Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

kuna wakati nilitamani kukimbia Physics adv ni balaa halafu mwisho wa siku watu mnakuja kusoma accounting, procurement sasa najiuliza mateso yote yale ya nini si bora ningesoma hata HGE? wanafunzi wengi hawapati ushauri kuhusu combination wanazosoma na options ambazo zipo vyuoni mimi nilikua mmoja wapo, ndio maana madogo wakiomba ushauri huku ni lazima nicoment,kama mwanafunzi hawezi hesabu asihangaike kusoma PCM,PCB PGM atajutia maana kuangukia pua si kitu cha ajabu
 
Nakumbuka kuna kipind mambo yalizid kuwa magumu maswal hayachomoki .... daaaah ikawa nikipata mda nitafuta sehemu najificha nalia weee nikimaliza narud zangu darasan au dom

Dah pole sana Finest, ila mwisho wa siku si ukamaliza tu vizuri licha ya magumu yote uliyopitia
 
Niliwahi msoviaga Mshkaj projectile ya mshare unarushwa juu na MTU aliyekaa juu ya gari ili kumrenga ndege anae pita juu....(NILIPOTOKA KWA COMMISSIONER).

Jamaa aligair kurud kwao ili likizo aje dar nae kupiga pindi kwa mudy-mchikidown haaah
 
Projectile INA multiconcept aiseee.....

Unaweza include newtons law of solid dymics,fluid dynsmics,energy,work and power,circular and SHM.

Haaaah that's craziest and mindful destroyer


P H Y S I C S
 
Hata Mimi sujui kwa nn projectile inapigwa pindi moja inaisha ila concepts kibao afu Mwl kizembe tu anawaambia attempt any question it won't stand upon your eyes
 
Hahaha Daaah physics ni balaa Kuna T.O mmoja hivi alimaliza 2006 alikuja Kutufundisha sisi tukiwa form 6 tukajiona Vilaza Wote.. vitabu vya Chand...Roger. vyote tuliona Tumemaliza na Hakuna Swali Gumu.. Jamaa Halafu alikuwa ana dharau balaa na Chuo alifukuzwa Kisa Dharau kwa Maprofesa kwahiyo akabak anapiga Tuition mtaani tu na Sifa Kibao na Kuwaona Watanzania wote hawana Akili ila Yeye peke yake

Ila Nakumbuka Siku ya Mtihani wa Physics Nilipiga msuli Usiku halafu kesho yake Pepa Asubuhi Na Nikasolve Maswali Kama matatu hivi ya Chand kwenye Pepa Yamekuja Vile vile Nikasema Nashukuru Mungu Ndalichako kaniona

Ila Yote tisa nitarudi Shule Zote ila Siyo Advance
Bila shaka unamzungumzia ELIAS KIHOMBO (2006)tosamaganga
 
nakumbuka siku ya kwanza nafika darasani nikakutana na vijana wamesoma vitu vya hatari huko watokako , sasa nikaenda kuomba msaada kwa jamaa mmoja ili anisidie swali (error and dimensions) kutoka kwenye notsi za mwalimu wetu wa physics alikuwa anaitwa NZOI , jamaa alinicheka saana akasema we dogo ushafeli tayari unashindwaje swali hili?, nikaona maisha yamekuwa magumu ghafla, japo nilifaulu ila yale maisha sitaki kuyakumbuka , ila advance physics iliifundisha kujiamini hahahah😀😀
Bila shaka wewe ni pugu boy. Msukuma yule error alikuwa anaitamka errrrrror. Kwenye practical anatoa mifano ya NECTA za miaka ya 60 an 70 hahaaaa. Kweli Advance ilinitesa kuliko kwingine kote nilikopitia.
 
Hahahahah shule yenyew O-level tulkuwa tunagonga Engineering Science badala ya Physics.....so ulikuwa ukichaguliwa Iyunga advance kama ulkotoka ulkuwa unabahatisha hakuna muujiza wa kutoboa.....ukigeuka kushoto unakutana na LE MUTUZ la Chemistry....Mr. SUDI.....***** mzee ana roho mbaya huyo.....kinyama.....

Umenkumbusha mbali sana kwa IYUNGA......
Hahahahaha Sudi namkumbuka vibaya mno yule mzee mwili mkuuubwa kisauti kidogo .
 
Sitasahau necta 2005 vifaa vya umeme viliponigomea Hadi msimamiz kunionea huruma nichukue data kwa jirani niendelee na swali kumbe jirani nae kapata data za uongo
Hahahahahah pumbavu[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Haha... Physics ya Alevel sitaki hata kuisikia
Ya OLevel simpo sana niliikung'utw kung'uta mtiti nilipofikq advance na shule yenyewe TAmbaza hahahahahqh kuna babu pale yupo na mjuni(Israel nkongo )

Wote wako shallow vibaya mno babu anakuja na Nelkon kuzugia tu nitakatoka kapa kabisa nashuruku Mungu nikapitia mlango mwingine
 
Back
Top Bottom