Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

-Ubora wa magari yanayoletwa na hali ya barabara zetu,kuna walakini.Watengenezaji wanajali faida yao,vifo vyetu haviwahusu,bila kutuuzia mbuzi kwenye junia,kazi kwao haziendi.Wenye mabasi nao,wanachotafuta ni pesa tu.

-Upande wa madereva,walio wengi wana leseni za kununua,ilimradi anaweza kubadili gia.Pamoja na kwamba ajali haiepukiki,uzembe unahusika kwa asilimia kubwa,lakini wazee na wanawake ndo wanaofaa kuendesha magari ya abilia.Lakini kwa kuwa Boss anataka trip nyingi,ana yake.Ajali lazima hapo.

Speed limit ya 80km/h kwa kutumia Speed Governor inatosha,ila swala la kupaki usiku liishe,magari yatembee masaa 24. Waliofiwa ndo wanaojua uchungu wa kupoteza wanafamilia,ambaye hajawahi atajiongelea tu.

-Kuwepo ukaguzi endelevu wa magari,matengenezo yawepo,hizo buku buku za barabarani ziishe,kosa la mwenye gari,asihusike dereva,kosa la dereva asihusike mwenye gari
 
Mie nashauri vyuo vya udereva virudishwe NACTEA kwa sasa vipo chini ya polisi ambao wana uwezo wa kusimamia sheria na sio kuendesha mafunzo. Na leseni zitolewe na NECTA badala ya kutolewa na TRA ambao ujuzi wao ni kukusanya mapato na sio kutathimini weledi.

Kama polisi wanahitaji kusimamia mafunzo ya udereva basi madereva wapelekwe ccp moshi
 
mkuu huweziamini nipo kwenye basi ndio nato mizani ya dikese nimekutana na ajali ya gari sasa hivi,ukweli bora ya maradhi kuliko hizi ajali zinazotukuta sisi watanzania.gari iliyopata ajali ni toyota colora.mungu tusaidie hata trafi hakuna wamekaa barabarani wanachanga hela ya mboga tu.innakera.
jamani pamoja na picha zote hivi bado hamja gundua tatizo???, ni nchi gani Highway ipo kama hizi zetu ambapo gari zinakutana? vibarabara vyembamba gari zinapishana utafikiri bado tupo kwenye 60s? kwa wenzetu magari yanayoenda upande mmoja haya kutani na yanayorudi! hivi hatuoni kwamba design ya bara bara zetu imepitwa na wakati? kwa mfano bara bara ya Dodoma hadi Babati ni pana ya kutosha kutenganisha kila upande bila gharama yoyote na magari mawili yaende kila upande bila matatizo lakini sijui wataalam wetu wamefungwa na nini kila siku masheria mara eti usimame kwenye zebra na upuuzi kibao! jengeni bara bara za kisasa tuache blah blah! Highway iwe highway sio mnabomolea watu nyumba halafu mje na design za kizamani mambo yatakua yale yale! hata kama nje hatuendi uki google "Highway" utapata majibu!
 
City Boy maeneo ya Igunga Tabora nasikia imechinja watu wengi sana 12+ .
ninachojiuliza mpaka sasa wasiojulikana wameua wangapi? na madereva wameua wangapi? nani kaua watu wengi zaidi?

Kwanini hatulioni hili zimwi la madereva wadhembe wakifanya kazi bega kwa bega na miundombinu mibovu?

badala ya ndege, elimu bure, maji na bajeti kubwa ya dawa kwanini tusihakikishe tunapata barabara oneway za mikoani namaanisha gari zinazokwenda zitumie barabara yake na za kurudi barabara yake naamini tutapunguza zaidi ya nusu ya ajari hizi.

ama kwa hakika vifo vitokanavyo na ajari vinahitaji waraka wa maaskofu.
 
Panua barabara ...ziwe at least mbili huku na mbili upande wa pili. Kuwe na ukaguzi wa magari makubwa haswa yanayofanya safari ndefu. Mfano yakaguliwe kila miezi mitatu (matairi n.k) na kupuwe cheti cha kupasi ukaguzi na hii iwe inahakikiwa kwenye vituo vya mizani...kwa kuangalia cheti na hali ya gari.

Leseni za magari makubwa ziwe ngumu kupata ....kwa sasa zipo kama pipi
 
Matukio ya ajali za kutisha barabarani zenye kupoteza roho nyingi zisizo na hatia yamekuwa yakija na kwenda. Kila tukio limekuwa likija na reactions tofauti tokea kwa mamlaka ambapo aghalabu ufumbuzi wa kudumu umekuwa hauonekani kuwa mahali popote karibuni.

Zimetokea ajali nyingi mbaya, kumbuka Majinja express, lukuki za city boy express, kigoma karibuni kulikuwa na ya kuonga train, kumbuka wale watoto wa shule arusha nk nk.

Ya Mbeya ya hivi karibuni imepelekea mabadiliko ya waziri wizara ya mambo ya ndani na wakuu kadhaa Polisi Mbeya kushushwa vyeo. Kabla hata hakujatulia, Mbeya huko huko tena, jana watu kadhaa wamefariki kwenye ajali ya lorry na magari madogo.

Ni wazi kuwa kwa mwendelezo wa approach zetu hizi zisizo angalia kwa undani sababu za haya kuendelea kutokea, basi hata sasa itakuwa ni suala la muda tu kusubiria ajali na vifo vingine na vingine, vingine na vingine, nk.

Kwa tafakari ya kawaida tu, haichukui muda kuona kuwa, ni aidha kwa makusudi au kutofahamu kuwa hatua sahihi hazichukuliwi. Kwa bahati mbaya sana kwa kuchukua hatua sahihi pana ulaji mkubwa wa watu fulani utaathirika.

Mzizi mkuu wa vyanzo vya ajali upo katika RUSHWA. Baadhi ya watu waliopo katika nafasi za kuweza kutupishilia mbali na ajali hizi za kila mara zenye kugharimu maisha yetu na kuwa ni suala la muda tu, ati kwa maslahi yao maovu, hawanayo nia wala utashi wa kuliongelea hili.

Jiulize ni nchi gani hapa duniani ati baadhi ya magari katika sehemu ipi ya barabara (you name it) yanaruhusiwa kutembea kwa mwendo kasi wowote pasipokuwa na limit kabisa?! Ati kuwa so long as hakuna restriction ya 50km/h then mwendo kasi ni discretion ya dereva husika?! Ama kweli hili ni katika Tanzania yetu peke yake na tena labda hii ya siku hizi. Jamani, hivi tumerogwa?

Mbaya zaidi magari ya wasimamia Sheria hizi zilizo fyongo namna hii wakiwamo Polisi, wa huko mahakamani, na hawa wenye kupeperusha bendera zao Fulani Fulani hata hizo 50km/h kwa saa haziwahusu. Hii ikiwa ni wao katika capacities zao kama taasisi na hata wao kama watu binafsi. Tafsiri kamili ya shamba la Bibi!

Kwa mtaji huu tutapona kweli humu barabarani? Si kweli kuwa rambirambi kisa ajali ni suala la muda tu? Haipo haja ya kuchoka kutuma rambirambi bali ni vyema nadhani kujiandaa kwa nyingi nyingine and very soon.

Katika hili pana mapato tena very lucrative yatokanayo na RUSHWA yenye mtizamo wa kuona mbali sana. In disguise serikali inafanywa kuona inapata inayodhani kuwa ni mapato halali kwa ajali ya maendeleo, kumbe nyuma ya pazia wanufaika wakuu tena ni binafsi ambao pia hata ndiyo wao wangetegemewa kushauri vilivyo wakiendelea kujineemesha wao na familia zao.

Hivi ni kwa nini askari wa usalama barabarani katika zao ngazi zote maisha yao hayaendani katu na mishahara yao rasmi? Kwa nini kuhamishiwa usalama barabarani huonekana ni promotion na kutolewa huko huwa kama demotion?

Chonde chonde kwa tamaa za hawa jamaa pasipo kuwa na jitihada za kuumong'onyoa huu mzizi wao mkuu wa RUSHWA walipojifichia, tutaendelea kulipa faini zisizo kuwa na tija yoyote, huku tukiendelea kuwaneemesha watu hawa wasiokuwa.na chembe ya huruma tukisubiria zamu zetu za kufa barabarani.

Tumelaaniwa na nani siye, hatuwezi hata kuona tofauti katika Sheria zetu barabarani hata kwa kulinganisha na majirani zetu basi, kama huko walikoendelea ni mbali?
 
Kuwa makini, mwendokasi ni sehemu ndogo sana ya kusababisha ajali, inaonekana wenye magari wanakukera sana. Ajali nyingi za sasa ni sababu ya miundombinu mibovu (barabara) ila kwa kuwa serikali inahusika hawataki kuliona hili. Sababu nyingine ni ubovu wa magari...hapa ndio kuna rushwa ya ukaguzi. Na sababu ya tatu ni rushwa katika upatikanaji wa leseni hapa pia Polisi na TRA wanahusika
 
ajali zinasababishwa na vitu kama vifuatavyo
1. mwendo kasi
2. uchakavu wa gari, hapa ni pamoja na kutofanyia gari service
3. ubovu wa barabara
4. uchovu kwa dereva
5. ulevi
6. ukosefu wa alama barabarani

ila kwa sasa watu wengi wanajiyahidi kwenye spidi, wanaenda spidi iliyo poa, ila sasa barabara zetu ni mbovu zina mashimo mfano barabara ya dar-lindi, ila tunashukuru serikali inaikarabati
 
Kuwa makini, mwendokasi ni sehemu ndogo sana ya kusababisha ajali, inaonekana wenye magari wanakukera sana. Ajali nyingi za sasa ni sababu ya miundombinu mibovu (barabara) ila kwa kuwa serikali inahusika hawataki kuliona hili. Sababu nyingine ni ubovu wa magari...hapa ndio kuna rushwa ya ukaguzi. Na sababu ya tatu ni rushwa katika upatikanaji wa leseni hapa pia Polisi na TRA wanahusika

Mkuu wenye magari hawanikeri. Tafadhari nisome kwa makini. Nina tatizo na RUSHWA. Pana RUSHWA sana penye mwendo kasi na pia zaidi ya 80 per cent ajali kwa takwimu zao polisi sababu za ajali ni mwendokasi.

Sioni ni sahihi kuwepo barabarani magari yasiyokuwa na restriction katika speed. Kwa nini mabasi yawe limited speed lakini si mengine?

Ajali zitaendelea kuwepo kwa sababu kwa human nature restriction kwako ni sawa lakini si kwangu. Ndiyo maana wale wasimamia Sheria hata 50km/h haziwahusu.

Siku sote tukiwa sawa mbele ya Sheria hizi tutakuwa na Sheria muafaka kwa ajili yetu sote na si kwa kundi fulani tu na hapo ndipo utii bila shuruti utawezekana.
 
ajali zinasababishwa na vitu kama vifuatavyo
1. mwendo kasi
2. uchakavu wa gari, hapa ni pamoja na kutofanyia gari service
3. ubovu wa barabara
4. uchovu kwa dereva
5. ulevi
6. ukosefu wa alama barabarani

ila kwa sasa watu wengi wanajiyahidi kwenye spidi, wanaenda spidi iliyo poa, ila sasa barabara zetu ni mbovu zina mashimo mfano barabara ya dar-lindi, ila tunashukuru serikali inaikarabati

Mkuu katika visababishi hivyo vya ajali vinatofautiswa na % ya prevalence.

Katika list uliyotoa lion's share - zaidi ya 80% ajali zaletwa na mwendokasi uliopitiliza.

Kisichoongelewa hapa ni unachoona exemption ya makundi fulani fulani katika udhibiti mwendo. Inahitajika jitihada ya ziada kuona hii actually ni ni divide and rule ya kujiwekea na kufanikisha kuwapo kwa RUSHWA kubwa kubwa tokea kwa samaki wakubwa kwa maslahi mapana ya wala RUSHWA hawa.

Wajua katika ajali yoyote ndogo au kubwa vehicle inspector lazima ale vilivyo?

Ni kwa malengo yao hayo ya mbali wamefanikiwa sana kutufunga midomo kudhani kuwa twanufaika na hizi unlimited speed barabarani kwa kuwa na private vehicles kumbe in actual fact si kwa manufaa yetu.

Hili la unlimited speed barabarani (mark my words) halipo duniani labda kwa Tanzania hii tu ya viwanda vya cherehani.
 
Mkuu wenye magari hawanikeri. Tafadhari nisome kwa makini. Nina tatizo na RUSHWA. Pana RUSHWA sana penye mwendo kasi na pia zaidi ya 80 per cent ajali kwa takwimu zao polisi sababu za ajali ni mwendokasi.

Sioni ni sahihi kuwepo barabarani magari yasiyokuwa na restriction katika speed. Kwa nini mabasi yawe limited speed lakini si mengine?

Ajali zitaendelea kuwepo kwa sababu kwa human nature restriction kwako ni sawa lakini si kwangu. Ndiyo maana wale wasimamia Sheria hata 50km/h haziwahusu.

Siku sote tukiwa sawa mbele ya Sheria hizi tutakuwa na Sheria muafaka kwa ajili yetu sote na si kwa kundi fulani tu na hapo ndipo utii bila shuruti utawezekana.
Issue ya ajali ni bara bara zisizokidhi viwango, magari yasiyokidhi vigezo vya usalama na rushwa katika uhakiki na utoaji wa leseni. Magari mengi nchini maximum speed ya manufacturer ni 180km/hr ambayo ni ya kawaida.
 
Mkuu katika visababishi hivyo vya ajali vinatofautiswa na % ya prevalence.

Katika list uliyotoa lion's share - zaidi ya 80% ajali zaletwa na mwendokasi uliopitiliza.

Kisichoongelewa hapa ni unachoona exemption ya makundi fulani fulani katika udhibiti mwendo. Inahitajika jitihada ya ziada kuona hii actually ni ni divide and rule ya kujiwekea na kufanikisha kuwapo kwa RUSHWA makubwa makubwa tokea kwa samaki wakubwa kwa maslahi mapana ya wala RUSHWA hawa.

Wajua katika ajali yoyote ndogo au kubwa vehicle inspector lazima ale vilivyo?

Ni kwa malengo yao hayo ya mbali wamefanikiwa sana kutufunga midomo kudhani kuwa twanufaika na hizi unlimited speed barabarani kwa kuwa na private vehicles kumbe in actual fact si kwa manufaa yetu.

Hili la unlimited speed barabarani (mark my words) halipo duniani labda kwa Tanzania hii tu ya viwanda vya cherehani.
Naomba uniambie mwendokasi uliopitiza ni speed ipi? Pia hata hizo takwimu sio scientific ni hear say baada ya ajali kutokea. Wakiulizwa watoe scientific evidance huo mwendokasi sijui kama wanazo
 
Naomba uniambie mwendokasi uliopitiza ni speed ipi? Pia hata hizo takwimu sio scientific ni hear say baada ya ajali kutokea. Wakiulizwa watoe scientific evidance huo mwendokasi sijui kama wanazo

Mkuu kwa kiingereza mwendokasi uliopitiliza uko phrased kama ,'over speed' hili likiwa na maana ya ya kuwa mwendo juu ya kiwango (limit) uliowekwa na mtengeneza barabara au mamlaka husika. Limit hizi ni mambo ya kiufundi hutegemea mambo mengi mfano idadi ya watumiaji wengine wa barabara, upana wa barabara, hali ya corner nk.

Jambo la uhakika haipo barabara isiyokuwa na speed Limit. Halipo lolote la kuyapa magari yoyote limitless speed incentive kwa sababu yoyote Ile ni Jambo ovu na linatuweka sote mashakani tukisubiria kudra pekee za mwenyezi Mungu kuwapo hai barabarani.
 
Mkuu katika visababishi hivyo vya ajali vinatofautiswa na % ya prevalence.

Katika list uliyotoa lion's share - zaidi ya 80% ajali zaletwa na mwendokasi uliopitiliza.

Kisichoongelewa hapa ni unachoona exemption ya makundi fulani fulani katika udhibiti mwendo. Inahitajika jitihada ya ziada kuona hii actually ni ni divide and rule ya kujiwekea na kufanikisha kuwapo kwa RUSHWA makubwa makubwa tokea kwa samaki wakubwa kwa maslahi mapana ya wala RUSHWA hawa.

Wajua katika ajali yoyote ndogo au kubwa vehicle inspector lazima ale vilivyo?

Ni kwa malengo yao hayo ya mbali wamefanikiwa sana kutufunga midomo kudhani kuwa twanufaika na hizi unlimited speed barabarani kwa kuwa na private vehicles kumbe in actual fact si kwa manufaa yetu.

Hili la unlimited speed barabarani (mark my words) halipo duniani labda kwa Tanzania hii tu ya viwanda vya cherehani.
Sheria za nchi yetu zipo vizuri tu na zimeelekeza kila kitu na hata kanuni za udereva wa kujihami zipo na vitabu vipo.
Vyuo vipo watu hawataki kwenda kusomea udereva wanabaki na lawama kwa jeshi la polisi.
Mtu umepata leseni kulingana na uwezo wako wa kuendesha lakini unataka ujionyeshe barabarani kuwa unaweza kuendesha kwa mbwembwe nyingi na speed kubwa kwa kujidanganya kuwa huna Limit ya speed.
Limit ipo kwenye kwenye alama za barabara.
Ukiona kibao cha speed 100 huruhusiwi kuendesha zaidi ya kiwango hicho. Na kama haujui ni wajibu wako kutafuta elimu Darasani au kuwatafuta Wataalam wa mambo ya uchukuzi au wakaguzi wa magari uwaulize.

Tatizo Watanzania wengi wanadharau mambo mengi na kujifanya kuwa wanajua.
Profesa anajiona yeye hawezi kukaa darasani na kujifunza udereva wa kujihami anaona ni elimu ndogo sana.

Matokeo yake bosi yupo kwenye gari na ana leseni na hua anaendesha gari ya nyumbani lakini anaendeshwa na dereva hovyo barabarani bila kumkemea kuwa anakiuka kanuni za bora za udereva na maadili take.

Wasimamizi wa sheria tutawalaumu bure mana wao wanajutahidi kuadhibu kama kanuni na sheria zinavyowaelekeza.
Elimu inatolewa kabla ya kosa kutendeka lakini ukisha vunja sheria jukumu la wasimamizi wa sheria ni kukuadhibu kwa mujibu wa sheria inayohusika.

Ingekua ni masuala ya kutoa elimu basi watu wangeomba wapekekwe mahakamani ili wakapewe elimu na hakimu.
Watu wanashindwa kutofanutisha kuonya na kutoa elimu.

Elimu inatolewa kwa wajinga na wale wanaotaka kujiendeleza ambao wao wanaelimu Ila wanaamua kusoma zaidi.
Sasa sio kazi ya Askari barabarani kumfundisha dereva alama za barabarani wakati yuko ndani ya gari anaendesha .

Lakini ni jukumu la wasimamizi hao wa sheria kutoa elimu mashuleni na kwa watembea kwa miguu wasiojua sheria na kanuni za usalama barabarani.
Ndio maana Mara nyingi wanafanya hivyo kwa abiria lakini sio kwa madereva.


Ni vizuri madereva hasa wa magari binafsi wakatafuta vitabu vya kanuni za udereva wa kujihami kwa Walimu wa NIT au Veta.
Ni kwa faida ya Taifa na wao wenyewe.
Sioni sababu ya kutegemea huruma ya Askari wakati mtu amevunja sheria kwa makusudi.

Askari tuwalaumu kwa kubambikiza makosa yasiyopo kama vile kumwandikia mtu faini kwa sababu gari INA vumbi. Hapo kama atafanya hivyo basis tumlaumu lakini kwa mwendo kasi kwa kuvuka Taa nyekundu,kutofuata alama za kukataza kupita gari jingine.
Kutozingatia speed ya wastani kwenye makazi ya watu ambayo sheria iko wazi kuwa isizidi 50km/hr. Hapa kwa kweli tusiwalaumu wasimamizi wa sheria.

Mara nyingi madereva wanawashawishi askari kwa kutoa rushwa baada ya kufanya kosa.
Kama huna kosa huwezi kutoa Rushwa kamwe utakua ni ujinga wa kupitiliza.
Kama sina kosa mtu akiniandikia nitakwena mpaka kwa Rais kama IGP hatanisikiliza.

Yani gari yangu taa zinawaka halafu uniandikie faini kuwa haziwaki. Itakua ni balaa la hatari.
Kwenye speed 50 ukitembea 48 nani atakuandikia?

Tukitimiza wajibu wetu kama madereva nadhani tutabaki kwenye suala la miundo mbinu na Ubovu wa gari lakini kwa dereva aliyesoma udereva hawezi kuendesha gari bovu.
Kitu cha kwanza kabisa kufundishwa kwenye udereva ni namna ya dereva kukafua mifumo muhimu ya gari.
 
Issue ya ajali ni bara bara zisizokidhi viwango, magari yasiyokidhi vigezo vya usalama na rushwa katika uhakiki na utoaji wa leseni. Magari mengi nchini maximum speed ya manufacturer ni 180km/hr ambayo ni ya kawaida.

Maelezo yako yana akisi kwa nini pasipo kuwepo limit zilizo wazi tunatembea barabarani kwa kudra tu na tuendelee kusubiria rambirambi.

Haipo barabara au kipande chochote cha barabara popote hapa nchini chenye kupitisha gari yoyote katika mwendo wa kufika 180km/h kama ilivyokuwa hapo kwenye maelezo yako.

Hii inatisha. Katika 180km/h usalama wako na watumiaji barabara wengine je, uhalisia uko wapii?
 
Back
Top Bottom