Adhabu mbadala wa viboko kwa watoto na wanafunzi wetu

Adhabu mbadala wa viboko kwa watoto na wanafunzi wetu

Wao unaweza kuwapa kazi mbalimbali vile vile, kama kupanda miti, ama kuchimba shimo la taka kama ni kikundi cha wanafunzi waliokosea, ama kumwagilia maua
Vipi kama ukiwapa na hawatafanya wanafunzi ni wakorofi sana
 
Mkuu kama wewe sio mwalimu bora ungakaa kimya tu. Usifundishe watu kufanya kazi. Viboko hufundishwa chuoni na kuna namna ya kumwadhibu mwanafunzi hivo hizi ni taaluma za watu. Huwezi niambia upeleke kufagia wanafunzi umekuta hawajafanya jaribio labda robo ya darasa wakati kuna vipindi vinaendelea.
Mi siongei, nasubiri watoto zao warudi shule na viduku niwape bakora na kuwakata nywele na mkasi.

Sent from my Nokia C1 using JamiiForums mobile app
 
Akikujibu nitag mkuu
Huyu baba junior anazingua sana ndio wale ukienda kwake unakutana na mtoto wake (hua wanawaita junior) utakuta junior bara apokonye simu ya mgeni, mara amjambie, mara aje ammwagie juice, mara kaseme toka kwetu.. halafu baba junior na mama junior wamekaa na kumwambia "junior stop" huku wakijichekesha chekesha
 
Tatizo we hujawahi kuwa mwalimu,hebu kaombe shule ufundishe hata kwa siku tatu alf uwe unatumia hzo adhabu zako uone kama zitaleta mabadiliko.

M nakubaliana na mawazo yako lakin kwa Afrika ili tuweze kutumia hizo adhabu na ziweze kutoa matokeo chanya inahitaji mabadiliko makubwa katika uleaji wa watoto wetu,na hayo mabadiliko yaanzie kwa wazazi kwa kubadili mitazamo ambayo tunayo,na itachukua hata miaka 100 ili kufikia lengo
Next time mkuu kuwa little bit careful kujibia mada ambazo huwezi to verify kupata ukweli,mimi ni mwalimu wa kusomea pale Mkwawa CNE chini ya principal SA Mshana, ambaye alikuja kuhamishwa na kuletwa dude Mushi ambaye alianzisha corporal punishment kwa waalimu watarajiwa, we pushed him back na aliondoka mazingira ya pale makanyagio kwenye box,nimefundisha for only 6mths na sijawahi kutumia adhabu hii ya viboko (nilisomea PC&Ed)
 
Next time mkuu kuwa little bit careful kujibia mada ambazo huwezi to verify kupata ukweli,mimi ni mwalimu wa kusomea pale Mkwawa CNE chini ya principal SA Mshana, ambaye alikuja kuhamishwa na kuletwa dude Mushi ambaye alianzisha corporal punishment kwa waalimu watarajiwa, we pushed him back na aliondoka mazingira ya pale makanyagio kwenye box,nimefundisha for only 6mths na sijawahi kutumia adhabu hii ya viboko (nilisomea PC&Ed)
Ulikuwa level gani unafundisha?
Tofautisha umri wa wanafunzi na adhabu zao!
 
Adhabu ya viboko, kwa maoni yangu HAIFAI, HAIFAI, HAIFAI KABISA si kwa watoto majumbani wala kwa wanafunzi mashuleni kote HAIFAI. Adhabu ya viboko inavyoendelea sasa ni kielelezo cha jinsi wanadamu walivyo na tabia za kinyama na kishenzi, wenye udumavu wa akili na wasiotaka kubadilika. Kwa lugha nyepesi ni kwamba UMEKOSA MUDA WA KUTULIA NA KUFIKIRI kupata namna bora ya kumuadhibu mtoto/mwanafunzi na kilichobaki ni kumdhuru mwili wake. Umekosa maarifa mbadala. Unatumia nguvu kuliko akili yako, kama wewe unatumia nguvu zaidi kuliko akili, wewe una tofauti gani na mnyama?

Wengi wanaoamini katika adhabu ya viboko wanasumbuliwa na imani kwamba mtoto au mwanafunzi ndiye mwenye tatizo, lakini kiuhalisia mwenye tatizo ni mchapa viboko au anayeamini katika viboko na si mtoto au mwanafunzi. Ndiyo, iko hivi, kama wewe hivi sasa una tabia ya kuchapa au kupiga watoto wako au wanafunzi wako viboko, basi tambua mwenye tatizo hapo ni wewe na si watoto au wanafunzi.

Jifanyie uchunguzi mdogo wewe mwenyewe (Mchapaji viboko) hasa pale wakati unapoinua mkono au fimbo kuchapa (hapo hapo!) jiulize swali: Hali yangu ya utulivu wa akili hapa ikoje? (What is my state of mind?) Utagundua akili yako haiko sawa, unagundua una hasira, una msongo fulani wa mawazo, una haraka, au umechoka, na mara nyingi kuchoka kwako kumesababbishwa na kitu kingine, labda kazi, ugumu wa maisha, mahusiano na kero zingine mbalimbali.

Hivyo kumchapa mtoto/mwanafunzi ni njia ya mkato ya kumaliza tatizo au ukorofi wa mtoto, hii si fikra sahihi, lakini hivyo ndivyo wachapaji wanavyoamini.

Adhabu mbadala za kuwapa watoto na wanafunzi wetu ziko tele tu, lakini inabidi ujifunze polepole na lazima uwe na nia ya dhati ya kujifunza misingi yake ni nini. Kujifunza ni mchakato hivyo, lazima ujipe muda wa kutuliza akili yako, ili mtoto akienda kinyume ujiulize msingi wa yeye kwenda kinyume ni nini, na hata ukiamua kumpa adhabu unampa bila wewe kuwa na hasira, kumbuka lengo si kumuumiza au kumkomoa, lengo la adhabu ni kufunza, atambue kipi ni sahihi na kipi si sahihi, akue, na awe mtu mwema kadiri anavyokuwa, kwa njia ya kistaarabu na si kwa njia za kinyama.

Changamoto waliyonayo wazazi/walimu wachapaji wengi ni kwamba hawana muda wa kutuliza akili zao, wana hasira zinazosababishwa na mengi, wana msongo, wa haraka, hawana muda kutafakari athari za muda mrefu na pia hawana maarifa mbadala ya adhabu.

Tunawachapa watoto na wanafunzi kwa kuwa 'wamekosea' si ndio? kwani sisi watu wazima, wazazi na walimu hatukosei? Je nasi tuchapwe pia? Si tunakosea kila siku?

Dunia imebadilika sana, hivyo nasi tubadilike, tutumie akili zetu zaidi kuliko nguvu zetu.
 
Ulikuwa level gani unafundisha?
Tofautisha umri wa wanafunzi na adhabu zao!
Mkuu tuna haki kabisa ya to disagree, pia mimi sipendi kabisa death penalty, nikiwa President wa 24hrs nitaifuta hii adhabu within 2hrs,corporal punishment within 45mins za Urais wangu
 
Mimi ji muumini wa dini yangu ya mizimu, hizi dini zimeletwa na merikebu!
Ndio, wenzetu waliipokea kutoka kwa Yesu kristo baadae wakaieneza mpaka huku africa.!

I hope one day utaachana na mizimu utakuja nuruni.
 
Hoja ya kutowacharaza watoto na hata wanafunzi mashuleni sio mpya, lakini je ni upi unaweza kuwa mbadala?!

Nimejaribu kuwashirikisha njia mbadala niliyojifunza mahali fulani.

Adhabu ya viboko ni ya muda mrefu sana duniani, ni ya karne na karne. Ikikita mizizi zaidi katika bara letu la Afrika.

Malezi ya watoto bila kutumia adhabu ni jambo gumu ama lisilowezekana kabisa, hata sisi watu wazima mamlaka zimeweka mbele yetu adhabu mbalimbali tukoseapo kama faini au vifungo gerezani.

Tunaweza kuwaadhibu watoto wetu bila kutumia viboko.

Badala ya kuwatandika watoto viboko, tumia adhabu hizi mbili, ninakupa uhakika kuwa adhabu hizo zitajenga nidhamu kwa watoto/wanafunzi wako si ajabu hata kuliko kuwacharaza.

Wanapokosea wanyime vitu wanavyovipenda kwa mfano wanyime ruhusa ya kwenda nje kucheza na wenzao, ama wanyime kutazama tv, ama wanyime kucheza game n.k

Au walazimishe kufanya wasivyovipenda mfano kufanya kazi fulani za nyumbani labda kusafisha nyumba, ama kuosha vyombo n.k
Lifimbo Moja tu kiunoni atahisi kaangukiwa na mti hatarudia kosa tena
 
Adhabu za kisaikolojia ni mbaya kuliko za viboko.

Mwafrika anaenda kwa kiboko trust me, tofauti na hapo hatutafika kabisa
Ni kweli. Ni kwa sababu tumelelewa hivyo. Mwafrika hawezi kuamini uko serious bila kutumia adhabu. Ndiyo maana inatakiwa tujiepushe na adhabu ya viboko ili tusiendelee kujenga hii culture.
 
Vipi kama ukiwapa na hawatafanya wanafunzi ni wakorofi sana
Ukorofi unaanza tangu malezi ya utotoni kabisa. Ukishanza kumtisha na kumchapa lazima awe mkorofi mpaka atakapoona kiboko. Umewahi kutembelea nchi zilizoendelea? Nchi nyingi hawachapi watoto siyo nyumbani siyo shuleni na watoto wana tabia nzuri kuliko huku kwetu mara mia. Ni vizuri kutofautisha utundu na udadisi wanaokuwa nao watoto na ukorofi. Kimaumbile mtoto yoyote aliye normal ni lazima atakuwa mtundu na mdadisi. Waafrika wengi wakiona hili huona kama ni usumbufu hivyo huamua kutumia viboko kumtuliza mtoto. Hili ni kosa kubwa. Mwache mtoto ajifunze na hakikisha hapitilizi mipaka kwa kuwa karibu naye na kumwelekeza.
 
Next time mkuu kuwa little bit careful kujibia mada ambazo huwezi to verify kupata ukweli,mimi ni mwalimu wa kusomea pale Mkwawa CNE chini ya principal SA Mshana, ambaye alikuja kuhamishwa na kuletwa dude Mushi ambaye alianzisha corporal punishment kwa waalimu watarajiwa, we pushed him back na aliondoka mazingira ya pale makanyagio kwenye box,nimefundisha for only 6mths na sijawahi kutumia adhabu hii ya viboko (nilisomea PC&Ed)
Acha unafiki hautakusaidia! La sivyo uko private na wanafunzi wako ni below 45 darasani au 300 shule nzima. Vinginevyo unadanganya watu!
 
Adhabu ya viboko, kwa maoni yangu HAIFAI, HAIFAI, HAIFAI KABISA si kwa watoto majumbani wala kwa wanafunzi mashuleni kote HAIFAI. Adhabu ya viboko inavyoendelea sasa ni kielelezo cha jinsi wanadamu walivyo na tabia za kinyama na kishenzi, wenye udumavu wa akili na wasiotaka kubadilika. Kwa lugha nyepesi ni kwamba UMEKOSA MUDA WA KUTULIA NA KUFIKIRI kupata namna bora ya kumuadhibu mtoto/mwanafunzi na kilichobaki ni kumdhuru mwili wake. Umekosa maarifa mbadala. Unatumia nguvu kuliko akili yako, kama wewe unatumia nguvu zaidi kuliko akili, wewe una tofauti gani na mnyama?

Wengi wanaoamini katika adhabu ya viboko wanasumbuliwa na imani kwamba mtoto au mwanafunzi ndiye mwenye tatizo, lakini kiuhalisia mwenye tatizo ni mchapa viboko au anayeamini katika viboko na si mtoto au mwanafunzi. Ndiyo, iko hivi, kama wewe hivi sasa una tabia ya kuchapa au kupiga watoto wako au wanafunzi wako viboko, basi tambua mwenye tatizo hapo ni wewe na si watoto au wanafunzi.

Jifanyie uchunguzi mdogo wewe mwenyewe (Mchapaji viboko) hasa pale wakati unapoinua mkono au fimbo kuchapa (hapo hapo!) jiulize swali: Hali yangu ya utulivu wa akili hapa ikoje? (What is my state of mind?) Utagundua akili yako haiko sawa, unagundua una hasira, una msongo fulani wa mawazo, una haraka, au umechoka, na mara nyingi kuchoka kwako kumesababbishwa na kitu kingine, labda kazi, ugumu wa maisha, mahusiano na kero zingine mbalimbali.

Hivyo kumchapa mtoto/mwanafunzi ni njia ya mkato ya kumaliza tatizo au ukorofi wa mtoto, hii si fikra sahihi, lakini hivyo ndivyo wachapaji wanavyoamini.

Adhabu mbadala za kuwapa watoto na wanafunzi wetu ziko tele tu, lakini inabidi ujifunze polepole na lazima uwe na nia ya dhati ya kujifunza misingi yake ni nini. Kujifunza ni mchakato hivyo, lazima ujipe muda wa kutuliza akili yako, ili mtoto akienda kinyume ujiulize msingi wa yeye kwenda kinyume ni nini, na hata ukiamua kumpa adhabu unampa bila wewe kuwa na hasira, kumbuka lengo si kumuumiza au kumkomoa, lengo la adhabu ni kufunza, atambue kipi ni sahihi na kipi si sahihi, akue, na awe mtu mwema kadiri anavyokuwa, kwa njia ya kistaarabu na si kwa njia za kinyama.

Changamoto waliyonayo wazazi/walimu wachapaji wengi ni kwamba hawana muda wa kutuliza akili zao, wana hasira zinazosababishwa na mengi, wana msongo, wa haraka, hawana muda kutafakari athari za muda mrefu na pia hawana maarifa mbadala ya adhabu.

Tunawachapa watoto na wanafunzi kwa kuwa 'wamekosea' si ndio? kwani sisi watu wazima, wazazi na walimu hatukosei? Je nasi tuchapwe pia? Si tunakosea kila siku?

Dunia imebadilika sana, hivyo nasi tubadilike, tutumie akili zetu zaidi kuliko nguvu zetu.
Kwahiyo, Biblia inekosea kushauri kutumia fimbo kidogo kwa watoto!
 
No no mkuu huwezi kwa mwalimu aliyeiva kumtoa mwanafunzi nje ya kipindi kama adhabu, kuna adhabu kama za kumsimamisha in a naught corner, pia fanya utafiti mdogo why mwanafunzi ana react kwa tabia Ile,then mwalimu anajua the way forward
Kwa nature ya watoto wetu it needs lot of time and commitment kutumia adhabu mbadala. Kumbuka nature ya malezi wanayopitia kabla hawajafika shule. Kuna wengine adhabu mbadala wanazifurahia. Sasa mchakato wa kuanza kufikiria ni adhabu gani mbadala itafanya kazi kwa nani nk na rundo la wanafunzi kulinganisha na idadi ya walimu ni nani ako na huo muda na kwa motisha upi labda!!

Ndio maana viboko inaonekana ni adhabu ya chap kwa haraka kila mtu akaendelee na stress zake.
 
Kwa nature ya watoto wetu it needs lot of time and commitment kutumia adhabu mbadala. Kumbuka nature ya malezi wanayopitia kabla hawajafika shule. Kuna wengine adhabu mbadala wanazifurahia. Sasa mchakato wa kuanza kufikiria ni adhabu gani mbadala itafanya kazi kwa nani nk na rundo la wanafunzi kulinganisha na idadi ya walimu ni nani ako na huo muda na kwa motisha ipi labda!!

Ndio maana viboko inaonekana ni adhabu ya chap kwa haraka kila mtu akaendelee na stress zake.
Utawala wa ccm umetugeuza kuwa mazuzu kweli kweli, US 🇺🇸 wameacha muda mrefu sana kutumia adhabu hii na muda huu wapo kwenye count down kupeleka Rocket 🚀 mwezini, weather ipo byeee isipokua NASA lauch team stops loading hydrogen into Artemis Rocket, wataalamu wote hawa hakuna aliyechapwa hata kiboko kimoja, ngoja nisogeze mbeta ya ulanzi hapa lingusenguse
 
Kwa nature ya watoto wetu it needs lot of time and commitment kutumia adhabu mbadala. Kumbuka nature ya malezi wanayopitia kabla hawajafika shule. Kuna wengine adhabu mbadala wanazifurahia. Sasa mchakato wa kuanza kufikiria ni adhabu gani mbadala itafanya kazi kwa nani nk na rundo la wanafunzi kulinganisha na idadi ya walimu ni nani ako na huo muda na kwa motisha upi labda!!

Ndio maana viboko inaonekana ni adhabu ya chap kwa haraka kila mtu akaendelee na stress zake.
Kumbe tatizo ni wewe, you need to create time and commitment, kwanini hufanyi hivyo?, kumbe tatizo si watoto!
 
Back
Top Bottom