Ajali Mbaya Goba Rd Masana, Magari (4) na Bodaboda Yagongana USO Kwa Uso!. Congestion ya Balaa!. Thanks God No Casualty, No Fatality!

Ajali Mbaya Goba Rd Masana, Magari (4) na Bodaboda Yagongana USO Kwa Uso!. Congestion ya Balaa!. Thanks God No Casualty, No Fatality!

Nipo nimepanga ubazi mzima jirani na Masana. Wewe ni wa pande zipi?.
P
How do u explain to ur children kuwa katika umri huo bado unaishi kwenye nyumba ya kupanga?
Nenda Kisarawe, kamata hata eneo la laki tano ujenge chumba na sebule.
Kisarawe ni karibu sana na Posta kuliko Bunju, Mbweni, Mabwepande na Chanika.
Pia kuna hali nzuri ya hewa.
 
How do u explain to ur children kuwa katika umri huo bado unaishi kwenye nyumba ya kupanga?
Nenda Kisarawe, kamata hata eneo la laki tano ujenge chumba na sebule.
Kisarawe ni karibu sana na Posta kuliko Bunju, Mbweni, Mabwepande na Chanika.
Pia kuna hali nzuri ya hewa.
Na wewe unaamini kweli alichoandika? anyway, kukaa nyumba ya kupanga mwisho ni umri gani?
 
How do u explain to ur children kuwa katika umri huo bado unaishi kwenye nyumba ya kupanga?
You don't need to explain anything to my kids, kwasababu hapo ndipo walipozaliwa, hayo ndio maisha yao. Mtoto ukizaliwa kwenye kaya masikini, utathubutu kuwauliza wazazi wako sababu ya umasikini wao, au utasoma kwa bidii ili usiishi maisha ya shida na dhiki kama ya wazazi wako?. Ikitokea ntu ni masikini, you don't have to explain anything to anybody kuhusu umasikini wako!.
Nenda Kisarawe, kamata hata eneo la laki tano ujenge chumba na sebule.
Kisarawe ni karibu sana na Posta kuliko Bunju, Mbweni, Mabwepande na Chanika.
Pia kuna hali nzuri ya hewa.
Nimepokea ushauri, soon nitatimiza 60 years, hivyo nitatumia fedha zangu za mafao, kununua ardhi Kisarawe, nihamie na kuachana na nyumba za kupanga.

Asante kwa ushauri
P
 
Wanabodi

Kumetokea ajali mbaya ya magari manne na boda boda, yamegongana huku mimi nikishuhudia huku nikiwa viti virefu hapa sebuleni kwangu Highland, mkabala na Masana Hospital.

Sijaweza kujua chanzo, ila gari moja ilikuwa inatokea Goba, Kwa spidi kali, mara uso kwa uso na Bodaboda, ikaikwepa kwa kuipiga ubavuni na katika kukwepa, ikaiparamia gari ya kwanza, ikaipiga pasi ya haja, ikaigonga gari gari ya pili na kutua uso kwa uso na gari ya tatu ikafunua bonnet!.

Mwenye Bodaboda akatupwa mtaroni, na kuparamia magari mengine mawili na kulivaa uso kwa uso gari la 3!.

Mawili kati ya magari manne yaliyoparamiwa, yanaendeshwa na madeva wadada, mmoja anayeendesha Subaru Impreza mpya, anawaka Balaa!.

Kilichosabisha congestion ya ajabu sio hayo magari manne yaliyogongana bali break down 4 zinazogombania tenda ya kuyavuta!. Magari yote 4 yanaweza kutembea hivyo sijui hizi break down zinazotuzibia njia zinagombea tenda gani!.

Thanks God, there is neither casualties nor fatalities!.
Mungu ni mwema!.
Paskali.
Nipo hapa kwa mwamposa kawe nakusubir
 
Back
Top Bottom