Airtel inazidi kutanua soko la Unlimited internet, Vodacom na Tigo wakiendelea kushupaza shingo watastuka soko lishamezwa

Tigo tatizo lao wamekuja na jina gani sijui, jina la ajabu hata sijui ni nn, kuwa na jina zuri linavutia wateja, sijui wameamua kuita kabisa Nyash wameona Tigo sio jina tena
Ili unvyotumia ujisikie raha zaidi kama unavyotumia Nyash
 
Halotel Home Wifi is the best, router bure na vifurushi vyao inaanzia 70k kwa mwezi na speed 20mb/s hicho ndio kifurushi cha chini na 95k kwa speed ya 40mb/s kwa mwezi na hicho kinatosha sana unlimited, Halotel wamekamata Dar sio mchezo
Halotel wana unlimited mkuu?
 
Ok,nataka line hiyo naipataje,infact niko mikoani,ila nataka kutumia line yangu ya kawaida je?
 
Ni kweli wenye router ni wachache ila taratibu watu wameanza kutoka huko. Router zinanunuliwa sana mkuu. Nimeona hili kwa macho yangu...
Zinanunuliwa na wachache sana. Na hao wanaonunua zinawashinda wanarudi tena kwenye mabando ya siku na wiki.

Tatizo mnafikiri Tanzania ni hapo M/City na maduka makubwa zinazouzwa hizo router

Watanzania wengi kwanza hawajui hata router ni nini.

Hili taifa bado lina umasikini mkubwa sana wa kipato cha mtu mmoja mmoja

Kweli Mtanzania wa kawaida atoe 250k au 110k kwa ajili ya intaneti? Tembeeni vijana mjionee uhalisi wa maisha ya Mtanzania
 
Halotel wana unlimited mkuu?


Yes, Viettel au Halotel wanayo Unlimited Home Wifi Internet kali sana, i am using it for a year now, see below test speed na bei zake rafiki sana na ina coverage hadi meter 100 na unlimited bando kwa mwezi na unlimited number of people kujiunga ukiwa home, yaani hata watu 100 mnajiunga

 
Watu wanazinunua sana mkuu na wengi wanaziweka kwenye biashara zao kama saluni za kike na kiume ili wateja wakienda watumie bure ni kama kuvutia wateja, kwenye maduka ya vinjwaji, bar, lodge, hotelini ndogo ndogo, sehemu kibao hata saluni za kawaida mkuu.
Pia watu ambao walikuwa unakuta kila sikua anatumia bundle ya 2500 kwa internet na bado halimtoshi, anaona hiyo ndiyo bora zaidi.
Lakini overall ni asilimia chache ya watanzania, lakini wa tanzania ni zaidi ya milioni 60, hata wakinunua watanzania laki mbili bado kwao ni biashara.
 
mkuu hii ndiyo nitanunua nikihama maana naona ina ping ya chini sana aisee. hata fier ninayotumia haioni ndani kwa screenshot hii
 
Kati ya salon na hotel ndogo 10 hapa Tz ngapi zina router?

Na mpaka sasa walionunua ambao bado wanazitumia ni wangapi?

Nimeona wengi wananunua kwa mkumbo mwisho wa siku zinawashinda. Wengi si watumiaji endelevu

Sikatai wenye mitandao ni sehemu ya biashara ila watumiaji ni wachache sana
 
mkuu hii ndiyo nitanunua nikihama maana naona ina ping ya chini sana aisee. hata fier ninayotumia haioni ndani kwa screenshot hii


Nzuri sana hii, hata ukiwa na Lodges or hotels zako unanunua halotel ya 95k per month kama hii hapa kwangu, wateja wote wanatosheka na haikati kati, very stable speed, sbb ni fiber, yaani fiber speed yake ni uhakika kama US or Europe..!!
 
Kati ya salon na hotel ndogo 10 hapa Tz ngapi zina router?
sasa unaniuliza hili swali unadhani nimefanya research naweza kukupa exact number? Ila mimi kila lodge ninayoenda hapa dar katika harakati za uzinifu nakuta wifi tena ni zile za 25000-35000, napoishi, nikienda sokoni kwenye saluni za kike na kiume kuna wifi, tena waameweka hadi vile vispka. Tunatoa huduma ya kunyoa nywele na mteja atapata free wifi.... Rafk zangu ninaozunguka nao wanatumia hizi router, mimi mwenyewe nimefnga fiber ila nahama soon nitanunua router maana nakohamia hakuna fiber.
Nakubaliana na wewe kuwa si watanzania wengi, ila vinanunulika sana na watu wanavitumia.
Kama DSTV ina wateja 180k na bado ina survive, basi bila shaka wakiwa na wateja 200k nao watasurvive. Kabla ya kufunga wifi, nilienda chukua router pale kibo complex, wakaniambia mzigo umeisha nisubiri.
 
Nzuri sana hii, hata ukiwa na Lodges or hotels zako unanunua halotel ya 95k per month kama hii hapa kwangu, wateja wote wanatosheka na haikati kati, very stable speed, sbb ni fiber, yaani fiber speed yake ni uhakika kama US or Europe..!!
mkuu ni wifi au fiber? kama ni fiber huku nakoishi natmia ya tigo ya speed 20 mbs kwa 55000 sasa nitahama nahamia mapinga hakuna fiber kabisa nilidhani ni router nije niichukue.
 
Ok,nataka line hiyo naipataje,infact niko mikoani,ila nataka kutumia line yangu ya kawaida je?
Nenda kwenye duka la halotel watakusajilia maana laini ya kawaida haikubali. Hata namba zake ni tofauti kabisa, zinaanza na 300 na siyo 062 kama hizi za kawaida...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…