Tetesi: Ajali Lucky Vincent School: Uzembe, Tamaa, Ubadhirifu na Kutokujali Usalama wa Wanafunzi

Tetesi: Ajali Lucky Vincent School: Uzembe, Tamaa, Ubadhirifu na Kutokujali Usalama wa Wanafunzi

Sawa Tuache mambo ya magari. KULIKUWA NA UMUHIMU GANI KWA WANAFUNZI KUSAFIRI KWA AJILI YA KWENDA KUFANYA JOINT EXAMS. WANGEWEZA KUTUNGA MTIHANI WAPAMOJA NA WATOTO WAKAFANYA BILA KUSAFIRI.
Umetoa hoja nzuri sana.
 
Kwaajili ya kawaida kama wanafunzi wa 4/6 wanakaa wawili wawili kwenye coaster iweje darasa la nne Na Saba wakae mmoja moja kweli haiwezekani labda shule kama briburn au St Jude kidogo
 
Hakuna shetani wala chunusi wala yunusi ukweli ajali nyingi no uzembe Na madereva wasiyo sifa tafuta riport zote mpaka sasa dereva hajulikani jina lake kamili hajatajwa popote anaitwa nan ingekuwa umeajiliwa zi jina lingetajwa mbona walimu Na wanafunzi wametajwa?
 
Taarifa ya habari ni kwamba mwenye shule amesema basi

Ilibeba watu 38
Wanafunzi 29 walikufa papo hapo pamoja na walimu 2 na dereva.

Mwanafunzi mmoja amefariki hospitali.

Hivyo wamejeruhiwa wanafunzi 5.

Hivi hilo basi linatakiwa kubeba abiria wangapi?
Tuwe tu wakweli hata nyumbani kwako kwenye sofa ya watu wawili watoto wako hukaa wangapi...
 
Mkuu siamini kwenye kuzidisha uzito.. Hao watoto ata wangepanda mia hawawez kuzidisha uzito kiasi cha mfumo wa breki kuzidiwa.. Labda unambie maintainance au ispection haikufanyika plus uzembe au kuchoka kwa huyo dereva.. Hatujui usiku wake alikua anafanya kabla hajaanza safar..
 
Duhh, kazi kweli kweli. Hivi hiyo bara bara ya mto wa mbu Karatu ilivyo sasa utalinganisha na ilivyokua miaka ya 1990s? Bara bara hiyo ina shida gani mkuu? Umewahi kuona barabara zenye shida? Au unadhani bara bara zote zitakua kama Ubungo - Posta? Uzembe wa dereva na uchakavu wa chombo ndo vinabeba asilimia kubwa sana katika ajali mkuu.
Lami tu ndio tofauti yake na 1990s Barbara zetu ni nyembamba sana na za hatari mno ukikosea kidogo umekwisha.

Toka Barabara ya Chalinze Morogoro ipanunilwe fuatilia takwimu ajali zimepungua kwa kiasi cha ajabu
 
Mradi ajari imetokea kila mtu atasema lake kumtafutia fulani makosa. Ukweli unabaki palepale, mauti ni haki, usipokufa leo utakufa kesho na mauti hayana umri!
Vifo vya hawa wanafunzi vimekuwa ni vya huzuni kubwa kwa wazazi na Taifa kwa ujumla, lkn hatuwezi kubadili ukweli kuwa hawa hatunao tena. Kujenga dhana wakati huu si jambo zuri, ni vyema tukasubiri mamlaka zinazohusika zikatoa taarifa rasmi. Ajari haina kinga. Nimesafiri sana na mabasi na malori lkn sijapata ajari hata mara moja, si kwa ujanja wangu bali ni kwa neema za Mwenyezi MUNGU. Hii inanifanya niamini kuwa Kila mtu ana siku yake ya kufa na ikifika utakufa tu, iwe kwa ajali au kifo cha ghafla hata kama upo kitandani kwako mauti yatakufuata. Hakuna mauti yanakosaga sababu, ni hulka ya mwanadamu kutafuta mahala pa kurusha lawama zake mauti yanapotokea.
 
Wazazi poleni kwa msiba huu uliowapata watoto wetu wapendwa wa Lucky Vicent na walimu wao! Hakika ni majonzi makubwa sana! Lakini yafaa tutafakari kwa kina kwanini janga kama hili liwafike watoto hawa, tumaini la maisha yetu! Maswali ni mengi, na kwa kweli yana hitaji majibu ya kina.

hatua za kuwawajibisha wahusika wote ili kuokoa maisha ya watoto wasio na hatia.

Well said, poor maintenance ndiyo tatizo kubwa la magari yanayo beba wanafunzi, majority ya magari haya yemechoka sana, wanacho fanya ni kuyapiga rangi basi - hata akili za kuchukua tahadhali wanapo panga safari ndefu kwamba wakague brake system nzima, power steering system na kibukwa zaidi condition za matairi, si ajabu ukakuta tairi lilipasuka wakati dereva akiwa kwenye mwendo kasi - vyeti feiki siyo maofisini tu hata madereva wengi wana liseni za kughushi.

Serikali inapaswa kukazania annual motor vehicle inspection by an Authorised Garages, tuwaige wenzetu wa Ulaya - gari aliruhusiwi kuwa barabarani kama alina cheti cha M.O.T - wako serious kwa saula hili.
 
Lami tu ndio tofauti yake na 1990s Barbara zetu ni nyembamba sana na za hatari mno ukikosea kidogo umekwisha.

Toka Barabara ya Chalinze Morogoro ipanunilwe fuatilia takwimu ajali zimepungua kwa kiasi cha ajabu
Ndiyo maana tunajadili ili tupunguze huko kukosea kidogo. Wembamba wa barabara ingekua hoja kama ajali ingekua ni ya kugongana. Pia bara bara zinatofautiana viwango kulingana na umuhimu wake. Mfano hiyo ya Chalinze - Morogoro ambayo ni TANZAM Highway ( Dar - Tunduma) ni T1, Chalinze - Arusha ni T2, Morogoro - Mwanza ni T3 nk. Utakuta hiyo Mto wa mbu - Karatu labda ni T30, sasa haiwezi kuwa na upana na viwango vingine kama bara bara zingine, lakini kwa ujumla ina lami na ni nzuri kwa category yake.
 
Ndiyo maana tunajadili ili tupunguze huko kukosea kidogo. Wembamba wa barabara ingekua hoja kama ajali ingekua ni ya kugongana. Pia bara bara zinatofautiana viwango kulingana na umuhimu wake. Mfano hiyo ya Chalinze - Morogoro ambayo ni TANZAM Highway ( Dar - Tunduma) ni T1, Chalinze - Arusha ni T2, Morogoro - Mwanza ni T3 nk. Utakuta hiyo Mto wa mbu - Karatu labda ni T30, sasa haiwezi kuwa na upana na viwango vingine kama bara bara zingine, lakini kwa ujumla ina lami na ni nzuri kwa category yake.
Gari sio Train useme litakaa kwenye line mwanzo mwisho lazima upewe upana wa kuweza kurudi barabarani ukiteleza
 
kumbuka tangu ndalichako aseme waliosoma english medium wakifika chuo kikuu hawapati mkopo watoto hawapelekwi tena shule hizo
Wewweee..... Embu wacha uongoo.. Duhh
 
Kwanza kabisa nianze kwa kutoa pole kwa Familia zote zilizokumbwa na huu Msiba mzito na mkubwa kabisa, pili nitoe pole zangu za dhati kabisa kwa Wana Arusha wote bila kumsahau Mkuu wao wa Mkoa Comrade Mrisho Gambo na mwisho kwa Watanzania wote kwa janga hilo lililotokea hapa nchini Kwetu Tanzania na tumuombe Mwenyezi Mungu azipokee roho na Watoto wetu wote, Walimu na Dereva wa gari lile la Shule ya Lucky Vicent aziweke mahala pema peponi Amin / Inshaallah.

Kwa mtazamo wangu binafsi naweza nikapingana na Mtoa mada juu ya baadhi ya lawama zake alizoziweka hapo juu japo nikiri wazi pia kuwa kuna mahala pengine amesema mambo ya wazi na ya kweli kabisa ambayo Mamlaka husika zinapaswa kuyachukua na kuyafanyia Kazi.

Najua kuwa wengi wetu tunaweza kumtupia lawama yule Dereva wa lile Basi ila niseme tu wazi kuwa ile ajali ya jana imetokea kwa BAHATI MBAYA sana na haina cha kumlaumu. Ukiona ajali yoyote ile inayohusisha Mabasi ya Abiria halafu hadi Dereva na zingine Dereva na Utingo / Kondakta wake nao ' wamekufa ' basi jua ya kwamba hiyo Gari hata Yeye ( Dereva ) ilimshinda na siyo ya kawaida.

Inasemekana kwamba sababu kubwa hadi iliyopelekea hiyo ajali ni kwamba Basi lilikuwa katika Spidi kiasi na siyo kubwa kama ambavyo tunaanza kupeana ' Sumu ' mitandaoni na kwamba Gari lilipofika katika huo Mlima kulitokea ' Ukungu ' mkubwa mno wa ghafla hali ambayo ulimchanganya Dereva kiasi cha kutaka kupunguza kidogo Spidi ili aende kwa ' tahadhari ' ndipo Gari lile ( Basi ) likaanza ' kuyumba ' huku likisaidiwa na ' utelezi ' uliokuwepo pale na ambao ulitokana na hali ya ' unyevu unyevu ' hali ambayo ilifanya Gari lile likose mwelekeo na kuanza kuyumba yumba hadi likaingia ' Korongoni ' pale na kusababisha yale ' mauti ' ya kutukuka ya Watoto wetu wapendwa, Walimu wao na Dereva.

Nadhani kwa maoni yangu kama tukisema tutupe lawama mahala fulani basi itapendeza sana kama tukizipeleka hizi lawama zetu kubwa kwa Mamlaka husika hasa Tanroads ya Mkoa wa Arusha na hata Serikali vile vile kwa kuweza ' kuzembea ' kuweka angalau ' Vizuizi ' vya pembeni ( Kingo ) ili kuweza kuepusha ' Ajali ' kama hii kwani hata ukiangalia tu ile sehemu ilipotokea ajali utaona ni barabara nzuri tu ila hapo katika bonde hakuna ' Kingo ' zozote hivyo ni rahisi mno kwa Gari lolote kutumbukia humo pindi pakitokea ' hitilafu ' yoyote.

Mwisho kabisa nimalizie tu kwa kusema kuwa kuanza kuwalaumu Walimu wa Shule au Mmiliki wa Shule au sijui Madereva wa wale Wanafunzi hakutosaidia kitu kwani wao kama wao walitimiza wajibu wao na bahati nzuri ni kwamba kumbe hii siyo mara ya Kwanza hao Watoto wanaenda kufanya hiyo mitihani ya ujirani mwema na kwamba ni mara ya tatu isipokuwa tu sisi kama Wanadamu tutambue kuwa kuna bahati mbaya maishani na siamini kabisa kama Walimu au Mmiliki wa Shule hiyo ya Lucky Vicent alipanga hili kutokea au hata amelifurahia.

Ni ajali tu ya bahati mbaya hivyo kikubwa tu kama Wanadamu kuanzia sasa tunatakiwa tuchukue tahadhari siyo tu hapo Karatu bali hata maeneo mengine ambapo tunajua kuna miundo mbinu mibovu au hali ya barabara siyo nzuri pindi pakiwa na mvua na hata Wahusika hasa TANROADS nao wanapashwa kuhakikisha kuwa sehemu zote hatarishi za barabara Kuu za Mabasi usalama wake hasa wa Kingo za bondeni umezingatiwa ili basi Tanzania isije ikapata tena ' Mkasa ' mkubwa kama huu.

Poleni sana Watanzania wote na GENTAMYCINE nipo nanyi katika ' majonzi ' katika kipindi hiki kigumu kabisa cha huu Msiba kikubwa tuwape ushirikiano mkubwa na wa hali na mali ' Wafiwa ' wote, tuwafariji na tuwaombee Mwenyezi Mungu awape moyo wa ' subira / uvumilivu ' mpaka pale tutakapowapumzisha ' Wapendwa ' wetu katika Nyumba zao za Milele na wala hakuna haja ya kuanza kuichukia Shule ya Lucky Vicent au kumchukia sijui Mwalimu Mkuu au Mmiliki wake kwani hili jambo lingeweza kutokea mahala popote pale na hata kumtokea Mtu yoyote yule.

Muinto Obrigado nyote na tupo pamoja.
Story tu... Same same...
 
Who is the real enemy!!! The devil??? Serious??? Ndiyo maana nchi hii haiendelei na haitaendelea kwa sababu wapiga kura na wapigiwa kura wote ni wale wale.
Wewe pia ni shetani... Maana naona unamtetea sana.
 
Back
Top Bottom