Afrika tuna shida sana, Kiongozi gari ya milion 600?

Afrika tuna shida sana, Kiongozi gari ya milion 600?

Mimi ni mtu wa enzi za Mwalimu, kuwa na private car ilionekana ni ufahari na hata kuwa na TV ilikuwa inahesabika ni anasa!. Kumbe usafiri ni kitu muhimu sana for mobility na if you can afford to get the best, why not?. Escort ya Nyerere ilikuwa Peugeot 404, mawaziri wa Nyerere walitumia Peugeot 504!. Benz ya rais ilikuwa E Class 240, Tajiri Lord Rajpar akaleta nchini S Class 720, alikamatwa na kutiwa ndani kwa kosa la kumiliki gari la ufahari kuliko la Mkuu wa nchi.
Ha haa! wewe mzee mwenzangu unakumbuka enzi zile kuendesha gari siku ya jumapili mwisho ilikuwa saa nane mchana? Na enzi zile hata hao waliokuwa na magari ya private walikuwa wachache maana kibali cha kuagiza gari kilikuwa kinatoka ikulu (au ilikuwa ni wafanyakazi wa serikali tu?)
 
Mimi ni mtu wa enzi za Mwalimu, kuwa na private car ilionekana ni ufahari na hata kuwa na TV ilikuwa inahesabika ni anasa!. Kumbe usafiri ni kitu muhimu sana for mobility na if you can afford to get the best, why not?. Escort ya Nyerere ilikuwa Peugeot 404, mawaziri wa Nyerere walitumia Peugeot 504!. Benz ya rais ilikuwa E Class 240, Tajiri Lord Rajpar akaleta nchini S Class 720, alikamatwa na kutiwa ndani kwa kosa la kumiliki gari la ufahari kuliko la Mkuu wa nchi.

Sasa TV sio anasa, magari ni mobility rais anatumia S Class ya 720, Speaker na CJ wao ni S Class 500!, kwanini wabunge, mawaziri, ma PS na wakurugenzi wasitumie ma V8?. Viongozi wetu wangekuwa wanatumia magari armored, Tundu Lissu angefanywa vile?.

Mimi naishi njia ya Bagamoyo, kila Mzee wa Msoga akieanda na kurudi kutoka Msoga, huku rodini ni shughuli!, nikashauri kwanini asitumie chopper?. Misafara ya viongozi inachosha, inatesa na kurudisha nyuma maendeleo, IGP Sirro peleka Traffic Sweden kujifunza misafara ya wenzetu, Time is Money!
Nashauri wenye uwezo na private jet walete wenye uwezo na Chopper walete, watu wa V8 walete na sisi wa TZ 11, bajaj, boda boda na dala dala, pia tuendelee!.
P
Dah we jamaa/bepari
 
Nikiwa Rais naondoa huu upuuzi wa magari..kila mtu ajinunulie gari lake au adandie daladala..

Mbona wafanyakazi wengine wanatumia gharama zao kufika maeneo yao ya kazi?.

Gari zitakuwa chache tu na zitakuwa hazina mwenyewe..ukitokea uhitaji wa kusafiri kikazi ndo utatumika tu and not otherwise.
Mambo mwafrika anayoyafanya yanaaibisha dunia hasa kwenye hii century ya 21...Kisha hilo V8 linaenda kufungua madarasa ya mkopo wa WB?!
 
Hebu lipeni kodi acheni kubwabwaja

Siku zote wanadam ndo mlivyo ,ukiona mwenzako anafaidi huchelewi kumtilia figisu,viongozi ni watoto wa masikini ,waacheni waendelee kula mema ya nchi hadi pale milija itakapo katika,hata tuwaweke nyie wana jf kwenye ulamba asali ,mtatufanyia mambo ya ajabu hadi tutamani kufa

Waacheni watembelee 600ml ,ni mda wao,mda ukiisha watatoka
Point ya kufungua mwaka
 
Kuambatana na Rais haina maana uwe na hadhi sawa na Rais.

Wewe umeona hilo gari pekee ndo lenye hadhi ya mkuu wa mkoa?

Akitembelea Prado, Harrier ama Vitz hawezi kuwa na hadhi ya mkuu wa mkoa?
Au Hard top mkonga L/Cruiser !
 
Huwa tunawapiga picha na haya magari wakiwa mjini.

Lakini kiuhalisia uwe mkuu wa mkoa Ruvuma halafu uanze ziara za Nantumbo huko sijui wilaya gani nyingine ambazo miundombinu ya barabara ovyo. Mara umeitwa Dodoma utoke Mwanza usiku wa manane

Au ziara za mawaziri mikoani sehemu zingine mapori, milima, upite kwenye mto; mjomba kama unatumia gari ‘tia maji, tia maji’ kila siku unabadili shock absorbers au unajikuta unatafuta fundi gari maporini na awepo huyo fundi mwenyewe.

Jumlisha na shughuli ya kushinda njiani siku kadhaa au week, surely unahitaji gari comfortable kidogo.

Binafsi sikubaliani na matumizi mengi ya ovyo ila kwenye magari naona logic yake, it is justified.
Huko wanafuata nini? Hakuna watumishi wengine wa umma?

Ni self justifications tu zisizo na maana na kutotaka kugatusha madaraka pamoja na resources
 
Back
Top Bottom