Acheni Ushamba, Hakuna gari za kike wala za kiume

Acheni Ushamba, Hakuna gari za kike wala za kiume

Siyo hivo mkuu we chukulia mfano unakutana na kigari kama ki-nissan duet ama ki-vitz alafu ndani yake anatoka mtu kama JB ama Le Mutuz yani haiji kabisa yani...

Kuna jamaa mmoja ni bonge la mtu halafu jamaa kaenda hewani mbaya halafu mchizi ni mweupe ana ki vitz seat za nyuma kazichomoa zote mchizi akichomoka ndani ya hcho ki vitz unaweza ukacheka had ukafa
 
wiseboy uko sahihi lakini kwa rangi hapana, it looks weird kwa mwanaume kuendesha gari yenye rangi ya pink kama usafiri binafsi

kaka hii rangi ya pink kwa kweli ukienda nchi za watu ukavaa pink utatizamwa, mpaka unakuwa na wasiwasi, kumbe rangi ina maana yake na hasa kwa mwanaume ukivaa ile, maana yake kwa kweli nilivyoambiwa nililiacha huko sijavaa tena nguo za rangi ya pink mpaka leo
 
Ujuha wao tu...
Tutasikia na mitaa ya kike na ya kiume, nyumba za kike na za kiume, mashamba ya kike na ya kiume, halafu tutahamia kwenye noti/sarafu za kike na za kiume.

wazaramo wana msemo unasema kusoma hujui hata picha huoni, kwani magauni ukinunua yanakuwa yameandikwa special for women, hakuna, lakini automatically mnavaa nyie tu, sasa na vigari vidogo ni automatically vinaeleweka ni vya kike,
 
Kwa muda mrefu sasa nimekuwa naona mada humu JF zikiwa zinaponda magari,kwamba magari kama Toyota Passo,Vitz,IST,Starlet,na n.k ni magari ya kike.

Naomba wote wanaoamini kuwa kuna magari ya kike watoe ushahidi,ni wapi ambako chombo cha moto kimeandikwa kuwa:

A Vehicle Special for female au for male?

Acheni Ushamba nyie watanzania ambao hamjui lolote ktk Dunia hii yenye mambo mengi na mazito.

Tanzania isiyotengeneza hata sindano eti wananchi wake wanadharau magari yanayotengenezwa nje na kuya Classify kuwa hili ni la kike na lile ni la kiume,huu ni ujuha wa hali ya juu.

Watanzania ambao hata kula yao ni shida kwa siku eti nao wanabagua magari,kwa lipi?

Ukienda,Japan,US,UK,Germany,Sweden na popote duniani ambako wanatengeneza magari,hawawezi kukuambia kuwa hili ni gari la kile na lile ni la kiume.

Siku zote maskini ni mtu anayejiona ni bora kuliko wote japokuwa hana lolote,Sasa wewe umehangaika ukapata vipesa vyako unanunua gari anakuja mjinga anakuambia ni la kike,wapi imeandikwa kuwa ni la kike,Ujinga uliokithiri.
Khaa! Vipi kiongozi, washakuvuruga nini? naona povu jingi sana
 
Tatizo la mtanzania akipata hela za wizi anajisikia ni wa maana sana. Nime own cars of different models for over 20 years now. Sasa nimerudi kwenye vitz new model na yale mengine I am happy.

Ukivimbiwa na hela za wiki usitukane wengine. Kila mbuzi anakula kulingana na urefu wa kamba yake.
 
Kwa muda mrefu sasa nimekuwa naona mada humu JF zikiwa zinaponda magari,kwamba magari kama Toyota Passo,Vitz,IST,Starlet,na n.k ni magari ya kike.

Naomba wote wanaoamini kuwa kuna magari ya kike watoe ushahidi,ni wapi ambako chombo cha moto kimeandikwa kuwa:

A Vehicle Special for female au for male?

Acheni Ushamba nyie watanzania ambao hamjui lolote ktk Dunia hii yenye mambo mengi na mazito.

Tanzania isiyotengeneza hata sindano eti wananchi wake wanadharau magari yanayotengenezwa nje na kuya Classify kuwa hili ni la kike na lile ni la kiume,huu ni ujuha wa hali ya juu.

Watanzania ambao hata kula yao ni shida kwa siku eti nao wanabagua magari,kwa lipi?

Ukienda,Japan,US,UK,Germany,Sweden na popote duniani ambako wanatengeneza magari,hawawezi kukuambia kuwa hili ni gari la kile na lile ni la kiume.

Siku zote maskini ni mtu anayejiona ni bora kuliko wote japokuwa hana lolote,Sasa wewe umehangaika ukapata vipesa vyako unanunua gari anakuja mjinga anakuambia ni la kike,wapi imeandikwa kuwa ni la kike,Ujinga uliokithiri.
Kuna magari yanayowapendeza wanawake
kuna magari mwanamke akiendesha huondoa mvuto wake
Kuna magari ''sports car''..ambayo hayana jinsia ila kwa mwanaume kuendesha ukiwa umevaa suti umechemka.
kuna magari yanapendeza kwa familia
kuna magari ya mabachela au wachumba yana siti mbili tu.
kuna magari ya mashindano(michezo)..langalanga.Haya ni ya kiume .
Kuna magari ya kulimia -Trekta-Haya ni ya kiume ni hatari kwa wanawake.
kuna magari ya viongozi -mara nyingi huwa salon kubwa au limo
kuna magari ya safari bus
kuna magari ya mizigo -haya ni ya kiume(kwa mwanamke ni sawa ila si kusudi lake ni maisha )
kuna magari ya kutembelea nje ya bara bara off road (4x4)..hapa kwetu utayaona kwa wabunge.
kuna magari kwa ajili ya watoto
kuna magari ya wazee
kuna magari ya vijana mengi huwa convertible


 
miafrika ndivyo mlivyo-nyani ngabu..mnaacha kujadili mambo ya maana ya maendeleo ya bongo na majanga huko na jinsi ya kuliondoa madarakani hilo li chama mnajadili vitu vya kijinga kabisa ambavyo havisaidii kabisa maisha yenu!!
miafrika ndivyo mlivyo!!! NN
 
Kiuhalisia hakuna gari ya kike wala ya kiume...lakini kimuonekano inaleta heshima kwa mwanaume kutulia ndani ya Land Cruiser au Range Rover kuliko mwanaume wa miraba minne kujificha ndani ya vitz au spacio....ambapo kimuonekano zinawapendeza sana wakiendesha wadada...

Ndio maana watu wamekuwa wezi na mafisadi kupindukia... katika hali ya kawaida ni watz wangapi wana afford hizo gari? Mwengine anaminyana ananunua, shughuli wese na maintanance.. mawazo!! Hana raha
I know some guy whi bought grand vitara of over 40 mil tshs.. shughuli mafuta!! matokeo yake kalipaki anasubirie aende nalo harusini na mizunguko ya hatua kumi... this is nuts!!
All this? For what?? Ili uitwe kidume.. nonsense!!
 
Toyota Rush za Kike hata matangazo yake ya kike kike wanatageti wanawake huko sokoni
 
Ulimbukeni tu, maskini akipata matako hulia mbwata.. wazazi wenu vijijini hata matoroli hawana halafu leo hii unajifanya unayajua magari daah wabongo bana
 
Ila inataka roho ngumu mtoto wa kiume umetuna mwenyewe kwenye ka-vitz halafu umeuweka muziki mkubwa na vioo umeshusha tuusikie, japokuwa haijaandikwa lakini...............................
 
Ha haaa, Ni bora utembee kwa mguu kuliko kuendesha kigari cha kidem. Itakujengea heshima zaidi... That is the fact!
 
313_700x.jpg


George Clooney na kigari chake huyooooo
 
aah mkuu... Na hii imekaje surual ya kike., viatu vya kike...Saa ya kike...
 
Back
Top Bottom