Afande Sele hafahamu kuwa miradi iliyotekelezwa na Rais Samia kipindi hiki ni mingi kuliko wakati mwingine wowote?

Afande Sele hafahamu kuwa miradi iliyotekelezwa na Rais Samia kipindi hiki ni mingi kuliko wakati mwingine wowote?

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Afande sele kawashangaza Sana mamilioni ya watanzania ambao wanaendelea kuhoji kuwa Ina maana Afande sele hajaona ndani ya mwaka mmoja wa Rais Samia madarakani alivyojenga na kuboresha secta ya Elimu hapa nchini? Watanzania wanahoji kuwa Afande sele amesahau Mara hii namna watanzania walivyokuwa wanahaha kulipa michango ya ujenzi wa vyumba vya madarasa Hadi wengine kukimbia Kaya zao?

Wanauliza je, hakuona mh Rais wetu mpendwa akitoa fedha kwa ajiri ya kwenda kujenga vyumba vya madarasa kila shule? hakuona miaka ya nyuma wengine wakienda muhula wa pili kuanza masomo yao kwa kuwa tu hakukuwa na madarasa ya kutosha? Je wangekuwaje sawa na waliolipoti mwezi wa kwanza?

Wanauliza Kwamba huyu msanii hajaona namna uamuzi wa serikali wakufuta Ada ya kidato cha tano na sita ilivyoweza kuwasaidia watoto wa wanyonge kupata Elimu bila shida? Wangapi walikuwa wanashindwa kuripoti shule kwa kukosa Ada? Je haoni Jambo hilo limeleta neema kwa familia masikini? Huyu msanii haoni kuwa hizo Ni faida za Tozo zetu?

Huyu msanii kwamba hajaona namna zahanati na vituo vya Afya vilivyosambazwa kila Kona ya nchi hii ndani ya muda mfupi wa Rais Samia? Kwamba hajaona wananchi walivyopunguziwa adha ya kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma za Afya? Haoni suala Hilo limesaidia hata wamama wajawazito kujifungulia hospitalini na hivyo kupunguza hatari ya kutokea kwa vifo vya mama na mtoto?

Huyu msanii haoni namna huduma za maji zilivyosogezwa Hadi vijijini na hivyo kupunguza Ile kero ya watu kuamka alfajiri kutafuta maji toka kilometa kadhaa? Anadhani pesa hizo zimetoka wapi? Au alitaka watanzania waendelee kuhenyeka kufuata maji umbali mrefu?

Huyu msanii hajaona juhudi za serikali kuinua maisha ya mkulima kwa uamuzi wake wa kutoa Ruzuku ya billion Mia moja hamsini? Haoni namna ambavyo kwa Sasa mbolea inapatikana kwa Bei nafuu ya elfu 70 kwa DAP ambayo msimu uliopita iliuzwa kwa laki na 40? Haoni Jambo Hilo litachochea uzalishaji kuongezeka msimu ujao! Haoni kuwa uchumi wa mkulima unakwenda kuinuka hasa ukizingatia Ni secta iliyo ajiri kundi kubwa la watanzania na ndio pumzi ya watanzania wengi

Hapana siyo kuwa haoni Bali kaamua tu kujipa upofu na kufanya upotoshaji kwa umma ambao hata hivyo umempuuza tu, watanzania hawamshangai maana bado wanakumbuka kuwa amewahi kuvua nguo jukwaani,kwa hiyo wanaona anatatizo linalohitaji ushauri wa kisaokolojia

Watanzania wanaendelea kumuunga mkono mh Rais wetu mpendwa, maana wameona juhudi zake katika kuijenga nchi yetu na maendeleo yaliyopatikana na namna yalivyogusa maisha ya watanzania kwa kupunguza kero zilizokuwa kidonda ndugu kwao

Watanzania wanasema Tanzania itajengwa na sisi watanzania, hatuwezi tukakaa tu ili wenzetu walipe Kodi na Tozo huko kwao halafu sisi tuletewa huku, Hatutaweza Kuendelea na aibu hiyo, Sasa Tumeamua kuijenga Tanzania yetu na mh Rais wetu mpendwa Samia ameongoza njia hiyo na watanzania tunamuunga mkono

Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia watanzania walipo
 
Siku CCM ikisoma alama za nyakati ikapinga tozo na kuiagiza serekali ifute tozo na serekali ikakubali kufuta tozo uje hadharani kuipinga serekali na usithubutu kuisifu serekali ya mama kuwa ni sikivu na bla bla zingine. Nitakutukana nipigwe ban.
 
Awamu ya Tano huduma za jamii (Afya, Elimu, Maji, Nishati) zilikuwa zinaboreshwa bila tozo. Isitoshe uboreshaji unaoendelea ni kwa fedha za UVIKO na mikopo
Tunataka tujitegemee, hatutaki tukope kwa kila kitu hata vilivyo ndani ya uwezo wetu, lazima Sasa tuanze kujibana ili kuijenga nchi yetu kupitia vipato vyetu, Hatutaki mzigo wa madeni uwe mkubwa kuliko mabega yetu
 
Siku ccm ikisoma alama za nyakati ikapinga tozo na kuiagiza serekali ifute tozo na serekali ikakubali kufuta tozo uje hadharani kuipinga serekali na usithubutu kuisifu serekali ya mama kuwa ni sikivu na bla bla zingine. Nitakutukana nipigwe ban
Panapohitaji maboresho patarekebishwa lakini wajibu wa kuijenga nchi yetu utabakia mikononi mwetu Watanzania.
 
Ndugu zangu Afande sele kawashangaza Sana mamilioni ya watanzania ambao wanaendelea kuhoji
Hao watanzania mamilioni wewe umewasiliana nao wapi? Kama ni utafiti, huo utafiti umeufanyia wapi? Ebu tuletee hadidu za rejea! Watanzania, ulituhoji lini tukakwambia hayo ndiyo maoni yetu?
Hivi mtaacha lini huu ujinga wa kufanya mawazo yenu binafsi kuwa ni mawazo ya watanzania?
Uchawa mwingine wa kijinga sana.
 
Nadhan na wewe ni mmojawapo ya waleeee walamba asali
Mtu alishindwa kuchangia ujenzi akakimbia, Ila sasa tozo zinamuua kabisa!
Poor you 🤪
Ni tozo hizo zilizopelekea kusogezwa kwa huduma karibu ya mwananchi, watanzania wameridhishwa na namna miradi ilivyotekelezwa kutokana na tozo, kila mtu anajivunia mafanikio tuliyoyapata kwa kuwa tunajuwa Ni nguvu zetu
 
Hao watanzania mamilioni wewe umewasiliana nao wapi? Kama ni utafiti, huo utafiti umeufanyia wapi? Ebu tuletee hadidu za rejea! Watanzania, ulituhoji lini tukakwambia hayo ndiyo maoni yetu?
Hivi mtaacha lini huu ujinga wa kufanya mawazo yenu binafsi kuwa ni mawazo ya watanzania?
Uchawa mwingine wa kijinga sana.
Fuatilia na kasome hata utafiti wa Twaweza
 
Mkopo wa Benki ya dunia mlisema unaenda kuondoa kabisa changamoto ya madarasa tanzania, sasa tozo inaenda kujenga madarasa yepi tena mkuu?
Ujenzi wa madarasa hauji kuisha maana hata sisi tunaongezeka kiidadi mwaka Hadi mwaka, hivyo Mahitaji lazima nayo yaongezeke tu
 
WA-IMG-20220909-3d247dae.jpg
 
Back
Top Bottom