Pre GE2025 Ahobokile Mwaitenda anusurika kuuawa kwa kuukosoa mkataba wa bandari!

Pre GE2025 Ahobokile Mwaitenda anusurika kuuawa kwa kuukosoa mkataba wa bandari!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ndugu Watanzania!
Tumeongea Ahobokile Mwaitenda ikiwa ni siku moja baada ya kunusurika kuuawa au kutekwa na watu wasiojulikana. Mwaitenda ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa CHADEMA na alikuwa ni Mgombea Ubunge Jimbo la Rungwe, Mbeya Uchaguzi wa Oktoba 2020 kupitia CHEDEMA.

Usiku wa 7 Julai 2023 akiwa anatokea uelekeo wa Mwenge kuelekea Goba, alivamiwa na watu 4 (wanaume 3 na mwanamke 1). Walimkimbiza na gari wakimpigia kelele asimame. Akifikiri huenda amegonga gari bila kujua, akakimbilia na karibu na Shule ya Makongo na kusimama.

Aliposimama wakashuka watu hao wakaanza kumpiga ngumi na mateke huku wakimfokea wakisema anajifanya anajua kusema sana juu ya Mkataba wa Bandari. Walinzi wa Shule ile waliokuwa mbali walipoanza kusongelea pale, watekaji wakamlazimisha Mwaitenda aingie kwenye gari. Muda huo tayari alikuwa mateka.

Aliendelea kuendesha gari huku wakimfuata na ndipo akakimbilia katika Kituo cha Polisi Kawe na kugonga Geti kwa gari. Alishuka haraka na kujisalimisha huku akiwa amenyoosha mikono juu. Wale watu wakegeuza gari na kukimbia.

Ndugu Watanzania! Jana tuliandika pia juu ya vitisho walivyopata wanasheria wanakosoa pia Mkataba wa Bandari ambao ni Dkt. Nshala na Boniface Mwabukusi! Mhe. Balozi Dkt. Willbrod Slaa alitishwa hadharani na kiongozi mmoja wa serikali baada ya Dkt. Slaa kuukosoa mkataba! Vitisho ni vingi sana na hatuwezi kuelezwa kila mtu anayetishiwa uhai wake.

Sisi Askofu Mwamakula tumesikitishwa sana na vitendo hivi vya kutaka kuteka, kuua na hata kunyamazisha watu waoikosoa serikali kuhusu Mkataba wa Bandari kati ya Ufalme wa Dubai na Serikali ya Tanzania. Sisi tunatoa wito kwa Serikali kutoa kauli kuhusu vitendo hivi kwani wafanyao vitendo hivyo wanajinasibisha moja kwa moja na serikali. Kukaa kimya kwa Serikali katika matukio yaliyojitokeza sasa itachukuliwa kuwa ni Serikali inayoratibu na kufadhili vitendo vya kutisha na kuteka na kutaka kuua watu.

Sisi Askofu Mwamakula tunatoa wito pia kwa viongozi wote wa dini ili wakemea kwa nguvu vitendo hivyo kwani vinalenga katika kufinya haki na kuendelea kuondoa amani na utulivu katika taifa letu. Uhuru wa kutoa maoni ni haki ya kila raia wa nchi hii. Hakuna mtu au taasisi ye yote ikiwemo serikali aliye na haki ya kuzuia wengine wasitoe maoni yao katika nchi yao.

Tunaendelea kuonya na kutahadharisha kuwa ikiwa yeyote anayeikosoa Serikali ya Tanzania juu ya Mkataba wa Bandari atadhurika au hata kuuawa, basi watu wote waliowahi kutoa kauli hadharani kuwatisha wakosaoji, basi watu hao watawajibika sambamba na serikali endapo pia yenyewe haitajitenga na vitendo hivyo.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania na Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Uamsho Duniani.
Dar es Salaam, 8 Julai 2023; 21:11 pm.

Waione na kuisoma:
1. Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC)
2. Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA)
3. Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT)
4. Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT)
5. Tanganyika Law Society (TLS)
6. Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania
7. Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania
8. Umoja wa Ulaya
9. Umoja wa Mataifa (UN)
10. Kituo cha Haki za Binadamu (LCHR)
11. Vyombo vyote vya Habari vya ndani na Nje
12. Sheikh Ponda Issa Ponda
13. Askofu William Mwamalanga
Akome, wapotoshaji wote washughulikiwe..

Hao mabeberu ndio watawasaidia nini? Mna Haki ya uhuru wa maoni ila sio upotoshaji Wala kudhalilisha Mamlaka.
 
Ndugu Watanzania!
Tumeongea Ahobokile Mwaitenda ikiwa ni siku moja baada ya kunusurika kuuawa au kutekwa na watu wasiojulikana. Mwaitenda ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa CHADEMA na alikuwa ni Mgombea Ubunge Jimbo la Rungwe, Mbeya Uchaguzi wa Oktoba 2020 kupitia CHEDEMA.

Usiku wa 7 Julai 2023 akiwa anatokea uelekeo wa Mwenge kuelekea Goba, alivamiwa na watu 4 (wanaume 3 na mwanamke 1). Walimkimbiza na gari wakimpigia kelele asimame. Akifikiri huenda amegonga gari bila kujua, akakimbilia na karibu na Shule ya Makongo na kusimama.

Aliposimama wakashuka watu hao wakaanza kumpiga ngumi na mateke huku wakimfokea wakisema anajifanya anajua kusema sana juu ya Mkataba wa Bandari. Walinzi wa Shule ile waliokuwa mbali walipoanza kusongelea pale, watekaji wakamlazimisha Mwaitenda aingie kwenye gari. Muda huo tayari alikuwa mateka.

Aliendelea kuendesha gari huku wakimfuata na ndipo akakimbilia katika Kituo cha Polisi Kawe na kugonga Geti kwa gari. Alishuka haraka na kujisalimisha huku akiwa amenyoosha mikono juu. Wale watu wakegeuza gari na kukimbia.

Ndugu Watanzania! Jana tuliandika pia juu ya vitisho walivyopata wanasheria wanakosoa pia Mkataba wa Bandari ambao ni Dkt. Nshala na Boniface Mwabukusi! Mhe. Balozi Dkt. Willbrod Slaa alitishwa hadharani na kiongozi mmoja wa serikali baada ya Dkt. Slaa kuukosoa mkataba! Vitisho ni vingi sana na hatuwezi kuelezwa kila mtu anayetishiwa uhai wake.

Sisi Askofu Mwamakula tumesikitishwa sana na vitendo hivi vya kutaka kuteka, kuua na hata kunyamazisha watu waoikosoa serikali kuhusu Mkataba wa Bandari kati ya Ufalme wa Dubai na Serikali ya Tanzania. Sisi tunatoa wito kwa Serikali kutoa kauli kuhusu vitendo hivi kwani wafanyao vitendo hivyo wanajinasibisha moja kwa moja na serikali. Kukaa kimya kwa Serikali katika matukio yaliyojitokeza sasa itachukuliwa kuwa ni Serikali inayoratibu na kufadhili vitendo vya kutisha na kuteka na kutaka kuua watu.

Sisi Askofu Mwamakula tunatoa wito pia kwa viongozi wote wa dini ili wakemea kwa nguvu vitendo hivyo kwani vinalenga katika kufinya haki na kuendelea kuondoa amani na utulivu katika taifa letu. Uhuru wa kutoa maoni ni haki ya kila raia wa nchi hii. Hakuna mtu au taasisi ye yote ikiwemo serikali aliye na haki ya kuzuia wengine wasitoe maoni yao katika nchi yao.

Tunaendelea kuonya na kutahadharisha kuwa ikiwa yeyote anayeikosoa Serikali ya Tanzania juu ya Mkataba wa Bandari atadhurika au hata kuuawa, basi watu wote waliowahi kutoa kauli hadharani kuwatisha wakosaoji, basi watu hao watawajibika sambamba na serikali endapo pia yenyewe haitajitenga na vitendo hivyo.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania na Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Uamsho Duniani.
Dar es Salaam, 8 Julai 2023; 21:11 pm.

Waione na kuisoma:
1. Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC)
2. Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA)
3. Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT)
4. Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT)
5. Tanganyika Law Society (TLS)
6. Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania
7. Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania
8. Umoja wa Ulaya
9. Umoja wa Mataifa (UN)
10. Kituo cha Haki za Binadamu (LCHR)
11. Vyombo vyote vya Habari vya ndani na Nje
12. Sheikh Ponda Issa Ponda
13. Askofu William Mwamalanga
hata hawajui kwamba wakiendeleza huo ujinga, wananchi nao wataamua kuchukua sheria mkononi, na hapo ndio unakuwaga mwanzo wa vita, mmarekani amekaa paleee anasuburi tugombane ili achague wa kumpa silaha watu wauane yeye auze silaha au achote dhahabu na gesi. hawa waarabu wana faida gani Tanzania hata kuja kutuondolea amani namna hii? angekuwepo magufuli wangekuja namna hii kweli ? kwamba wanagombanisha serikali na wananchi, si waondoke tuishi kwa amani kama tulivyozoea?
 
Screenshots_2023-07-08-04-03-39.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watekaji wakamlazimisha kuingia Kwa gari akawa mateka..
Halafu akaendesha gari peke yake huku wanamfata??
Hii tabia ya kunyamazisha watu baada ya kufanya kazi kwa namna fulani wakati wa dhalimu, na sasa tunaona taratibu inaanza kurejea. Nina hakika tabia hii itarudi rasmi kadiri mikataba mingine ya hatari itakavyokuwa inaanza kukaa wazi. Watakaokuwa salama ni nyie mnaokula cake ya taifa kwa sasa.
 
Nashauri CHADEMA iandae timu ya ulinzi hasa kwa wale waliopo kwenye hatari ya kushambuliwa,ila hawa walinzi wasitembee nao kama Mabodigadi ila wawe wanakaa mbali kidogo bila kuonekana kama wanamlinda,ili hawa watekaji wakijichanganya kwanza Tuwakamate wao,tuwateke ili tuwajue ni kina nani,Unaweza kuta ni UVCCM tu wanatisha watu kama sivyo wakimdaka kweli 'asiyejulikana'kweli hapo tuuweke ukweli hadharani ili serikali ikose pa kujificha.

Namaanisha tumteke Mtekaji kwanza ili tumjue nani kamtuma.
🤣🤣🤣🤣🤣 Tuliwaambia lakini hamkusikia , acheni upotoshaji hao beberu hawatawasaidia..

Kwa taarifa yenu kuanzia Egypt Hadi Rwanda,Kenya Hadi Senegal kwote huko Wapinzani wanapelekewa moto na Wazungu wanakuja kuwekeza.

Ni hivi Jiwe alikuwa na sera za Kijamaa ambazo Wazungu hawazijubali Samia ana sera za ubepari ambazo Wazungu wanazikubuli so mambo ya siasa Wala hawatayapa umuhimu ikiwa maslahi ya Nchi yanazingatiwa..

Tutaenda Kwa staili hiyo na Ile ya Uongozi wa JK.
 
Tusipokuwa makini hata mlima Kilimanjaro siku moja atauziwa mwarabu. Tuna viongozi washamba sana


Tunataka BANDARI zetu tulipihania Uhuru Kwa kutaka Mali zetu Leo Samia MANGUNGO anagawa Kwa waarabu , DPWORLD waondoke
Kweli dunia inazunguka,eti leo Etwege anawakosoa viongozi wa ccm!!
 
Tusipokuwa makini hata mlima Kilimanjaro siku moja atauziwa mwarabu. Tuna viongozi washamba sana


Tunataka BANDARI zetu tulipihania Uhuru Kwa kutaka Mali zetu Leo Samia MANGUNGO anagawa Kwa waarabu , DPWORLD waondoke
Anawajua wachagga wamwulize Bichwa korosho aliingiza pua zake saivi yuko wapi ? Mwanae Sabazuri naye katulia analea mishono ya wahuni waliomtega na sabuni 😂
 
mshaanza michezo yenu ya kutekana na kuuana halafu msingizie wengine
 
Tusipokuwa makini hata mlima Kilimanjaro siku moja atauziwa mwarabu. Tuna viongozi washamba sana


Tunataka BANDARI zetu tulipihania Uhuru Kwa kutaka Mali zetu Leo Samia MANGUNGO anagawa Kwa waarabu , DPWORLD waondoke
Nimecheka sana mh waziri mkuu kuna clip nimeona anasema watanzania tuwamini , kwamba serikali ya tz imewatega DP WORLD, Ila Majaliwa kiboko, unamtegaje Dp WORLD kwa mkataba ule?
 
Sasa imekua the comedy show 😂😂 watanganyika wanaburuzwa tu, huku wakizidi kufanywa mazuzu kwa Drama kama hizi.
 
Back
Top Bottom