Adhabu mbadala wa viboko kwa watoto na wanafunzi wetu

Adhabu mbadala wa viboko kwa watoto na wanafunzi wetu

Raphael Thedomiri

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2019
Posts
442
Reaction score
729
Hoja ya kutowacharaza watoto na hata wanafunzi mashuleni sio mpya, lakini je ni upi unaweza kuwa mbadala?!

Nimejaribu kuwashirikisha njia mbadala niliyojifunza mahali fulani.

Adhabu ya viboko ni ya muda mrefu sana duniani, ni ya karne na karne. Ikikita mizizi zaidi katika bara letu la Afrika.

Malezi ya watoto bila kutumia adhabu ni jambo gumu ama lisilowezekana kabisa, hata sisi watu wazima mamlaka zimeweka mbele yetu adhabu mbalimbali tukoseapo kama faini au vifungo gerezani.

Tunaweza kuwaadhibu watoto wetu bila kutumia viboko.

Badala ya kuwatandika watoto viboko, tumia adhabu hizi mbili, ninakupa uhakika kuwa adhabu hizo zitajenga nidhamu kwa watoto/wanafunzi wako si ajabu hata kuliko kuwacharaza.

Wanapokosea wanyime vitu wanavyovipenda kwa mfano wanyime ruhusa ya kwenda nje kucheza na wenzao, ama wanyime kutazama tv, ama wanyime kucheza game n.k

Au walazimishe kufanya wasivyovipenda mfano kufanya kazi fulani za nyumbani labda kusafisha nyumba, ama kuosha vyombo n.k
 
Hoja ya kutowacharaza watoto na hata wanafunzi mashuleni sio mpya, lakini je ni upi unaweza kuwa mbadala?!

Nimejaribu kuwashirikisha njia mbadala niliyojifunza mahali fulani.

Adhabu ya viboko ni ya muda mrefu sana duniani, ni ya karne na karne. Ikikita mizizi zaidi katika bara letu la Afrika.

Malezi ya watoto bila kutumia adhabu ni jambo gumu ama lisilowezekana kabisa, hata sisi watu wazima mamlaka zimeweka mbele yetu adhabu mbalimbali tukoseapo kama faini au vifungo gerezani.

Tunaweza kuwaadhibu watoto wetu bila kutumia viboko.

Badala ya kuwatandika watoto viboko, tumia adhabu hizi mbili, ninakupa uhakika kuwa adhabu hizo zitajenga nidhamu kwa watoto/wanafunzi wako si ajabu hata kuliko kuwacharaza.

Wanapokosea wanyime vitu wanavyovipenda kwa mfano wanyime ruhusa ya kwenda nje kucheza na wenzao, ama wanyime kutazama tv, ama wanyime kucheza game n.k

Au walazimishe kufanya wasivyovipenda mfano kufanya kazi fulani za nyumbani labda kusafisha nyumba, ama kuosha vyombo n.k
Shida ni huo muda wa kumchunga asiende kucheza, ila viboko ukimchapa vinne vya maana unaendelea na kazi zako bila kumuazia mtoto
 
Adhabu za kisaikolojia ni mbaya kuliko za viboko.

Mwafrika anaenda kwa kiboko trust me, tofauti na hapo hatutafika kabisa
Lakini viboko ni kwa ajili ya wanyama kama mbuzi, ng'ombe kwamba waelekee njia hii ama ile.

Lakini binadamu sivyo, yeye kwa kuwa ana saikolojia basi itumike adhabu hiyo
 
Lakini viboko ni kwa ajili ya wanyama kama mbuzi, ng'ombe kwa waelekee njia hii ama ile.

Lakini binadamu sivyo, yeye kwa kuwa ana saikolojia basi itumike adhabu hiyo
Adhabu ya kiboko ni muhimu sana kwa mtoto,tuache kujidanganya na uzungu jamani,wengine sisi bila kunyoloshwa na kiboko tungelikuwa watu wa ajabu sana
 
Copral punishment ni ushenzi,ukatili, at its best, adhabu hii ndio inatupatia familia katili, definitely waliofundishwa na mwendazake pale sengerema sec school waliumia mno kwa viboko vyake na matokeo yake tunapata viongozi kama aliyemteua kuwa home affairs, tuachane na adhabu hii ya kishenzi
 
Copral punishment ni ushenzi,ukatili, at its best, adhabu hii ndio inatupatia familia katili, definitely waliofundishwa na mwendazake pale sengerema sec school waliumia mno kwa viboko vyake na matokeo yake tunapata viongozi kama aliyemteua kuwa home affairs, tuachane na adhabu hii ya kishenzi
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] umefikiria nini kuandika hivi

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] umefikiria nini kuandika hivi

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
Side effects za corporal punishment na nimetoa mfano hai, Nami ni mwalimu wa kusomea hadi nacho ualimu sikuwahi kutumia adhabu hii ya kikatili
 
Pili
Muda wa mwalimu kumtafutia adhabu ya kufanya kazi ngumu haupo.....kumbuka huyo mwanafunzi unayemtoa nje ya darasa ili kumpatia adhabu kwa vitendo na siyo viboko atakosa masomo ya siku hiyo au muda huo wa kufanya adhabu hiyo....
Kuokoa muda mwalimu inabidi amzabue mwanafunzi viboko vya ghafla ghafla ili akaendelee na masomo.....imeisha hiyo..!!
 
Pili
Muda wa mwalimu kumtafutia adhabu ya kufanya kazi ngumu haupo.....kumbuka huyo mwanafunzi unayemtoa nje ya darasa ili kumpatia adhabu kwa vitendo na siyo viboko atakosa masomo ya siku hiyo au muda huo wa kufanya adhabu hiyo....
Kuokoa muda mwalimu inabidi amzabue mwanafunzi viboko vya ghafla ghafla ili akaendelee na masomo.....imeisha hiyo..!!
No no mkuu huwezi kwa mwalimu aliyeiva kumtoa mwanafunzi nje ya kipindi kama adhabu, kuna adhabu kama za kumsimamisha in a naught corner, pia fanya utafiti mdogo why mwanafunzi ana react kwa tabia Ile,then mwalimu anajua the way forward
 
Mimi naona mmbadala wa viboko shuleni ni kukitilia maanani kipengele cha recomendation ya nidhamu kwenye leaving certificate ambacho kiwe tiketi ya kuendelea na masomo pamoja na kupata ajira.
Wazazi na wanafunzi waambiwe wazi kabisa kwamba nidhamu yao itakuwa judged huko mbeleni.
 
No no mkuu huwezi kwa mwalimu aliyeiva kumtoa mwanafunzi nje ya kipindi kama adhabu, kuna adhabu kama za kumsimamisha in a naught corner, pia fanya utafiti mdogo why mwanafunzi ana react kwa tabia Ile,then mwalimu anajua the way forward
Kumsimamisha mwanafunzi in a naughty what..??....Hebu kuwa serious eti.....hakuna namna eti wala huo muda wa mwalimu kumvuta pembeni mwanafunzi mmoja mmoja na ku-deal naye na hapo darasani ana wanafunzi zaidi ya 100 na pia ana vipindi madarasa mengine.....short and clear anamaliza mchezo kwa fimbo zake tatu tatu za nguvu...
 
Back
Top Bottom