Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

Hahaaa advance kazi yangu ilikua ni kukariri page za vitabu na maswali+majibu yake kwenye page husika...
Kwahio mtu akiniletea swali namtajia page alipolitoa halafu namtajia jibu kwa mbwembwe mwisho na swali linanishinda..
 
Hahaha Daaah physics ni balaa Kuna T.O mmoja hivi alimaliza 2006 alikuja Kutufundisha sisi tukiwa form 6 tukajiona Vilaza Wote.. vitabu vya Chand...Roger. vyote tuliona Tumemaliza na Hakuna Swali Gumu.. Jamaa Halafu alikuwa ana dharau balaa na Chuo alifukuzwa Kisa Dharau kwa Maprofesa kwahiyo akabak anapiga Tuition mtaani tu na Sifa Kibao na Kuwaona Watanzania wote hawana Akili ila Yeye peke yake

Ila Nakumbuka Siku ya Mtihani wa Physics Nilipiga msuli Usiku halafu kesho yake Pepa Asubuhi Na Nikasolve Maswali Kama matatu hivi ya Chand kwenye Pepa Yamekuja Vile vile Nikasema Nashukuru Mungu Ndalichako kaniona

Ila Yote tisa nitarudi Shule Zote ila Siyo Advance
T.O alikuwa mduwanzi sana, ukisoma kwa moudy physics utacheka kipindi anampiga madongo t.o
 
Hahaha Daaah physics ni balaa Kuna T.O mmoja hivi alimaliza 2006 alikuja Kutufundisha sisi tukiwa form 6 tukajiona Vilaza Wote.. vitabu vya Chand...Roger. vyote tuliona Tumemaliza na Hakuna Swali Gumu.. Jamaa Halafu alikuwa ana dharau balaa na Chuo alifukuzwa Kisa Dharau kwa Maprofesa kwahiyo akabak anapiga Tuition mtaani tu na Sifa Kibao na Kuwaona Watanzania wote hawana Akili ila Yeye peke yake

Ila Nakumbuka Siku ya Mtihani wa Physics Nilipiga msuli Usiku halafu kesho yake Pepa Asubuhi Na Nikasolve Maswali Kama matatu hivi ya Chand kwenye Pepa Yamekuja Vile vile Nikasema Nashukuru Mungu Ndalichako kaniona

Ila Yote tisa nitarudi Shule Zote ila Siyo Advance
Nampata huyo, bila shaka ni T.O from Tosa boys
 
Watu tunatofautiana kweli kweli.. Mie chemistry ndio ilinipa tabu..
Physics hasa form 5 ilikuwa kitonga kwangu kwa kiasi kikubwa namkumbuka madam aliyekuwa ananipigia pindi, nilianza nae na mkosi ila tukaishia kuwa marafiki wakubwa..

Kipindi cha likizo ya kumaliza form 4 watu walijichimbia mchikichini na tuition center kupiga mapindi.. Mie nilikuwa najilia zangu bata.. Sasa siku ya kwanza nareport school nakuta madam wa phyics anapiga pindi la measurements, nikaenda zangu kukaa kiti cha nyuma kabisa, kutupa jicho ubaoni naona mapicha picha tu, kidogo sijakaa vizur madam ananiita na kuniuliza swali, halaf njemba sijui kitu nikaona leo maseke, nikamwambia tu sijui kitu, wacha anichane we hujui kitu bado umechelewa kuripoti shule, na bado unakaa nyuma, kuanzia leo ukae mbele, darasa lote halina mbavu.
Kutokana mie katuni nikamwambia ticha usipate tabu nipe siku 3 tu ntakuwa safi ila mbele sikai sababu macho yangu hayaoni karibu maana hata yeye mwenyewe simuoni vizur kwa jinsi tulivyokaribu kicheko kikaongezeka.. Baadae alikuja kuwa swahiba wangu mzuri tu, kama ningekaza ningeruka pale..

Physics yoote ya 4m 5 naikumbuka mpaka leo hii
Nakumbuka nilikuwa mie na mwanangu jonii kutumia measurement tukajidai kitengeneza formula ya kwichi kwichi(kokojoa), tukasaka vitu muhimu katika kwichi kwichi kama vile friction force, heat, velocity n.k halafu hisia tukaweka costant(K)[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji85] [emoji85] [emoji85]
 
Mgote ndio mwalimu aliyefundisha vizur topic ya projectile...pamphlet lake lilikuwa na solving nondo hatari....ila mnyama adv PHYSICS syo wa mchezoo mchezo...nakumbuka kwny necta ya physics kuna jamaa katikat ya pepa alianza kuliaa ...invigilator anamuuliza vp..anasema pepa haliendii..kitu ilikuwa imekaza hatarii yaani balaah...ila yote hayo elimu ya kibongo ni ya kukariri sana na kufanyia mtihani baasi...tusitegemee kuzalisha wakina elon musk kamwe
Mgote alikuwa mass nondo, nilikuwa namuita mkompliketi maisha na mipamplets yake.. Ukiona dubwasha la projectile zigo hilo, kwa moudy ni kimtindo tu ila idea yake iko kwa kichwa mpaka kesho.
 
Mkuu umenikumbusha mbali sana, sisi kihombo alikuja kutupigia tuition shule,akakuta watu wanakomaa na vitini vya kina muddy,mgote nk acha aanze kutupondea, mara ooh madogo nyie mnaandaa buyu...akaanza kutuimiza kusolve atleast vitabu 8 vya physics sijui Roger muncaster,UP,nelkon edition zote,chand nk ***** watu tukaanza kuona maisha magumu ukishika tu roger maswali hayatembei...kudadadeki si akatunga test nilitembea na 5/100,jamaa kiukweli alitukimbiza ile mbaya...
Nb mwaka wetu aliyeongoza physics alikua na C ndo ujue hili dude si la mchezo
 
Hiyo Projectile motion ilinipa marks zote kwenye pure maths... alaf watu wa egm walikuwa wanaiogopa vibaya mi nikasema nakomaa nayo... kama mtoa mada nikawa nacalculate height, range, angle na kuderive formula tu na swali likaja humo humo!!

Ila wanafunzi wa Advanced Physics kuwen wakweli, ambacho huwa kinawafelisha hasa ni kipi?
 
Back
Top Bottom