Hiyo Luka 4:1-13 hii hapa
4:1 Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
4:2 Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
4:3 Ndipo Ibilisi akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate."
4:4 Yesu akamjibu, "Imeandikwa: `Mtu haishi kwa mkate tu."`
4:5 Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
4:6 "Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
4:7 Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."
4:8 Yesu akamjibu, "Imeandikwa: `Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."`
4:9 Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
4:10 kwa maana imeandikwa: `Atawaamuru malaika wake wakulinde,`
4:11 na tena, `Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe."`
4:12 Lakini Yesu akamjibu, "Imeandikwa: `Usimjaribu Bwana Mungu wako."`
4:13 Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
HAYA MANENO YAKO, NI AYA IPI HAPO ???
1. Sababu ya Yesu kwenda jangwani ilikuwa ni kutafakari na kujiimarisha yeye binafsi katika siku 40 alizotumia kufunga baada kubatizwa na kutiwa mafuta.
2. Yesu alipokuwa jangwani ndipo alikutana moja kwa moja na Shetani mpinzani wa baba yake. Na huyo Shetani alitumia mbinu sawa na zile za bustani ya Edeni. Shetani Ibilisi alijaribu kumshawishi Yesu ili aonyesha ubinafsi, ajiinua, kumjaribu na kutomtegemea Mungu. Tofauti na Adamu, Yesu aliendelea kuwa muadilifu na, kwa mara nyingi Yesu alinukuu maandiko ambayo yalikuwa mapenzi ya Mungu. Na hiyo ilisababisha Shetani kushindwa kumshawishi na kuondoka zake, "mpaka wakati mwingine unaofaa."