Afghanistan: Zaidi ya watu 600 wamefanikiwa kupanda ndege ya Jeshi la Marekani

Afghanistan: Zaidi ya watu 600 wamefanikiwa kupanda ndege ya Jeshi la Marekani

Kumbe hata atcl tunaweza shika bomba, hii level seat inatupunguzia mapato
 
Baada ya kushuhudia Waafghanistan wakijaribu kudandia ndege ya Jeshi la Marekani katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Khamid Karzai mjini Kabul jana, Wizara ya Ulinzi ya Marekani imetoa picha inayoonesha watu 640 wakiwa ndani ya ndege yake ya kijeshi.

Idadi hiyo ya watu inatajwa kuwa zaidi ya mara tano ya uwezo wa ndege hiyo kubeba abiria na moja ya idadi kubwa zaidi kuwahi kubebwa katika ndege hiyo aina ya Boeing C-17 Globemaster III. Waliofanikiwa kuingia ndani ya ndege hiyo walitumia mlango ambao haukufungwa vizuri wakati ndege hiyo ikiwa katika uwanja wa ndege mjini Kabul.

Wizara ya Ulinzi ya Marekani imeripoti kuwa haikuwa na mpango wa kuwabeba watu hao, lakini ililazimika kutokana na vurugu zilizotokea katika uwanja wa ndege jana. Inaripotiwa kuwa watu wawili wamefariki baada ya kuanguka kutoka kwenye ndege hiyo.

Kujaa kwa watu katika Uwanja huo wa Ndege kulitokana na taarifa za uzushi kusambaa awali Mjini Kabul kuwa Jeshi la Marekani linatoa usafiri wa bure kuwapeleka wananchi wa Afghanistan kwenda Marekani na Kanada, ndipo mamia ya watu walipovamia uwanja huo wakijaribu kupata usafiri huo wa bure na kuyaokoa maisha yao kutoka kwa Wataliban.

Waliofanikiwa kupanda ndege hiyo - wakiwamo wanawake na watoto wachanga - wamefanikiwa kutua salama nchini Qatar.

Wapiganaji wa Taliban wamefanikiwa kuchukua udhibiti wa Mji Mkuu na mipaka ya nchi. Uwanja huo wa ndege ndio sehemu pekee iliyo chini ya udhibiti wa Jeshi la Marekani.

Chanzo: Guardian US

View attachment 1895144
Aisee!
 
Ndio hivyo Sharia Law nzuri ila hakuna anaetaka kuishi nchi za Sharia tunakimbilia kwa Waefeso.
Hujiuluzi hao wazungu miaka yote walikuwa wanafanya nini afghanistan???? Kwanini wasiwaache na nchi zao wakajitawala wenyewe, wameenda kuanzisha vita na vurugu kwenye nchi za watu so they are obliged kuwahakikishia usalama watu wa eneo husika simple as that,
Kama walivyoenda kuharibu nchi ya libya na nchi nyingi including congo, chad etc
Tatizo linalowasumbua ni uelewa , mnakariri sana shule ila hamuelimiki
 
Halafu utakuta hawa ndio wanaandamana kutaka sharia law kwenye nchi walizokimbilia
 
tatizo litaisha pale magharibi watakapoacha kuvamia nchi zao na kuiba rasilimali zao,
Mkuu umewahi kujiuliza kwanini hawawezi kwenda kuiba hizo mali Urusi au Japan au china au korea nk nk

Ni kwa sababu wenzetu kwa asilimia kubwa wanatumia common sense hawaishi kwa kutumia some ancient scriptures zilizotungwa na some ignorant people during the ancient time to control them

Faraq Foda mwanafalsafa wa Kimisri aliwahi kusema hivi
Our arab countries is doomed because we have doctors, Engineers, university professors attending Friday sermons to listen to uneducated person selling them an illusions and encourage them to use violence
 
Mkuu umewahi kujiuliza kwanini hawawezi kwenda kuiba hizo mali Urusi au Japan au china au korea nk nk

Ni kwa sababu wenzetu kwa asilimia kubwa wanatumia common sense hawaishi kwa kutumia some ancient scriptures zilizotungwa na some ignorant people during the ancient time to control them

Faraq Foda mwanafalsafa wa Kimisri aliwahi kusema hivi
Our arab countries is doomed because we have doctors, Engineers, university professors attending Friday sermons to listen to uneducated person selling them an illusions and encourage them to use violence
Hayo ni mawazo yake huyo faraq, mungu ni huyu huyu mmoja na hajawahi kubadilika,hata japan ,vietnam wote walishwahi kuingia vitani na marekani,
MUngu ataendekea kuabudiwa siyo tu kila ijumaa bali kwa kusali mara tano kwa siku hilo halina mjadala
Sasa mzungu aende korea kuna rasilimali gani za kuiba? Tatizo hata kama umesoma bado hujaelimika
Kuna mataifa mungu ameyabariki hata kama ukiyachukia, leo unaweza kuamini kama huyo huyo muarabu unayesema hana akili ana miliki hadi airport kubwa duniani (heathrow) kwenye ardhi ya mzungu
 
Hayo ni mawazo yake huyo faraq, mungu ni huyu huyu mmoja na hajawahi kubadilika,hata japan ,vietnam wote walishwahi kuingia vitani na marekani,
MUngu ataendekea kuabudiwa siyo tu kila ijumaa bali kwa kusali mara tano kwa siku hilo halina mjadala
Sasa mzungu aende korea kuna rasilimali gani za kuiba? Tatizo hata kama umesoma bado hujaelimika
Kuna mataifa mungu ameyabariki hata kama ukiyachukia, leo unaweza kuamini kama huyo huyo muarabu unayesema hana akili ana miliki hadi airport kubwa duniani (heathrow) kwenye ardhi ya mzungu
Hakuna taifa lililo laaniwa wala hakuna taifa lililo barikiwa

Dunia haijawahi kuwa fair wala haitakaa ije kuwa far....... ni wale tu wenye UHURU wa kufanya maamuzi sahihi ndio watashinda na wenye kushikiwa akili watakaliwa

Ngoja sisi tukeshe kwa mwamposa na mzee wa upako kuomba neema za bwana na tushinde sana misikitini mara tano kwa siku tukiomba Allah atufanyie wepesi
Wakati wenzetu wapo busy kufanya kazi kurahisisha na kufurahia maisha
 
Back
Top Bottom