Tetesi: Afrika Kusini: Rais Magufuli adaiwa kutunukiwa Tuzo ya Amani ya Mandela (Mandela Peace Prize)

Status
Not open for further replies.
Utaelewa tu, mdogomdogo

Kushabikia ujinga ni tatizo. Hivi unaweza kuona kwenye hizo tuzo yupo Nkurunzinza na bado ukatoka unashangilia rais wetu kuwepo? Hii aibu mnaitia nchi ni ajabu na kweli. Halafu huu upuuzi mnautumia kama sehemu ya kujifariji kwa kile alichokisema Kakobe juzi. Shida ukweli hauzuiliki kirahisi.
 

Hiki ulichoongea kinaonyesha ni jinsi gani mnaendesha maisha yenu kwa kutetea uovu. Bado Kakobe yuko sahihi na ukweli utabaki kuwa ukweli. Huwezi kizuia ukweli kwa kutumia uongo
 
Acha upuuzi kwani we na mmeo mkimchikia jpm unadhani ni wote
 
Huu ni uongo mwenye uthibutisho hii tuzo imetoka atuwekee link hapa vinginevyo ni sawa na kujamba alafu mnaziba pua wenyewe!
 
Hii habari ina walakini. Uwalakini wake ni kuonekana kwenye tovuti moja tu duniani kote ya azaniapost.com. Kadhalika, uwalakini wake upo kwa Nkurunzinza kupewa tuzo hiyo inayodaiwa kuwa ni ya Mandela. Na kama hii habari ingekuwa ya kweli, hakika nawaambia, gazeti fulani hivi lingeiandika habari hii kila kurasa ya toleo lake la leo, na hata kesho na hadi Jumatatu ya mwaka mpya. Sijajua hao walioitoa habari hii walikuwa wana dhamira gani? Nakumbuka kuna wakati kuna watangazaji wa TBC walifukuzwa kazi kwa kudai Rais Magufuli amesifiwa na Donald Trump, ila wanahabari wale walirudishwa kazini kwa parole ya Rais. Ha ha ha ha ha ha Ha.
 
Nkurunzinza naye kazawadiwa? Angalieni hizo tuzo badala ya ku-promote democracy ndo zikawa zinaididimiza
Afu yy si kapewa ya ujasiri ( Mandela courage) so ataendeleza ubabe wake maana huo ndo ujasiri unaompa hizo tuzo
 
Hizi tuzo zingine bwana..nielekezeni namna ya kufungua kesi kupinga huyu mtu kupewa tuzo..hakustaili kabisa na vielelezo vya kwanini nakataa hii tuzo asipewe ninavyo..SISI RAIA NDO TUNATUNZA AMANI NA WALA SIYO YEYE.umetubomolea nyumba tumekaa kimya mnapiga watu risasi tumekuvumilieni..watu wanaokotwa kwenye mifuko bahari bado tunavumilia..waandishi wanapotezwa na wasiojulikana bado tunavumilia..na SASA TUKISEMA UFUATE KATIBA ULIYOAPA KUILINDA UNAYOVUNJA KILA SIKU UNATUITA WACHOCHEZI..NGOJA CKU HAO WACHOCHEZI WATAKAPOAMUA KUPLAY PARTY YAO YA UCHOCHEZI KAMA AMANI ITAKUWEPO
 
Si lazima wote tuone nyekundu!

Ni kweli ila uwe na aibu. Haiwezekani uone tuzo bila kujali ni za kweli au uongo zinamuhusisha na Nkuruzinza kisha ushabikie kwamba hata rais wetu kapata. Kama una akili timamu unapaswa kutia shaka.
 

Hizo tuzo ziktakuwa za mtaa wa Lumumba
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…