa miaka mitatu kila mwezi napewa 500,000/= na baada ya miaka mitatu narudishwa hamsini yangu au ni-renew mkataba
Doo angalia mzee baba usijekuwa unadroo hela zako mwenyewe
 
Uko sawa,kutokana na kuyumba kwa uchumi kuna baadhi ya bank ziko kwenye mchakato wa kufilisika na wateja wao waliwekeza fedha huko,mwisho wa siku wale wateja wanashindwa kupata fedha zao kwa wakati.mfano inatokea unataka utoe M.10,wanakuambia utoe M.5;Kwahali hiyo fedha haitakiwi kukaa bank inatakiwa kupita tu iende kuzalisha;ingawa itaathiri malengo ya bank.Ndio maana bank zinapambana kushawishi wateja kwa kigezo cha riba kwa wale watakaoweka fedha bank kwa muda mrefu bila kuzitumia
True bro
 
Back
Top Bottom