Aibu kuona Wasabato wanaokataa nguruwe na pombe wamelegeza msimamo kuhusu kuchonga nywele/ndevu, kuvaa hereni na kusuka

Aibu kuona Wasabato wanaokataa nguruwe na pombe wamelegeza msimamo kuhusu kuchonga nywele/ndevu, kuvaa hereni na kusuka

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Ni moja ya kanisa linaloendelea kufuata sheria za agano la kale ikiwemo kuheshimu sheria zilizowekwa na Mungu kuhusu uchambuzi wake wanyama wa kula pamoja na kuendelea kuamini Pombe ni chukizo kwa Mungu, Siku yao ya kuabudu huanza ijumaa jioni hadi jumamosi kama ilivyo kwa wayahudi wanaoabudu siku hio kwa kuiita shabat (Sijajua uhalali wa wao kuona ndio siku ya sabato)

Ila sasa kuna baadhi ya sheria wameanza kupwaya.

Miaka ya 90s na 2000s mwanzoni nilishuhudia wasabato wengi wakienda kunyoa walikuwa wanakataa kuchongwa mpaka wakajipatia umaarufu wa mtindo wao kuitwa "kunyoa kisabato", Lakini leo hii hali ni tofauti, ukienda makanisa ya wasabato utaona mpaka wachungaji wamepiga panki na kuzichonga nywele, ndevu wamechonga kwa mtindo wa O.

Huyu ni mojawapo wa kundi la wachungaji wengi wa kisabato wanaochonga nywele na ndevu.

1697022122665.png


Pia mabinti wengi sana walikuwa hawasuki wala kuvaa hereni waliamini kwa
mujibu wa Nyaraka za Mitume- Paulo na Petro, KUSUKA kumetizamwa kama MAPAMBO, Kwa mujibu wa Biblia, MAPAMBO MAZURI ni Tabia Njema, utu wa Moyoni, kuvaa kwa kujisitiri, kujikubali uumbaji wako bila kujitoboa (hereni), kuchora tattoo, ama kubadili mtindo wa nywele ulizoumbiwa mfano kuzirefusha nywele fupi kwa kuzisuka rasta.


, lakini leo hii imeshakuwa kawaida kuwakuta hereni zinaninginia masikioni na kila wiki/mwezi msuko mpya.

1697022248897.png
 
Ni Suala la mda tuu
Siku zote huwa nasema Dini za kikristo nyingi zinageuka kuwa kituko kwasababu hakuna misimamo ya kukemea maovu, vitu vinachukuliwa poa kwa kisingizio kwamba kila mtu ana maamuzi yake,

mtu kaenda kutubu kanisani dhambi zake za uzinzi na kutafuta njia ili kuziepuka lakini kanisa linaruhusu mabinti kuingia huku wamevaa magauni yanayowachora shepu, ni sawa na mraibu wa dawa za kulevya kupelekwa sober house inayoruhusu kutumia madawa.
 
Nashangaaa sana
Ukristo unakoelekea ni kama Ulaya, makanisa ya Ulaya hayakuwa na misimamo, matokeo yake makanisa yamegeuka kituko watu wameacha kwenda.

Misimamo!! Misimamo!! Misimamo!!
Uovu ukemewe sio wa kuukalia kimya!!
 
Ni moja ya kanisa linaloendelea kufuata sheria za agano la kale ikiwemo kuheshimu sheria zilizowekwa na Mungu kuhusu uchambuzi wake wanyama wa kula pamoja na kuendelea kuamini Pombe ni chukizo kwa Mungu, Siku yao ya kuabudu ni Jumamosi kama ilivyo kwa wayahudi wanaofanya hivyo tangu enzi za kale (Sijajua uhalali wa wao kuona ndio siku ya sabato)

Ila sasa kuna baadhi ya sheria wameanza kupwaya.

Miaka ya 90s na 2000s mwanzoni nilishuhudia familia kibao watoto wakinyolewa kinyozi alikazwa kuwachonga nywele, Lakini leo hii ukienda makanisa ya wasabato utaona mpaka wachungaji wamepiga panki na kuzichonga nywele, kidevuni wamechonga ndevu kwa mtindo wa O.

Huyu ni mojawapo wa kundi la wachungaji wengi wa kisabato wanaochonga nywele na ndevu.

View attachment 2778741

Pia mabinti wengi sana walikuwa hawasuki wala kuvaa hereni, lakini leo hii imeshakuwa kawaida kuwakuta hereni zinaninginia masikioni na kila wiki/mwezi msuko mpya.

View attachment 2778744


kukemea mapepo wakati vitu vinavyoleta mapepo havikemewi ni sawa na kufukuza nzi wakati unatunza uchafu,
Kunyoa na kusuka na kuvaa hereni vinaletaje mapepo?
 
Kunyoa na kusuka na kuvaa hereni vinaletaje mapepo?
Mfano mdogo tu unasuka rasta ama weave kurefusha nywele, Je huoni huko ni kumkiuka Mungu aliempa mtu nywele fupi kwa sababu alizoona anafaa kuwa na nywele fupi ?

Ujitoboe sehemu za mwili sikioni, puani, ulimi ili uweke hereni,huku ni kumkashifu Mungu wako aliekuumba.
 
Mfano mdogo tu unasuka rasta ama weave kurefusha nywele, Je huoni huko ni kumkiuka Mungu aliempa mtu nywele fupi kwa sababu alizoona anafaa kuwa na nywele fupi ?

Ujitoboe sehemu za mwili sikioni, puani, ulimi na kuweka hereni huku sio kumkiuka Mungu ?
Wewe Dini gani kwanza

Kila Dini ina matatizo yake, ukisema tuanze kushushuana mbona ni kasheshe.

Hao wote ni binadamu kuna kuteleza, pia kwenye maandiko hawajaweka namna ya unyoaji au husukaji... Usilete hukumu ambazo hazipo
 
Wewe si ni mvaa kobazi.. Diamond Platnumz anafanyeje, Hamisa Mobetto anavaaje, Zari the Bosslady anavaaje...

Wavaa kobazi ndio wanaongoza kwa kuvaa Heleni, kuchora tatuu, kwenda maklabu, wanawake wao ndio wanaongoza kwa umalaya, angalia kina zuchu, wanapigwa pumbu tu awaolewi
Kobazi Huwa navalia chumbani kwako?
 
Wewe si ni mvaa kobazi.. Diamond Platnumz anafanyeje, Hamisa Mobetto anavaaje, Zari the Bosslady anavaaje...
Jua kujulikana ni wa dini flani na mtu kuwa na imani ya dini yake. Dini ni imani sio kutambulika tu kwamba una jina la dini flani, wazazi ni dini flani, umezikwa dini flani, n.k.

Mtu anaweza kutambulika ni mkristo ama muislamu lakini ni mshirikina balaa.

Kuna mganga nguli huko Njombe alifariki mwaka jana allitwa "Mwandulami" pia alikuwa na wake nane ila alijulikana ni mkatoliki na akazikwa kikatoliki.

Kina Diamond kuvaa hereni sio uislamu ni sawa na wanaocheza video za x huku wamevaa misalaba huo si ukristo,

Ndio maana kuna siku ya kiama na utaangaliwa matendo yako, sio ulizaliwa dini gani ama ulienda kanisani / msikitini mara ngapi
 
Mtu kukataza kunyoa kusuka ua kutinda ni msimamo wake tu... Haina uhusiano na wasabato...

Kusuka hasa rasta wengi wanakataa kwa sababu hawajui nywele zinatoka wapi, au kutinda ni kwa sababu ya kiafya tu kwa sababu pale wanakwangua ngozi uwezi kujua mashine imetumika na kwa nani

Lakini kimaandiko hakuna hayo maelezo... Huo ni msimao wa wahusika tu
 
Jua kujulikana ni wa dini flani na mtu kuwa na imani ya dini yake. Dini ni imani sio kutambulika tu kwamba una jina la dini flani, wazazi ni dini flani, umezikwa dini flani, n.k.

Mtu anaweza kutambulika ni mkristo ama muislamu lakini ni mshirikina balaa.

Kuna mganga nguli huko Njombe alifariki mwaka jana allitwa "Mwandulami" pia alikuwa na wake nane ila alijulikana ni mkatoliki na akazikwa kikatoliki.

Kina Diamond kuvaa hereni sio uislamu ni sawa na wanaocheza video za x huku wamevaa misalaba huo si ukristo,
Wewe nimekuuliza ni Dini gani.... unaanza kuleta maelezo mengi... Niimekuuliza wewe ni dini gani ili twende kwa reference.


Kinyoa, kusuka, kutinda ni hulka ya mtu binafsi na haiendani na maandiko... Japo maandiko yanataka mtu hawe wa kupendeza na utanashati ambao hauwakeli au kuwasumbua watu wengine kifikra
 
Wasabato walishauza chama tangu walipobadili nembo yao,wamebakia kushika siku tu.
Wanaenda na smartphone siku hizi badala ya kubeba Biblia ni hatari kwa mtu kuangalia ngono wakati wa ibada ukidhani anaangalia vifungu
 
Wewe nimekuuliza ni Dini gani.... unaanza kuleta maelezo mengi... Niimekuuliza wewe ni dini gani ili twende kwa reference.


Kinyoa, kusuka, kutinda ni hulka ya mtu binafsi na haiendani na maandiko... Japo maandiko yanataka mtu hawe wa kupendeza na utanashati ambao hauwakeli au kuwasumbua watu wengine kifikra
Maandiko yanataka Mkristo asifanane na watu wa kidunia kuanzia mavazi, chakula,nk
 
Wewe Dini gani kwanza

Kila Dini ina matatizo yake, ukisema tuanze kushushuana mbona ni kasheshe.

Hao wote ni binadamu kuna kuteleza, pia kwenye maandiko hawajaweka namna ya unyoaji au husukaji... Usilete hukumu ambazo hazipo
Hahaha Huu uzi ningekukosa ningemwambia Melo afute apps 🤣🤣🤣
By the way biblia imeelekza jinsi ya kunyoa na kiwango cha nywele 👏👏
 
Mtu kukataza kunyoa kusuka ua kutinda ni msimamo wake tu... Haina uhusiano na wasabato...

Kusuka hasa rasta wengi wanakataa kwa sababu hawajui nywele zinatoka wapi, au kutinda ni kwa sababu ya kiafya tu kwa sababu pale wanakwangua ngozi uwezi kujua mashine imetumika na kwa nani

Lakini kimaandiko hakuna hayo maelezo... Huo ni msimao wa wahusika tu
Maandiko Yameeleza mkuu
 
Jua kujulikana ni wa dini flani na mtu kuwa na imani ya dini yake. Dini ni imani sio kutambulika tu kwamba una jina la dini flani, wazazi ni dini flani, umezikwa dini flani, n.k.

Mtu anaweza kutambulika ni mkristo ama muislamu lakini ni mshirikina balaa.

Kuna mganga nguli huko Njombe alifariki mwaka jana allitwa "Mwandulami" pia alikuwa na wake nane ila alijulikana ni mkatoliki na akazikwa kikatoliki.

Kina Diamond kuvaa hereni sio uislamu ni sawa na wanaocheza video za x huku wamevaa misalaba huo si ukristo,

Ndio maana kuna siku ya kiama na utaangaliwa matendo yako, sio ulizaliwa dini gani ama ulienda kanisani / msikitini mara ngapi
Mkuu mwambia Kina petro kibao wanatukaba Mtaani huku na kuna kila abubakar na Kina Mohamed mateja kibao na kina Fatuma na kina Mariam (Sana sana Mariam biriani)
micharuko na Malaya kutupwa wakati hayo ni majina ya watakatifu waliobarikiwa kwa mujibu wa Imani za Ibrahimu
 
Back
Top Bottom