DOKEZO Achana na kunguni, UDOM ina vyoo vichafu sijawahi kuona

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
ACHA UJINGA
Sipingi ulichokizungumza
Ila umekosa busara kwenye uwasilishaji wa hoja yako

1.Ulikuwepo UDOM kwa miaka kadhaa,ulifanya nini kuboresha hilo??
2.Mbona umetumia lugha ngumu Sana, ni kweli hali iko hivyo au umeamua kuichafua serikali?? Kwa nini nisiamini kuwa unahoja uliyonayo nje ya hoja uliyoiwasilisha??
3. Kama mtanzania mzalendo unatambua madhala ya hiyo post ndani na nje ya nchi??
4.Hivi Kama maji yanapatikana mita kadhaa toka jengo la hostel ni chanzo Cha uchafu vyooni kweli? Nilisoma UDSM nilikuwa pale mabibo hostel block C second floor. Bafuni hakukuwahi kuwa na maji. Maji tulichota kwenye matank yaliyopo nje ya mabweni lakini tulizingatia usafi.

Kuwa Muungwana bro, Hapo hujengi bali unabomoa.



Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
That is your take.My take na mimi ni hii:
Hakuna maji tiririka kwenye mabomba mabwenini(hasa floor za juu)
Ili uweze kujisaidia basi kuna mchakato mrefu kidogo(kujisaidia sio raha/action ya ku relax tena!).Itakubidi uwe na ndoo,uende kisimani kuchota maji(nadhani kisima kipo ground huko),urudi toilet,then uendelee.Hapo umebanwa na haja ila ufanye hayo kwanza,halafu unakimbizana na muda wa vipindi!!!
Watetezi wa youdomu(sijui ndio wenyewe)wanakwambia maji kutokuwepo sio hoja ya msingi,hoja ni usafi wa mmoja mmoja,usafi ambao msingi wake(maji) haujapewa kipaumbele.
Udom/vyuo ni majumba ya kisasa na yanaishi watu wengi.Sharti kuwe na miundombinu wezeshi ili mazingira ya majengo yakidhi matarajio.
Watanzania(wanafunzi) tumetoka vijijini,tuna maisha yetu huko na ustaarabu wa vyoo ni tofauti kati ya jamii moja na nyingine.Ukiwaleta chuoni usiwape hayo maisha ya mjengoni,wataishi kama kule vijijini kwao.Pengine kwa hali hiyo hata wapo wengi hujisaidia humo kwenye pori lenu.
Hoja ingine: Vyuo vingine visafi na mifano imetolewa.Vyuo hivyo watanzania wanaotumia ni hawahawa ila suala la usafi limeratibiwa vizuri na chuo hudika,usafi unafuatiliwa,na wanafunzi wameona na wanafurahia na kutii,pia maji yapo 24/7 au jirani ya hapo.
Watetezi wa yudomu wanajinadibu na uwepo wa maji vyoo vya madarasani,lakini mbona hata huko madarasani vyoo vichafu mno!!Anyway,nadhani yudomu inapaswa kujisifu kwa uwepo wa maji mabwenini na darasani. Asante
 
Usiisingizie serikali maana vyuo vingine vya serikali ni visafi hakuna shida.Usijifiche katika hilo neno vyuo vingine vya vserikali visafi Tatizo ni hapo so ni hapo 😂
 
Kunguni wapo ili kukukumbusha kuwa hapo sio kwako, unasoma unaondoka. Pia upate akili ya kwenda kupannga mtaani ujifunze maisha. Dawa ya kunguni super inaitwa TwigaForce ni balaa hiyo.

Chooni mtu akiingia anatakiwa akimaliza kazi amwage maji yaani asafishe, sasa hapo wanafunzi watakuwa na kosa lakutozingatia usafi. LABDA KAMA MAJI NI TATIZO HAPO CHUONI HALI HIYO HAIEPUKIKI.
 
Haya
Mmeshalalamika na maji hayajawekwa,semester nzima maji yanatoka siku moja chooni.

Hapo mpuuzi ni nani?
Mimi ninayechota maji kisimani na kwenda nayo chooni?
Ama mpuuzi ni wewe unayetua zigo la mavi juu ya mavi mengine kisa maji hawajawaletea?
 
Tatizo la kwanza ni maji..
Na tatizo la pili ni wanafunzi.

UDOM hakuna maji,
Na hata kisimani kwenyewe ,Kuna muda maji yanakua chini sana hadi kuvuta na ndoo ni shida,,inakulazimu uzamishe kichwa chote mule ndani kisimani.


Kuna muda maji yanatoka bomba la nje la nyumba ya Warden.
Sasa pale mtu atatakiwa kusomba maji ya kutosha kwenye madiaba na madumu ili kuweza kusurvive.
 
Kwahiyo kama maji hakuna
Na mmeshalalamika na hayajaletwa,
Utakaa bila kuoga ili kukomesha uongozi ?
Utaenda chooni kushusha mzigo juu ya mzigo mwingine ili kuwakomesha viongozi?
Hapo unakomesha viongozi ama unajikomesha mwenyewe?
 
Tatizo la kwanza ni maji..
Na tatizo la pili ni wanafunzi.
mbn km umegeuza mkuu. hilo la pili ndo inabidi liwe la kwanza na ilo la kwanza liwe la pili.

madogo wapuuz sana. hawa kwa mwendo huu kuna siku watataka wawe wanapanua midomo tu walishwe kwa kisingizio wamekuja kusoma ivo vitu vingine haviwahusu
 
mbn km umegeuza mkuu. hilo la pili ndo inabidi liwe la kwanza na ilo la kwanza liwe la pili.

madogo wapuuz sana. hawa kwa mwendo huu kuna siku watataka wawe wanapanua midomo tu walishwe kwa kisingizio wamekuja kusoma ivo vitu vingine haviwahusu
Sijageuza Mkuu.
Nimeshangaa mdau anasema eti hawakwenda kusombelea maji.
Ina maana watakaa bila kuoga kisa kusoma?

Siwatetei viongozi kwa kushindwa kuleta maji vyooni kwa sababu ni upuuzi ,Mimi hadi naondoka pale,maji yalikuwa hakuna na tumesombelea maji visimani semester zote..na viongozi wapo,udoso wapo..kama maji yanatoka kwa warden ,,yanashindwaje kutoka vyooni hostel?


Lakini pia siwatetei wanafunzi.

Kuna muda semester nzima,maji yanatoka mara moja tu vyooni...
Wewe kama mwanafunzi ,tena wa chuo kikuu,utaendelea kushusha mavi juu ya mavi ya mwenzio semester zote 10 eti kwa sababu maji hakuna!
Haiingii akilini.
Watu hawana kinyaa..ni uchafu wa hali ya juu..
Lazima ukubali tu kuingia gharama kubeba maji,kwanza ya kusafisha kinyesi na choo ili uweze kutumia,,na maji mengine ya kusafisha choo na kujisafisha mara baada ya kutumia.
Ukitita juu ya mavi ya mwenzio na kuacha,unaweza kuwa unauokomoa uongozi,lakini pia unajikomoa mwenyewe.
 
Hicho chuo ni kipya intake ya kwanza ni 2008 lakin leo kinazidiwa na Sua chuo cha mwaka 1984 vyoo visafi mpaka unafua nguo
Kama unaweza kufua na nguo chooni ina maana kuna maji.

Hata UDOM maji yakitoka hukuti choo kichafu,,na nguo huwa zinafuliwa chooni.

Yaani maji yakitoka tu hata wiki moja...hukuti uchafu chooni.
 
Ukweli UDOM panatisha kwa uchafu, unakuta pedi, magunzi yamsokomezwa kwenye "sink" la choo. Uongozi ufanye kampeni mahsusi ya usafi. Ni heri kuua vipindi Fulani, wanafunzi waone umuhimu wa usafi. Unaweznkipata is janga la magonjwa
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Haya
Mmeshalalamika na maji hayajawekwa,semester nzima maji yanatoka siku moja chooni.

Hapo mpuuzi ni nani?
Mimi ninayechota maji kisimani na kwenda nayo chooni?
Ama mpuuzi ni wewe unayetua zigo la mavi juu ya mavi mengine kisa maji hawajawaletea?
Kujibu swali lako....ni yule ambaye atapoteza ajira yake hivi karibuni,kwa ishu hii
 
Km umesharudi USA njoo nikushike mkono nikupeleke ukashuhudie utofauti,

Sehemu ya umma hadi unipeleke mwenyewe? Wewe sema maeneno gani ya umma yana choo kisafi bongo nakuhakikishia hamna hata moja. Kuanzia Ikulu, bunge nk kote kuna vyoo vichafu.
 
Babuuu acha kutetea uchafu. Choo kikisafishwa huku watumiaji ni wachafu ni kazi bure. Watz wachafu chooni.
 
Kama unaweza kufua na nguo chooni ina maana kuna maji.

Hata UDOM maji yakitoka hukuti choo kichafu,,na nguo huwa zinafuliwa chooni.

Yaani maji yakitoka tu hata wiki moja...hukuti uchafu chooni.
Ndio muwaambie UONGOZI wa Chuo wavute maji Chooni, kwani hawana akili au Chuo kinaongozwa na Mazuzu?

Namaanisha wavute maji ya kwenye visima sio ya Dawasco, si kuna visima vya maji wavute hayo maji yatumike vyooni

Mahafari yanafanyika kila Mwaka Ina maana anapokuja mgeni rasmi kero hii haisemwi wanafunzi na uongozi wa Chuo wameridhika tu?

Kuna Serekali ya wanafunzi Rais wa wanafunzi yupo yupo tu anavuta mshahara wake anapita kushoto hawasemei kwa UONGOZI wa Chuo kua wanafunzi wenzake wana vyoo vichafu wanaishi mazingira magumu?
 
Wapo wadada wa usafi wanasafisha kila siku asubuhi kwa sabuni na dawa za kuondoa harufu. Tatizo ni wanafunzi ndo wachafu mtu anaweza kukata gogo bafuni na kuacha vyoo. Kuna siku umeme ulikatika mtu akakata gogo kwenye sehemu ya kunawia mikono. Uchafu wa vyoo unasababishwa na wanafunzi wenyewe sio chuo wala shida ya maji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…