ACP Kingai ni vyema na haki ikiwa utarejesha Tsh 260,000 fedha za mtuhumiwa wa ugaidi

ACP Kingai ni vyema na haki ikiwa utarejesha Tsh 260,000 fedha za mtuhumiwa wa ugaidi

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
20,654
Reaction score
35,887
Wakuu wote heshima sana.

Sote tumekuwa tukifuatilia kesi ya UGAIDI inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA na watuhumiwa wengine watatu.

Jana baada ya upande wa mashtaka kuwaondoa mashahidi wanne,mtuhumiwa wa Ugaidi mwanajeshi mstaafu au ukipenda mstaafishwa alipanda kizimbani kwa minajili ya kujitetea.

Akiongozwa na wakili wa utetezi alibainisha wazi wakati wa ukamataji ACP Kingai alichukua simu zake na fedha kiasi cha Tsh 260,000.

Muungwana ni vitendo ni vyema Kingai akamrejeshea mtuhumiwa fedha zake bila kujali Mtuhumiwa atashinda au atashindwa kesi yake.

Ikiwa ACP Kingai alishatafuna fedha za mtuhumiwa na hali ya uchumi imemkalia vibaya basi atoe namba zake za simu Sisi waTanzania ni watu wenye huruma hakika tutachanga kama tunavyochangia watu wengine bila kinyongo wala hiyana.

Naomba kuwasilisha.
 
... hiki chombo kina watendaji wachafu mno wengine very senior! Ukiona uchafu unaofanyika huko chini kwa matrafiki na watendaji wengine ni reflection ya kutokea juu.
Kutumia neno uchafu huwatendei haki- tumia neno wameoza na funza juu... wachafu sana ...wanamnyang'anya mtu sh 260,000, mtu aliyetoa maisha yake kwa ajili ya nchi na bado wanaenda kumshuhudia uongo. Hao ni funza tu ndani ya kidonda au parasite ndani ya tumbo.
 
Kutumia neno uchafu huwatendei haki- tumia neno wameoza na funza juu... wachafu sana ...wanamnyang'anya mtu sh 260,000, mtu aliyetoa maisha yake kwa ajili ya nchi na bado wanaenda kumshuhudia uongo. Hao ni funza tu ndani ya kidonda au parasite ndani ya tumbo.
Dah...wakilipa hizo....wakawalipe 400m walizompora Hamza 🤣🤣🤣🤭
 
Wakuu wote heshima sana.

Sote tumekuwa tukifuatilia kesi ya UGAIDI inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA na watuhumiwa wengine watatu.

Jana baada ya upande wa mashtaka kuwaondoa mashahidi wanne,mtuhumiwa wa Ugaidi mwanajeshi mstaafu au ukipenda mstaafishwa alipanda kizimbani kwa minajili ya kujitetea.

Akiongozwa na wakili wa utetezi alibainisha wazi wakati wa ukamataji ACP Kingai alichukua simu zake na fedha kiasi cha Tsh 260,000.

Muungwana ni vitendo ni vyema Kingai akamrejeshea mtuhumiwa fedha zake bila kujali Mtuhumiwa atashinda au atashindwa kesi yake.

Ikiwa ACP Kingai alishatafuna fedha za mtuhumiwa na hali ya uchumi imemkalia vibaya basi atoe namba zake za simu Sisi waTanzania ni watu wenye huruma hakika tutachanga kama tunavyochangia watu wengine bila kinyongo wala hiyana.

Naomba kuwasilisha.

Ila kibaka kurudisha loot hivi hivi? Si ni rahisi kwa huyu mwamba kusikia:

IMG_20210829_163746_049.jpg


bila damu masikioni?
 
Fedha walitumia yeye na Mahita toka Moshi na kuja kutanulia Dar es Salam
Kuna tofauti gani kati ya huyu na aliyejifanya kaimu afisa kodi Lengai Ole Sabaya?

Tulifika mahali pabaya.
 
Back
Top Bottom