Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Mkuu inawezekana kwani mimi nilikwishawahi kusafiri kutoka Mbeya kuja Dar,kulikuwa na utaratibu basi la kwanza kuondoka kituoni anapanda Trafik,mabasi yanayofutia yalikuwa yanakuja kwa mwendo mzuri bila kulipita basi lililotangulia,kizaza kinakuwa anaposhuka yule Trafik mwendo kasi unaaza.Utaratibu huu unaweza kuwa mzuri ukiboreshwa na sina hakika kama unaendelea huko Mbeya.
 
Polisi hawa hawa wapiga mabao au tuombe msaada wa kupata polisi wengine toka nje ya nchi?
 
Wakuu ni wazo tu,

Kwamba ili kupunguza ajali ambazo zimepoteza maisha ya ndugu zetu wengi.

Haya mabasi yaendayo mikoani yawe na polisi hata mmoja kwa kila basi,kwa mfano safari kutoka Dar kwenda Arusha polisi anaweza akashuka Tanga kupokezana na mwingine na akarudi na lingine kuelekea Dar.

Kuwe na utaratibu basi linapoondoka abiria kuhakikisha kuwepo na polisi na kuangalia vitambulisho vyake,haya yote ili kupunguza ajali,atakuwa anajua gari linaendaje.

Haya ni maoni yangu tu mwenye maoni tofauti atoe ili kupunguza ajali za barabarani.

Kwahio nyie abiria 65 ndani ya basis hamjitambui au hamjui gari likiendeshwa kihasarahasara mpaka muwekewe polisi?! Akili ya polisi mmoja inawzidi nyie wote!? Inashangaza Sana abiria 65 mnashindwa kumnyoosha dereva?!
 
Mkuu kuna taarifa kuwa imetokea ajali leo barabara ya Dodoma Basi la abiria kwa jina la kidia one limegongana na Lori la mizigo uso kwa uso watu wawili wamepoteza maisha na zaidi ya watu 40 wamejeruhiwa, chanzo cha ajali Dereva wa Basi la Abiria kutaka kulipita gari na kukutana na Lori uso kwa uso.Abiria hawana habari na usalama wao.
 
Muundo wa basi na kontena (picha hapo chini) hakuna tofauti hasa kwenye shape na nguzo zake, tofauti ni kuwa yawezekana kuwa kontena ni gumu kubonyea kwani halina madirisha. Kufanana kwa shape kuna maanisha kuna nguzo zinazobeba hizo dimensions 3.

Mabasi mengi ya Tanzania ni malori yenye bodi la basi lilotengenezwa Tanzania na kukosa nguzo imara. Mengi ya hayo mabasi yakipinduka matairi juu, sehemu yote ya juu kuanzia madirisha ubonyea kwani nguzo zake ni weak, au material ya nguzo ni weak, ama hakuna nguzo kabisa. Kwa picha hiyo chini hilo body la basi halina nguzo kabisa, na limebonyea kabisa!!

Serikali iondoe 'mabasi-malori' barabarani kupunguza vifo vya wasafiri kwa mabasi wengi wao wakiwa watanzania. Kwanza huo ni wizi kumtoza mtu nauli ya basi la ukweli na kumpandisha kwenye 'basi-lori'. Waziri Sitta na TBS wanatakiwa kushughulikia suala hili!!

Wananchi nawaomba tusipande 'mabasi-malori'!!

ajali_mafinga.jpg


Source ya picha: Mwananchi Corporation Ltd.
 
Harafu hilo gari ukiriangalia ivi utafikiri wametengenezea singboard na mabati tu ya kawaida harafu wamepaka na rangi si unajua mambo ya mchina tena na hayo mabasi yako mengi sana
 
Hatari sana mi ndio maana nilikuaga nawatoa wenge madereva hiace kelebu mbili matata sana kwa upuuzi kama huu.
 
Ajali nyingine zinasababishwa na uzembe wa madereva siyo bangi hata ulevi unaweza kuchangia pia katika hili.
 
Mzee funguka vizuri una maana waliogoma jana au? Maake mie nahisi madereva wengi wanaendesha magari yao madogo
 
Ajali nyingine zinasababishwa na uzembe wa madereva siyo bangi hata ulevi unaweza kuchangia pia katika hili.
Halafu watu wanaunga mkono madereva kukataa kwenda kusoma,hii hatari,sijui wanaona raha watu wanavyokufa?
madereva wakasome jamani,nani ajui umuhimu wa kusoma hata kama ni dereva?
kuna kujua alama,sheria na Technolojia ya magari.
 
Ni kweli kabisa mkuu na sidhani kama wanafamilia kwa vitu vya kipumbavu wanavyofanya
 
Jamani wadau tuache ushabiki hawa madereva wakasome watatuua sana jamani,hata kama ni ndugu zetu,
wengi ni wavuta bangi,wasiosoma,kazi wanayoifanya ni kubwa na Nzuri sana ila hawapendi kabisa kujiendeleza..
hi inakuaje Mtu kaajiriwa kama Operator wa folk lift,operator wa mitambo,au operator wa maji,lakini utakuta wanajiendeleza ili awe mzuri zaidi,na kuweza kupambana na trouble shooting,sasa trouble shutting za kwenye magari ni kifo,halafu hawa jamaa hawataki kabisa kusoma,hata kujitolea kusoma ni wachache sana sana 2 kati ya 45.ok sio mbaya sana basi uanzishwe utaratibu waajiri wao wawapeleke shule,kozi fupi kwa ajili ya kunoa na kuimarisha fani yao.
Technolojia inabadilika kila mara,hata injini,gear box,nk zinabadilika kulingana na uwezo na muda,mtu kasoma miaka 10 tu iliopita anataka kila siku aendeshe kama alivyozoea,changamaoto barabarani ni nyingi sana,
Mimi nachukulia udereva ni kazi kama kazi nyingine za Mitamboni,mtu anaendesha mtambo jamani,ambapo kila baada ya miaka kadhaa say 2,3 kuna kuwa na tathmini ya kazi yako,sasa hawa nani anawatathmini,AJALI NDO TATHMINI YAO..
GARI NI CHOMBO KINARAHISISHA KAZI YA USAFIRI,HIVYO GARI NI MASHINE,HIVYO MWENDESHA MASHINE WA MITAMBONI ANAEFANYA SHIFT,NA DEREVA WA MABASI NA LORI MIMI SIWATOFAUTISHI.
TUBADILIKE Kusoma sio upate Phd,la hasha upate maarifa ya ziada ambayo yanapatikana kwenye fani yako pia u share changamoto unazokumbana nazo barabarani na wenzio.
Ahsante.
Usalama kwanza,kazi baadae.
Safety first,Work later"
 
Halafu watu wanaunga mkono madereva kukataa kwenda kusoma,hii hatari,sijui wanaona raha watu wanavyokufa?
madereva wakasome jamani,nani ajui umuhimu wa kusoma hata kama ni dereva?
kuna kujua alama,sheria na Technolojia ya magari.

Mkuu ni elimu pekee ya kujitambua,kujali na kuthamini ndio inayoweza kusaidia!madereva wamekosa hivyo vitu hapo juu,magari na sheria husika zote wanazijua.
 
Wandugu wapendwa

Nimesikitishwa sana kuona kila kukicha hapa jukwaaani habari kubwa siku hizi ni ajali za barabarani huku watu wengi wasio na hatia wakipoteza maisha. Hili ni jambo baya sana kwa taifa letu na ni wajibu wetu kwa kila Mtanzania kutoa ushauri kwa serikali nini kifanyike kupunguza ajali

Mimi kama Mtanzania, ninapenda kutoa ushauri wa mambo machache tu ambayo nadhani kama yakifanyiwa kazi ajali zitapungua sana nchini

1. Mabasi na malori yote yafungwe speed govenors ili yasikimbie mwendo mkali at least 80km

2. Serikali ipanue barabara kuu kama zile za Mbeya Dar na Chalinze Arusha kuwa na njia nne, yaani mbili kwenda na mbili kurudi .

3. Barabara kuu zote ziwe zimetenganishwa katikati kwa kutumia ukuta mgumu wa zege (Hutasikia tena magari yakigongana uso kwa uso)

4. Alama za barabarani ziongezwe kwa wingi kila sehemu na ziwe visible kwa madereva(SEHEMU NYINGI ZENYE KONA KALI HAZINA ALAMA)

5. Kuwe na Highway patrol ya police kwenye barabara zote kuu

6. Kuwe na ambulance kila baada ya kilomita mia kwenye barabara kuu ili kuokoa maisha ya watu

7. Kuwe na taa za barabarani zinazofanya kazi kwenye barabara zote kuu nchini , hii itasaidia madereva kuwa wanaona vizuri kwani wakati mwingine ajali husababisha na dereva anaekuja kutokea upande mwingine kutumia full beam kwa sababu hawaoni vizuri.

8. Polisi warudishiwe tochi ili wakamate madereva wakorofi

9. Adhabu ya kifungo itolewe kwa madereva walevi

10. Wananchi tuisaidie polisi kwa kureport madereva wanaoendesha magari kwa kuhatarisha maisha ya wengine, tumieni simu zenu kuwarekodi,

Najua kua uchumi wetu ni mdogo na serikali imejitahidi sana kutujengea bara bara nzuri ambazo hatujawahi ziona tokea uhuru, lakini tujue uzuri wa barabara ndio chanzo cha hizi ajali. Madereva wanajisahau sana kwani walizoea mashimo na vumbi tupu, sasa wamewekewa lami wanataka kwenda spidi kuliko hata magari yenyewe
 

Attachments

  • motorway.JPG
    motorway.JPG
    510.7 KB · Views: 200
Inaonekana kwenye pic hii magari makubwa yana njia ya pekee

Hapana mkuu,

Magari makubwa kisheria yanatakiwa yatembee upande wa kushoto ili kuyapisha magari yanayokwenda kasi upande wa kulia yapite, upande wa kulia ni kwa ajili ya ku ovateki tu au kama magari ni mengi basi kwa ajili ya magari yanayokwenda kasi zaidi.

Ni makosa mtu uko peke yako barabarani kuendesha gari upande wa kulia
 
Tatizo sio barabara.
Kinachochangia kuongezeka kwa ajali ni viongozi wa sasa ambao wako busy kuua reli za kati na Tazara, ambazo zilikuwa zinasaidia kupunguza idadi ya magari makubwa ya mizigo barabarani
 
Back
Top Bottom