Afrika hii tabia tutaacha lini?

Afrika hii tabia tutaacha lini?

Kinkunti El Perdedo

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2020
Posts
5,200
Reaction score
12,762
Mwalimu Nyerere aliwahi sema "Uchumi tunao, lakini tumeukalia' ithibati ya maneno ya Baba wa taifa ilikuwa sahihi kabisa, kwa kuzingatia baraka ya rasilimali asili na rasilimali watu katika bara letu la Afrika ni nguzo na mtaji muhimu wa kujiletea maendeleo, kwa kupitia vile vilivyo ndani yetu wenyewe.

Lakini kwa sababu ya upumbavu, ukosefu wa maarifa, ubinafsi na kupenda vya kupewa bure au vya nafuu mfano ni hii mikopo ya riba nafuu. Viongozi wetu wamekuwa makuwadi na madalali wa rasilimali zetu(Madini, gesi, Wanyamapori, misitu, ardhi nk) kwa mataifa ya kigeni, kwa kile wanachodai kudumisha ushirikiano katika sekta za kimkakati na kutafuta wawekezaji na uhisani.

Tabia hii ndio imezaa makongamano ambayo nchi zenye uchumi mkubwa mfano USA, Urusi, China nk wamekuwa wakiwaita viongozi madalali na makuwadi wa rasilimali za nchi zao, kwenda kusaini mikataba ya kinyonyaji, kifedhuli na kibaradhuli, pasi kuangalia maendeleo endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Ni jambo la aibu, fedhea na dhihaka mtu kuwa katika utajiri halafu Kutwa kutembeza bakuli ughaibuni, huku ukitambua wazi kabisa kufanya hivyo ni kuuza uhuru wako, utu wako na watu wako, hili hata Rais wa awamu ya pili Mzee Mwinyi (rip) wa Tanzania kashawahi sema.

Ni Afrika pekee ambayo viongozi wa nchi wanajisifu nchi zao kuwa na sifa ya kukopesheka badala ya kujisifu ni kwa namna gani matumizi bora ya rasilimali zilizipo katika nchi zao zimeweza kubadili maisha ya raia wao na mageuzi katika kila sekta na mwisho kutoa mikopo kwa nchi hitaki.

Na kitu kibaya zaidi nao baadhi ya wadau kutoka bara la Afrika na wengi wao wakiwa wasomi wazuri kabisa, wanahoji na kulalamika juu ya kiwango kidogo Cha pesa kinachotolewa na mataifa makubwa kwa ajili ya kugharamia miradi ya kimaendeleo barani Afrika, huu ni upumbavu na uzuzu.

Toka lini nguo ya kuazima kwa jirani ikawa yako milele? Au toka lini mpangaji wa vyumba akampagia kiwango cha Kodi Baba/Mama mwenye nyumba? Hawa ndo aina ya wasomi ambao bwana Denis Mpagaze aliwaandika katika kitabu chake cha "Wasomi Huru Gerezani"

Hakuna taifa duniani ambalo wananchi wake wanavuja jasho na damu kulipa Kodi kwa maendeleo ya taifa lao, wakubali kukupa pesa ya kufanya maendeleo makubwa wewe uliye mvivu wa fikra, kazi, ujuzi na maarifa. Mikopo yote toka nchi zenye uchumi mkubwa malipo yake ni kuchuma rasilimali muhimu kwa ajili ya ujenzi wa nchi zao, huku sisi tukibaki na mashino na mikataba ya kinyonyaji.

Hawa viongozi wetu ipo siku wakishamaliza kuuza rasilimali zote za asili, watageukia kuuza rasilimali watu.
 
Mwalimu Nyerere aliwahi sema "Uchumi tunao,lakini tumeukaria' ithibati ya maneno ya Baba wa taifa ilikuwa sahihi kabisa,kwa kuzingatia baraka ya rasilimali asili na rasilimali watu katika bara letu la Afrika ni nguzo na mtaji muhimu wa kujiletea maendeleo,kwa kupitia vile vilivyo ndani yetu wenyewe.
Yeye alifanya nini wakati wake kwa zaidi ya miaka 24 au aliishia kuikimbia ikulu ?
 
Yeye alifanya nini katika miaka 24 .?

Ukilinganisha na wakoloni na yeye nani aliweza kuiletea Tanganyika maendeleo.
 
Mwalimu Nyerere aliwahi sema "Uchumi tunao,lakini tumeukaria' ithibati ya maneno ya Baba wa taifa ilikuwa sahihi kabisa,kwa kuzingatia baraka ya rasilimali asili na rasilimali watu katika bara letu la Afrika ni nguzo na mtaji muhimu wa kujiletea maendeleo,kwa kupitia vile vilivyo ndani yetu wenyewe.

Lakini kwa sababu ya upumbavu,ukosefu wa maarifa, ubinafsi na kupenda vya kupewa bure au vya nafuu mfano ni hii mikopo ya riba nafuu.Viongozi wetu wamekuwa makuwadi na madalali wa rasilimali zetu(Madini,gesi,Wanyamapori,misitu,ardhi nk) kwa mataifa ya kigeni,kwa kile wanacho dai kudumisha ushirikiano katika sekta za kimkakati na kutafuta wawekezaji na uhisani.Tabia hii ndo imezaa makongamano ambayo nchi zenye uchumi mkubwa mfano USA,Urusi,China nk wamekuwa wakiwaita viongozi madalali na makuwadi wa rasilimali za nchi zao,kwenda kusaini mikataba ya kinyonyaji,kifethuli na kibaradhuli,pasi kuangalia maendeleo endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Ni jambo la aibu,fedhea na dhihaka mtu kuwa katika utajili alafu Kutwa kutembeza bakuri ughaibuni,huku ukitambua wazi kabisa kufanya hivyo ni kuuza uhuru wako,utu wako na watu wako,hili hata Rais wa awamu ya pili Mzee Mwinyi (rip) wa Tanzania kasha wahi sema.

Ni Afrika pekee ambayo viongozi wa nchi wanajisifu nchi zao kuwa na sifa ya kukopesheka badala ya kujisifu ni kwa namna gani matumizi bora ya rasilimali zilizipo katika nchi zao zimeweza kubadili maisha ya raia wao na mageuzi katika kila sekta na mwisho kutoa mikopo kwa nchi hitaki.

Na,kitu kibaya zaidi nao baadhi ya wadau kutoka bara la Afrika na wengi wao wakiwa wasomi wazuri kabisa,wana hoji na kulalamika juu ya kiwango kidogo Cha pesa kinacho tolewa na mataifa makubwa kwa ajili ya kugharamia miradi ya kimaendeleo barani Afrika,huu ni upumbavu na uzuzu.Toka lini nguo ya kuazima kwa jirani ikawa yako milele ? Au toka lini mpangaji wa vyumba akampagia kiwango cha Kodi Baba/Mama mwenye nyumba? Hawa ndo aina ya wasomi ambao bwana Denis Mpagaze aliwaandika katika kitabu chake cha "Wasomi Huru Gerezani"

Hakuna taifa duniani ambalo wananchi wake wanavuja jasho na damu kulipa Kodi kwa maendeleo ya taifa lao,wakubali kukupa pesa ya kufanya maendeleo makubwa wewe uliye mvivu wa fikra,Kazi,ujuzi na maarifa.Mikopo yote toka nchi zenye uchumi mkubwa malipo yake ni kuchuma rasilimali muhimu kwa ajili ya ujenzi wa nchi zao,uku sisi tukibaki na mashino na mikataba ya kinyonyaji.

Hawa viongozi wetu ipo siku wakisha maliza kuuza rasilimali zote za asili,watageukia kuuza rasilimali watu.
Nang'atuka
 
Yeye alifanya nini katika miaka 24 .?

Ukilinganisha na wakoloni na yeye nani aliweza kuiletea Tanganyika maendeleo.
WAKOLONI walituletea maendeleo kuliko maumivu.

Hata Wasomi wakwanza Tanganyika na Zanzibar na Africa nzima ni zao la Ukoloni

Walijenga Shule nyingi, Hospitali, Barabara, Viwanda n.k

Nchi zilizowaacha kwa muda mrefu leo zina neema tele

Wabantu ni jamii Hovyo duniani
 
Mwalimu Nyerere aliwahi sema "Uchumi tunao, lakini tumeukalia' ithibati ya maneno ya Baba wa taifa ilikuwa sahihi kabisa, kwa kuzingatia baraka ya rasilimali asili na rasilimali watu katika bara letu la Afrika ni nguzo na mtaji muhimu wa kujiletea maendeleo, kwa kupitia vile vilivyo ndani yetu wenyewe.

Lakini kwa sababu ya upumbavu, ukosefu wa maarifa, ubinafsi na kupenda vya kupewa bure au vya nafuu mfano ni hii mikopo ya riba nafuu. Viongozi wetu wamekuwa makuwadi na madalali wa rasilimali zetu(Madini, gesi, Wanyamapori, misitu, ardhi nk) kwa mataifa ya kigeni, kwa kile wanachodai kudumisha ushirikiano katika sekta za kimkakati na kutafuta wawekezaji na uhisani.

Tabia hii ndio imezaa makongamano ambayo nchi zenye uchumi mkubwa mfano USA, Urusi, China nk wamekuwa wakiwaita viongozi madalali na makuwadi wa rasilimali za nchi zao, kwenda kusaini mikataba ya kinyonyaji, kifedhuli na kibaradhuli, pasi kuangalia maendeleo endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Ni jambo la aibu, fedhea na dhihaka mtu kuwa katika utajiri halafu Kutwa kutembeza bakuli ughaibuni, huku ukitambua wazi kabisa kufanya hivyo ni kuuza uhuru wako, utu wako na watu wako, hili hata Rais wa awamu ya pili Mzee Mwinyi (rip) wa Tanzania kashawahi sema.

Ni Afrika pekee ambayo viongozi wa nchi wanajisifu nchi zao kuwa na sifa ya kukopesheka badala ya kujisifu ni kwa namna gani matumizi bora ya rasilimali zilizipo katika nchi zao zimeweza kubadili maisha ya raia wao na mageuzi katika kila sekta na mwisho kutoa mikopo kwa nchi hitaki.

Na kitu kibaya zaidi nao baadhi ya wadau kutoka bara la Afrika na wengi wao wakiwa wasomi wazuri kabisa, wanahoji na kulalamika juu ya kiwango kidogo Cha pesa kinachotolewa na mataifa makubwa kwa ajili ya kugharamia miradi ya kimaendeleo barani Afrika, huu ni upumbavu na uzuzu.

Toka lini nguo ya kuazima kwa jirani ikawa yako milele? Au toka lini mpangaji wa vyumba akampagia kiwango cha Kodi Baba/Mama mwenye nyumba? Hawa ndo aina ya wasomi ambao bwana Denis Mpagaze aliwaandika katika kitabu chake cha "Wasomi Huru Gerezani"

Hakuna taifa duniani ambalo wananchi wake wanavuja jasho na damu kulipa Kodi kwa maendeleo ya taifa lao, wakubali kukupa pesa ya kufanya maendeleo makubwa wewe uliye mvivu wa fikra, kazi, ujuzi na maarifa. Mikopo yote toka nchi zenye uchumi mkubwa malipo yake ni kuchuma rasilimali muhimu kwa ajili ya ujenzi wa nchi zao, huku sisi tukibaki na mashino na mikataba ya kinyonyaji.

Hawa viongozi wetu ipo siku wakishamaliza kuuza rasilimali zote za asili, watageukia kuuza rasilimali watu.
Duu ila kwenye gas ⛽ wahusika Mungu anawaona yaani tuna gesi yetu lakini tunayo tumia kwasasa inatoka nje? Kweli hata kama ni kujizima data, lakini imepitiliza
 
Duu ila kwenye gas ⛽ wahusika Mungu anawaona yaani tuna gesi yetu lakini tunayo tumia kwasasa inataka nje? Kweli hata kama ni kujizima data, lakini imepitiliza
Taifa liliimbishwa neema na nafuu ya umeme wa gesi,kumbe makuwadi na madalali washa kula chao mapema.Mwisho leo hii ni mapambio ya umeme wa maji.
 
Taifa liliimbishwa neema na nafuu ya umeme wa gesi,kumbe makuwadi na madalali washa kula chao mapema.Mwisho leo hii ni mapambio ya umeme wa maji.
Hiyo gesi unaweza kuta huko chini kwa chini wameunganisha mitambo tayari gesi inaenda kwao, mimi nilishangaa eti mitambo iko uingereza inaona nini kinafanyika Tanzania kwenye mradi wa gesi
 
Mwalimu Nyerere aliwahi sema "Uchumi tunao, lakini tumeukalia' ithibati ya maneno ya Baba wa taifa ilikuwa sahihi kabisa, kwa kuzingatia baraka ya rasilimali asili na rasilimali watu katika bara letu la Afrika ni nguzo na mtaji muhimu wa kujiletea maendeleo, kwa kupitia vile vilivyo ndani yetu wenyewe.

Lakini kwa sababu ya upumbavu, ukosefu wa maarifa, ubinafsi na kupenda vya kupewa bure au vya nafuu mfano ni hii mikopo ya riba nafuu. Viongozi wetu wamekuwa makuwadi na madalali wa rasilimali zetu(Madini, gesi, Wanyamapori, misitu, ardhi nk) kwa mataifa ya kigeni, kwa kile wanachodai kudumisha ushirikiano katika sekta za kimkakati na kutafuta wawekezaji na uhisani.
Naunga mkono hoja tena Mwalimu Nyerere alisisitiza hakuna umasikini mbaya kabisa kama umasikini wa fikra!. Jambo hili niliwahi kuliulizia Umasikini wa Afrika, Je tumelogwa?. Licha ya Kuongoza kwa Utajiri, Tuna Bilionea 1 tu kwenye Top Hundred Mabilionea wa Dunia. Ni Aliko Dangote Pekee!

P
 
Next 6 years..
What will we have left!?
😇😇
 
Ni laana ya CCM, serikali ya Tanzania ina matumizi makubwa na ya anasa kuliko China, kuna Ikulu kila Wilaya zimejengwa kwa mabilioni eti za kulala Rais siku akitembelea kuna Wilaya mpaka anamaliza miaka 5 hajawahi kutembelea lakini kuna nyumba inamsubiri kulala siku akitembelea na hapo hapo kuna zahanati hazina dawa na watumishi, wizi na ujinga ndiyo maendeleo yetu.
 
Back
Top Bottom