Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

Hahaha Daaah physics ni balaa Kuna T.O mmoja hivi alimaliza 2006 alikuja Kutufundisha sisi tukiwa form 6 tukajiona Vilaza Wote.. vitabu vya Chand...Roger. vyote tuliona Tumemaliza na Hakuna Swali Gumu.. Jamaa Halafu alikuwa ana dharau balaa na Chuo alifukuzwa Kisa Dharau kwa Maprofesa kwahiyo akabak anapiga Tuition mtaani tu na Sifa Kibao na Kuwaona Watanzania wote hawana Akili ila Yeye peke yake

Ila Nakumbuka Siku ya Mtihani wa Physics Nilipiga msuli Usiku halafu kesho yake Pepa Asubuhi Na Nikasolve Maswali Kama matatu hivi ya Chand kwenye Pepa Yamekuja Vile vile Nikasema Nashukuru Mungu Ndalichako kaniona

Ila Yote tisa nitarudi Shule Zote ila Siyo Advance
kwakweli hata mimi nitarudi shule zote lkn sio advance ya PCB!
Biology na Chemistry zinatembea lkn Advanced physics hapana aiseee! Topic kama Magnetism, Adiabatic Expansion! Kwakweli A.physics ni nomaaaa.
Nakumbuka nilotoka jasho kwenye Practical baada ya kukuta pendulum la ajaab, unafunga uzi kwenye rula halafu bob inaning'inia kwa kutengeza umbo la pembe tatu! I wont forget
2b2d2de6dda6ca2dc8227dea3e98ca59.jpg
 
Mgote ndio mwalimu aliyefundisha vizur topic ya projectile...pamphlet lake lilikuwa na solving nondo hatari....ila mnyama adv PHYSICS syo wa mchezoo mchezo...nakumbuka kwny necta ya physics kuna jamaa katikat ya pepa alianza kuliaa ...invigilator anamuuliza vp..anasema pepa haliendii..kitu ilikuwa imekaza hatarii yaani balaah...ila yote hayo elimu ya kibongo ni ya kukariri sana na kufanyia mtihani baasi...tusitegemee kuzalisha wakina elon musk kamwe
 
Hahaha UP ilikuwa hatari na zile units zake za inch, yard, ile UP ya njano ile page zake ziko kama unga wa dona hahahaha, kuna kitu inaitwa ROTATIONAL DYNAMICS ilinitesa sana hii kitu asee
mimi topic ya electronics niliingia bila kusoma kabisa baada ya kuona inanisumbua. Noma sana Physics
 
Guys

Mnanikumbusha iyunga boys,dah acha tu,nadhan mm nilikuwa kilaza kuliko wote
Hahahahah shule yenyew O-level tulkuwa tunagonga Engineering Science badala ya Physics.....so ulikuwa ukichaguliwa Iyunga advance kama ulkotoka ulkuwa unabahatisha hakuna muujiza wa kutoboa.....ukigeuka kushoto unakutana na LE MUTUZ la Chemistry....Mr. SUDI.....***** mzee ana roho mbaya huyo.....kinyama.....

Umenkumbusha mbali sana kwa IYUNGA......
 
Concept za mgote ndo zilinifanya kuikatia tamaa mapema physics.
 
Physics noma sana aisee hasa kwa watu wa PCB maana maswali mengine unahitaji kuingiza hesabu za differentiation au intergration na bahati mbaya watu wa PCB sio wazuri sana wa hesabu hizo maana olevel hazifundishwi. Ulimwengu wa advanced Physics kwa watu wa PCB ni wa mateso makubwa. Namshukuru Mwenyezi MUNGU nilitoboa.
 
Hicho sio kitabu cha Tanzania.Hatukutumia ya hivyo ,pia ile OP ilikuwa toka miaka ya 80 ila labda wewe hukutumia na hakuna uliyemjua aliyekuwa nacho.
Ndio, ni vya India nadhani. Zamani vitabu vingi vya a'level physics hapa Tanzania vilikuwa ni vile vilivyotungwa na wazungu (England)
 
Hahaha Daaah physics ni balaa Kuna T.O mmoja hivi alimaliza 2006 alikuja Kutufundisha sisi tukiwa form 6 tukajiona Vilaza Wote.. vitabu vya Chand...Roger. vyote tuliona Tumemaliza na Hakuna Swali Gumu.. Jamaa Halafu alikuwa ana dharau balaa na Chuo alifukuzwa Kisa Dharau kwa Maprofesa kwahiyo akabak anapiga Tuition mtaani tu na Sifa Kibao na Kuwaona Watanzania wote hawana Akili ila Yeye peke yake

Ila Nakumbuka Siku ya Mtihani wa Physics Nilipiga msuli Usiku halafu kesho yake Pepa Asubuhi Na Nikasolve Maswali Kama matatu hivi ya Chand kwenye Pepa Yamekuja Vile vile Nikasema Nashukuru Mungu Ndalichako kaniona

Ila Yote tisa nitarudi Shule Zote ila Siyo Advance
huyo mwalimu ni kihombo na wewe umesoma feza boyz hahah dadeki mi ndo ba shwalehe
 
Sio Siri Wave na Heat ndo nilipokuwa napamudu..projectile ndo ilikuwa topic ngum sn..afu Swali Lina maks tatu, ila Stefans law haa murua kabisa...ni Kama pure math na probability....
 
Sitasahau necta 2005 vifaa vya umeme viliponigomea Hadi msimamiz kunionea huruma nichukue data kwa jirani niendelee na swali kumbe jirani nae kapata data za uongo
Vile vifaa ni vya kichina vingine ni feki kabisa.
Nafikiri hii ni moja sababu ya watu kufeli physics.
Tena hata vile vinavyotumika o'level vya practical ya electricity ni vya kichina vinaleta data za uongo.
Kufaulu pale unahitaji akili ya ziada (uwe kichwa kwelikweli)
 
Back
Top Bottom