Ni sahihi Mkuu, lakini pia tuseme Abdul Nondo alikuwa na bahati pia..Ccm wanapokea ruzuku 3.2 BILLION kila mwezi.
..huenda usafiri wa umma KIUSALAMABumemsaidia Abdul Nondo kuliko angetumia usafiri binafsi.
Haitoshi. Wanachotakiwa kufanya ni kuhakikisha kuna watu angalau wawili wa kumpokea na kumsalimia katika kila mji anaopita.Umeongea sahihi
Kama sikosei ACT Wazalendo wanapokea Ruzuku zaidi ya milioni 15 Kwa Mwezi
Nafikiri hawawezi kushindwa kuwanunulia ist ama Klugger Viongozi wao wa Kitaifa
Hata hivyo, zipo Benki zinakopesha vyama vyenye Usajili wa kudumu na vyenye kupata Ruzuku hata kama ni milioni 3 Kwa Mwezi
Nafikiri ni ubinafsi tu wa Viongozi wao
Nimetoa maoni yangu kwamba Kuna option ya kukopa pia.mil. 15 uendeshe ofisi na kununua gari unaumwa wewe
Ama wapewe usaidizi wa walinzi.Haitoshi. Wanachotakiwa kufanya ni kuhakikisha kuna watu angalau wawili wa kumpokea na kumsalimia katika kila mji anaopita.
Amandla...
Umefanya vizuri kuwasemea, najua baada ya hili andiko lako, Chama Chao kitafanyia kaziHawa kina Nondo ni vijana wetu
Wanawasemea Watanzania huku wao hakuna wa kuwasemea
Umefanya vizuri kuwasemea, najua baada ya hili andiko lako, Chama Chao kitafanyia kazi
Ni sahihi Mkuu, lakini pia tuseme Abdul Nondo alikuwa na bahati pia
Kwa maana hata Marehemu Mzee Ali Kibao alichukuliwa akiwa kwenye usafiri wa Umma pia.
Kwahiyo hawa jamaa walipofikia wanaweza kukuteka sehemu yeyote tu kasoro Kanisani ama msikitini tu
Hakuna huo uhusiano.
Asilimia tisini na Tisa ya waliotekwa hawakuwa na magari na hawakuwa katika vyombo vya Usafiri akiwemo huyo Nondo
Kwa nini useme kuna uhusiano wa utekaji na vyombo vya Usafiri?
Kwa mazingira hayo ni rahisi sana kutekwaKuna jamaa humu anaitwa Masawe Nani aliwahi kumponda Nondo baada ya kumkuta Pale makumbusho stendi akijifichaficha huku akiwepa mvua
Ni sahihi Mkuu..uko sahihi.
..angalau ukitekwa taarifa zitatoka kwa haraka kama kuna watu karibu.
Ni sahihi Mkuu
Taarifa za Kutekwa Ali Kibao zilitolewa mapema lakini hakuna kilichosaidia
Mwishowe ikaonekana Maiti yake tu
Mbaya zaidi alitekwa akiwa kwenye Basi lililojaa abiria 65 ama zaidi ambao hawakuweza hata kumsaidia masikini 🙌
Nyie pandeni hizo Boeing 737 acha sie tupande Saratoga na maelfu kwa maelfu ya walalahoi.Wewe unaona Sawa kiongozi ngazi ya taifa kuishi maisha hayo?
Ni sahihi Mkuu, ila kama una Vijana wako wakati huu wa Likizo wapeleke training ya Judo/Karate n.k..ukiwa eneo la watu wengi, halafu ukapiga kelele, na kufurukuta, watekaji lazima wataingia mawenge, na upo uwezekano wa kukuachia, au kuacha ushahidi utakaosaidia kupatikana kwako.
Ni sahihi Mkuu, ila kama una Vijana wako wakati huu wa Likizo wapeleke training ya Judo/Karate n.k
Kwa maana hizi Siasa za kutekana zilizokwisha asisiwa, haziwezi kuisha Leo ama kesho
Self defense ni muhimu sana
Hata kama utatekwa, lakini walau mtu mmoja ama wawili kati yao lazima uwatoboe macho
Umewasahau Chadema walitumia Corolla ya Chacha Wangwe vizuri?Kwema Wakuu!
Mwezi wa tano mwaka huu nilikuwa maeneo ya Kigoma. Kwa usafiri wa Basi kutoka Kigoma Mpaka DSM ni mbali Sana. Hayatapungua Masaa 20 ukiwa njiani unaugulia maumivu ya mgongo na kiuno.
Sasa kufuatia tukio la kutekwa kwa ndugu Abdul Nondo ambaye kwa mujibu wa maelezo yake anadai alikuwa anatoka Kigoma kwa Basi Mpaka DSM. Nimejiuliza maswali Mengi Sana
Hivi kijana mwenye cheo cha Mwenyekiti wa vijana bila Shaka ngazi ya taifa kwa chama cha ACT Wazelendo anakosaje usafiri binafsi Mpaka asafiri umbali mrefu kiasi hicho.
Tufanye hakuna Pesa ya gari vipi hata kupanda ndege. Ili kuokoa Muda na mateso ya umbali wa safari ya Kigoma Dsm?
Je ACT Wazalendo hawana pesa ya kurahisisha utumishi wa viongozi wao kama Abdul Nondo?
Je ACT Wazalendo hawajali viongozi wao hasa vijana? Kama hawamjali Mwenyekiti wa ngome ya vijana taifa watamjali kijana yupi?
Je Abdul Nondo ndiye Mbishi hataki kutumia Usafiri aliopewa na chama?
Ndugu Zitto Kabwe embu wafikirie hao vijana hapo ACT Wazalendo wasitie tie huruma.
Mtu ameshafikia nafasi ya juu ya uongozi kumaanisha tayari ni public Figure. Kukosa vitu Vidogo kama Usafiri binafsi ni kumnyanyasa kisaikolojia.
Kijana atatia Tia huruma
Kijana ataathirika kisaikolojia.
Kijana atakuwa anajificha ficha akipita kwenye msongamano WA watu.
Mpeni heshima anayostahili Huyo kijana.
Yaani masaa ishirini kwenye Basi. Loooh! Labda ingekuwa adventure
Kwako johnthebaptist