Aibu: Air Tanzania yalalamikiwa kuchelewesha abiria na kisha kuwakodia hoteli ya hadhi ya chini

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Baadhi ya wateja wa Air Tanzania wamelalamika mtandaoni kuwa ndege yao ya Air Tanzania iliyokuwa iwapeleke Dar es Salaam ilichelewa jambo lililosababisha wafike Dar kwa kuchelewa.

Air Tanzania iliwatafutia vyumba vya kufikia ambavyo wateja hao wamelalamika kuwa vilikuwa na hadhi ya chini sana.
---
Our flight to Dar res salaam with Air Tanzania got delayed, we ended up landing in Dar very late. Air Tanzania booked us into a hotel room for the night and it was the ghettoest hotel I have ever been in lol

The window view from our hotel room was giving Matapi.



Tazama video hii hapa chini:

Your browser is not able to display this video.
PIA SOMA
- Huduma kwa wateja ya Air Tanzania siyo nzuri
 
Alitegemea CENTRAL PARK VIEW kama New York ili apost status.
Huu utaratibu wa kulipia abiria hotel unatumika kama njia moja ya upigaji pale ATCL.
 
Afrika Bado kuna shida sana.

Walifuta Fastjet wakidhani wanaweza kutoa huduma bora.

Ndege moja wafanyakazi 100, hahaha
 
Watanzania hatuwezi kuendesha chochote kwa ujinga wetu.


Niliwahi kuandika hivi:


Na hivi:

 
Mwaka ajana naenda Uwanja wa andege moja wapo wa Kimataifa hapa Tanzania, naondoka na Halotel yangu.

Nafika Uwanjani no Cellphone internet lakini pia Wife ya uwanjani ni mbovu kupita maelezo.

Hata kupost ujumbe whatsapp haiwezi.
Tunaelekea Dubai-hapo Airpot internet yake ni ya maajabu, speed ambayo sijawahi kushuhudia.

Nikajiuliza hivi sisi wafrika kwanini tuko nyuma kila kitu. Wale Mainjinia wa Viwanja vya ndege, wafanyakazi, mafundi wa ICT n.k hakuna anayeona hili au hawatembei kujifunza kwa wengine?

Nakaa Dubai siku Tatu baadae naelekea Uturki Instabul very wonderful services.

Nikarudi Tena Nyumbani nikadhani labda siku ile mtandao ulikuwa mbovu......nakutana wasafiri wanalalamikia Internet mbovu mtu hata ndugu yake anashindwa kuwasiliana.

Viwanja vyetu vinapokea maelfu ya wageni kutoka duniani kote. Kukosa internet ya uhakika kwa watu kuwasiliana ni aibu kubwa sana.
 
Na Sasa hivi nyie ndio mmeshika Hatamu, ujinga wenu uko dhahiri
 
Eti bwana kama imechelewa kwa bahati Mbaya kuna ulazima wa kulipia Vyumba watu? Mbona tunalala airport hata nchi zingine?
Sikumbuki ni masaa mangapi ila yakizidi hayo masaa inatakiwa upelekwe Hotel Ethiopian Airline wana utaratibu huo na SAA na Rwanda kidogoo...Bus tu Intercape lina utaratibu huo mkuu au Greyhound bus..
 
Kutoka wapi, uendeshaji wa ndege ni gharama sana pia ndege inaweza beba abiria hata 15 badala ya 100 huduma za usafiri wa ndege ni ghari sana, na Ndiyo maana wanapata hasara
 
Wabongo hatuna culture nzuri kwneye kutoa huduma. Haya mambo yanatakiwa yaanze kufindishwa tokea chini kabisa
 
CCM siyo watanzania wote.
 
Vyumba vichafu sana hivyo kiasi kwamba inaweza kupelekea abiria kutapika.Atcl mjitathimini.ndege siyo basi la kuamua tu kuchelewesha aboria pasipo sababu za msingi
 
Ndege ilikua inatoka wapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…