Ajali iliyohusisha Magari Nane, maelezo ya Polisi yanatia shaka

Ajali iliyohusisha Magari Nane, maelezo ya Polisi yanatia shaka

chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa gari no.T.131 dvu how yenye tela no.T.329 dmr kujalibu kulipita gari iliyokuwa mbele yake pasipo kuchukuwa tahadhali (×) dereva amekamatwa yupo mahabusu kituo cha polisi Kabuku kwa ajili ya mahojiano
Polisi si wa kuwamini hata kidogo,
Ukiangalia kwa macho ya kawaida kabisa utaona kwamba Lorry T131 DVU lipo kwenye site yake isipokuwa Basi la Polisi Ashok Leyland ndilo linaonekana lilikuwa likitaka kulipita Basi lingine la Polisi lkn alishindwa kumaliza kwa sababu aidha alikosea timing au ni uzembe ambao polisi wanao kwa kutumia nguvu zaidi kuliko akili!!!

Wakati mwingine Polisi wasijitishe hiz aibu za waziwazi kwa kuihada Umma. naamini Polisi wachache ndio wanaoharibu taswira ya jeshi zima la polisi ni jukumu la viongozi wao kutokufumbia macho maswala kama haya yaliyo waziwazi!!!
 
Basi la Polisi Ashok Leyland ndilo linaonekana lilikuwa likitaka kulipita Basi lingine la Polisi lkn alishindwa kumaliza kwa sababu aidha alikosea timing au ni uzembe ambao polisi wanao kwa kutumia nguvu zaidi kuliko akili!!!
Walikuwa kwenye ligi, kwa mtazamo wangu, jamaa akakomaa ampite jamaa sehemu isiyoruhusiwa, ghafla likatokea lory, jamaa aakrudisha basi kushoto, jamaa yake badala ya kukwepa aingee mtaroni, akakomaa barabarani, matokeo yake huyo kaingi hapo na huyo kamla hapo kwenye shoo
 
Walikuwa kwenye ligi, kwa mtazamo wangu, jamaa akakomaa ampite jamaa sehemu isiyoruhusiwa, ghafla likatokea lory, jamaa aakrudisha basi kushoto, jamaa yake badala ya kukwepa aingee mtaroni, akakomaa barabarani, matokeo yake huyo kaingi hapo na huyo kamla hapo kwenye shoo
Ashok kwa Ashok mweee polisi jamani kweli wanatakiwa walinde tu bank mengine wayaache!!!
 
ndio ujue zile ligi tamu sana sana
images (2).jpeg

Ndugu abiria ligi zimeruhusiwa au?

images (3).jpeg


images (4).jpeg
 
... ndio polisi wa Tanzania; nguzo yao kuu ni UONGO! Kama jambo la wazi hivi wanadanganya, yale ya sirini hali ikoje? Kinachoitwa taarifa za polisi nchi hii sio cha kuamini kabisa!

Bila kuwa na oversight body ya ku-oversee utendaji wa polisi nchi hii, hatutoki. Hii inapaswa kuwa ajenda muhimu ya kisiasa. Wana mandate kubwa sana isiyohojiwa worse enough abuse imevuka mipaka.
ndio polisi wa Tanzania; nguzo yao kuu ni UONGO! Kama jambo la wazi hivi wanadanganya, yale ya sirini hali ikoje? Kinachoitwa taarifa za polisi nchi hii sio cha kuamini kabisa!


Sina mengi ya kusema ila polisi wa tz ni waongo sana
 
Kuna mkanganyo mkubwa:

1: Namba ya tela inayotajwa siyo inayoonekana kwenye picha, labda kuna gari jingine?

2: Mpaka upate namba za magari yote kwa uhakika ndo unaweza kujua ukweli.
Peleka upumbavu wako huko,kusoma hujui hata picha ?
 
Nimejaribu kusoma kwa utulivu kisha nikaangalia picha, naona kama yanapingana na uhalisia, anyway Wajuvi nisaidieni, lory HOwo ame-ovrtake kweli hapo??

Afande taarifa ya ajali:

KAB/TR/ar/16/2021(×)ajali ya magari manane kugongana na kusababisha majeruhi na uharibifu wa magari (×) mnamo tar 14/11/2021 majira ya saa 18:30 huko katika kijiji cha Kwedilomba kata ya Kwedibomba tarafa ya mzundu wilaya ya Handeni mkoa wa Tanga barabara kuu ya Segera-Chalinze gari No.T.131 DVU aina ya HOW yenye tela No.T.329 DMR ikiendeshwa na Saimon S/O kristo @Mwanyila, 36yrs, Mbena, mkazi wa Kibaha Pwani akitokea kabuku kuelekea Chalinze alipokuwa akijalibu kulipita gari la mbele yake mahala pasipo ruhusiwa ndipo ghafla mbele yake kukatokea gari nyingine iliyokuwa ikitokea Chalinze kuelekea kabuku yenye No.Pt.4036 ashok leyland mali ya jeshi la polisi Tanzania likiendeshwa na H.3637 CPL Juma wa chuo cha Polis CCP Kilimanjalo na ndipo dereva wa gari No.Pt.4036 alisimama ghafla ili kuepuka ajali isitokee na ndipo baada ya gari hiyo kusimama ghafla ikatokea gari nyingine kwa nyuma iliyokuwa ikitokea Chalinze kuelekea Kabuku PT.4087 ashok leyland ikiendeshwa na F.7658 CPL John Robert wa makao makuu madogo ya polisi DSM na kugonga kwa nyuma.

Ghafla tena ikaja gari nyingine kwa nyuma No.Pt.4097 ashok leyland ikiendeshwa na F.5889 CPL Kigiri wa Polisi makao makuu madogo ya Polisi DSM na kusimama ghafla PT.4087 ashok leyland na kusababisha gari No. PT.2370 Isuzu bus ikiendeshwa na g.6123 CPL abel wa chuo cha polisi Kidatu na kugonga ubavuni gari no.Pt.4087 ashok leyland pia ikatokea tena gari No.T.573 AYR toyota corolla ikiendeshwa na Amin S/O UR Rasul@Khan, 60yrs, mkazi wa Tanga na kusimama ghafla baada ya kuona ajali na kusababisha gari no.SU 44275 gx v8 mali ya TANESCO DSM ikiendeshwa na Tuma S/O Hassan lean na kuigonga kwa nyuma gari hiyo no.T.573 AYR Toyota corolla pia ikasababisha gari nyingine yenye no T.773 CND Toyota hilux kuigonga kwa nyuma gari hiyo no.Su.44275 GXV8 TANESCO na kusababisha majeruhi kwa watu 16 ambao ni 1.D.8420 s/SGT John Mwakipesile 2.Pf.18891 insp sister 3.G.6123 CPL Abel ambao wote watatu wamepelekwa hospitali ya rufaa Bombo kwa matibabu

Na 4.Pf.17534 insp Rashida 5.Pf.18326 insp Nyalugembe 6.Pf.17896 insp Gonga 7.Pf.18202 insp Said 8.Pf.17166 insp Ally juakal 9.Pf.17899 insp Sanya 10.Pf.18445 insp pangane 11.Pf.17691 insp Peter 12.Pf.18719 insp Ohusso 13.Pf.17321 insp Ilomo 14.Pf.18616 insp Anthony 15.Pf.17674 insp Zongho 16.H.1659 pc gift (×) majeruhi wote wameumia sehemu mbalimbali za mwili na kutibiwa kituo cha afya Kabuku na kuruhusiwa (×) chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa gari no.T.131 dvu how yenye tela no.T.329 dmr kujalibu kulipita gari iliyokuwa mbele yake pasipo kuchukuwa tahadhali (×) dereva amekamatwa yupo mahabusu kituo cha polisi Kabuku kwa ajili ya mahojiano (×) eneo la tukio limekaguliwa na acp. Sofia jongo rpc Tanga akisaidiwa na ssp leopord .N. Fungu rto tanga , sp. Elias Rwambano ocs Kabuku, a/insp Rajabu kaimu DTO Handeni pamoja na g.3191 cpl Mussa ambaye ndiye amechora na kupima eneo la tukio (×)///////////

Taarifa kwa maandishi inafuata //////////


Toka rto tanga ///////////

Picha tu, zinaeleza kila kitu. Lorry liko upande wake, tena karibu linaacha njia, basi la polisi limechukua nafasi ya lori linalojaribu kulikwepa Hilo basi la kwanza. Kama kawaida yao, inaonesha polisi walikuwa mwendo Kasi, wakifuatana Kwa karibu, wakitanua pia ndio maana wameishia kugongana Kwa nyuma. Magari mengine yote ni wahanga wa ubabe wa hii laana inayoitwa polisi.
 
Kama ni kweli RTO, anaweza kutoa maelezo hayo, huku picha zinaonyesha basi mbili za PT zikiwa sambamba kama parallel lines za kwenye maumbo ya hesabu za darasa la 5, basi niungane na James Mbatia, kulia mama Tanzania.

Everyday is Saturday................................😎
 
Kuna mkanganyo mkubwa:

1: Namba ya tela inayotajwa siyo inayoonekana kwenye picha, labda kuna gari jingine?

2: Mpaka upate namba za magari yote kwa uhakika ndo unaweza kujua ukweli.
Na sio No tu na hata hicho kichwa cha lorry ni FAW na sio HOWO me naona watu wanatiririka tuu au kuna picha nyingine mimi sijaziona
 
Dereva wa Lori alijaribu kurudi kwenye njia yake baada ya kuona uso kwa uso lakini bahati mbaya horse tu ndio ilifanikiwa, tela ndio ikasababisha ajali
ukitizama kwa makini kwenye lami hiyo picha ya mwisho utaona jinsi tairi za kichwa zilivyoacha alama kwenye lami kutoka upande mmoja kwenda mwingine
Ifahamike pia picha huwa inajigeuza hapo ndio wengi mnajichanganya kupata uelekeo
Inawezekana wewe ni polisi au akili zako hazipo timamu.
 
Back
Top Bottom