Ajali ya basi la Ester, Rav4 yaua watatu Kilimanjaro

Ajali ya basi la Ester, Rav4 yaua watatu Kilimanjaro

Inasikitisha mno tena mno .
Kuna nchi ili upate leseni ya udereva ni hadi uwe umehakikiwa kweli kweli sana hatari haikuwa kwake yeye dereva mzembe bali anaweza kusababishia wengine kufa au ulemavu wa kudumu ambao wako innocent.
Na ndio ukweli we unaweza kufata sheria akaja mwingine akakuletea shida
Nadhani tz ni Moja kati ya nchi watu hawafati sheria duniani na sio TU barabarani Bali kwenye mambo mengi zikiwemo ofisi
 
Dah! Pole Kwa familia zilizopoteza wapendwa wao..

RIP
Watu watatu wamefariki dunia papo hapo baada ya gari aina ya Toyota Rav4 waliokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na basi la abiria la Kampuni ya Ester Kuxury, mkoani Kilimanjaro leo Jumamosi Februari mosi, 2025.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoani Kilimanjaro, Jeremiah Mkomagi amesema ajali hiyo imetokea eneo la Mdawi, Wilaya ya Moshi.

"Ajali imetokea leo asubuhi eneo la Mdawi, watu watatu waliokuwa kwenye gari dogo aina ya Toyota Rav4 wamefariki dunia baada ya gari hilo kugongana uso kwa uso na basi la kampuni ya Ester Luxury lililokuwa likitokea Moshi kwenda Dar es Salaam," amesema Mkomagi.

Amesema chanzo cha ajali ni baada ya dereva wa gari dogo kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari na kwenda kugongana uso kwa uso na basi hilo.

Hata hivyo, Kamanda Mkomagi amesema hakuna majeruhi kwenye basi hilo, na miili ya marehemu waliokuwa kwenye gari dogo imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro, Mawenzi.

 
Ajali imetokea leo asubuhi eneo la Mdawi, watu watatu waliokuwa kwenye gari dogo aina ya Toyota Rav4 wamefariki dunia baada ya gari hilo kugongana uso kwa uso na basi la kampuni ya Ester Luxury lililokuwa likitokea Moshi kwenda Dar es Salaam," amesema Mkomagi.
Pole wafiwa
Ila tusidanganye watu hakuna luxury buses Tanzania
 
Hizi basi za kampuni ya Ester zikiwa barabarani wanajiona kama wao wanamiliki hii nchi. Hawajali watumiani wengine wa barabara na ndiyo chanzo cha wao kupata ajali mara kwa mara.

Hizi basi inabidi kuchukua tahadhari sana unapokutana nazo njiani. Hawachelewi kukuletea ajali makusudi tu.

Wapate pumziko la amani marehemu wote wa hii ajali
 
Hizi basi za kampuni ya Ester zikiwa barabarani wanajiona kama wao wanamiliki hii nchi. Hawajali watumiani wengine wa barabara na ndiyo chanzo cha wao kupata ajali mara kwa mara.

Hizi basi inabidi kuchukua tahadhari sana unapokutana nazo njiani. Hawachelewi kukuletea ajali makusudi tu.

Wapate pumziko la amani marehemu wote wa hii ajali

Zinakimbia balaa huko barabarani.
Mwendokasi kama wote.
Ukizikuta usiku zinavyo overtake hovyo Yaani ni hatari balaaa.
 
Watu watatu wamefariki dunia papo hapo baada ya gari aina ya Toyota Rav4 waliokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na basi la abiria la Kampuni ya Ester Kuxury, mkoani Kilimanjaro leo Jumamosi Februari mosi, 2025.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoani Kilimanjaro, Jeremiah Mkomagi amesema ajali hiyo imetokea eneo la Mdawi, Wilaya ya Moshi.

"Ajali imetokea leo asubuhi eneo la Mdawi, watu watatu waliokuwa kwenye gari dogo aina ya Toyota Rav4 wamefariki dunia baada ya gari hilo kugongana uso kwa uso na basi la kampuni ya Ester Luxury lililokuwa likitokea Moshi kwenda Dar es Salaam," amesema Mkomagi.

Amesema chanzo cha ajali ni baada ya dereva wa gari dogo kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari na kwenda kugongana uso kwa uso na basi hilo.

Hata hivyo, Kamanda Mkomagi amesema hakuna majeruhi kwenye basi hilo, na miili ya marehemu waliokuwa kwenye gari dogo imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro, Mawenzi.

Kwa kumjua Mmiliki wa Basi la Ester, alivyo Kitabia na anapenda nini huku mwaka huu ukiwa ni mwaka wa Uchaguzi Mkuu hapa najua sana Kafara limekubali na mwaka huu atashinda tena Ubunge huko Jimboni Kwake na kuendelea kutamba hadi katika Noti mpya za duniani.
 
Tatizo lipo pande mbili, kutofuata sheria lakini pia miundo mbinu sio rafiki. Baada ya kukamilika miradi iliyopo sasa ya SGR, BWAWA, MADARAJA, nk. Ingependeza sasa Mradi mkubwa uwe wa kuweka Barabara Nne za Njia kuu zote nchini. Itasaidia kupunguza ajali kwa asilimia kubwa sana.
 
Ajali nyingi bongo ni kukosa umakini Kwa madereva, barabara zenyewe za ku overtake hovyo ziko wapi Sasa?. Njia ikitanda semi moja la maana tu ishakuwa kama kiuchochoro Fulani hivi, tuwe makini sana barabarani na kama una gari ndogo omba sana usifanye uzembe highway ukakutana na semi ya mizigo ama basi Iko full masinondo utakunya Hadi mavi ya mwisho.
 
Ila kuna madereva wengine nao ujinga umewajaa hasa wa malori na mabasi.

Anaona kabisa usha-overtake upo upande wake na umbali aliopo hakuna shida,ajabu naye ananyoosha goti kwa vile tu wewe una gari dogo!

NB:Ajali za wakati wa ku-overtake huwa ni kifo maana mwendo lazima uwe wenyewe!
 
Huko shule hauwezi funzwa vingine tofauti na serikali inavyotaka.
Si umeona huyo wa rav4,alikua anamfuata Kidia bila kuchukua tahadhari yake binafsi,shuleni tumefundishwa somo la tuwe na udereva wa kujihami,akauziwa kicheche,hakufuata sheria za driving,kwamba uovertake tu pale unapojihakikishia usalama wako kwanza.

Shule haijawahi kudanganya,ni kama kioo vile
 
Si umeona huyo wa rav4,alikua anamfuata Kidia bila kuchukua tahadhari yake binafsi,shuleni tumefundishwa somo la tuwe na udereva wa kujihami,akauziwa kicheche,hakufuata sheria za driving,kwamba uovertake tu pale unapojihakikishia usalama wako kwanza.

Shule haijawahi kudanganya,ni kama kioo vile
Hapo ilipotokea ajali huwa kuna Misongamano ambayo hupelekea hizo overtake , tungekua na barabara pana inayoweza kukidhi uwingi wa vyombo , ingekupunguza ajali kwa kiasi kikubwa .
 
Hizi basi za kampuni ya Ester zikiwa barabarani wanajiona kama wao wanamiliki hii nchi. Hawajali watumiani wengine wa barabara na ndiyo chanzo cha wao kupata ajali mara kwa mara.

Hizi basi inabidi kuchukua tahadhari sana unapokutana nazo njiani. Hawachelewi kukuletea ajali makusudi tu.

Wapate pumziko la amani marehemu wote wa hii ajali
Soma vizuri na sikiliza kwa makini maelezo ya mashuhuda, chuki zako usituhusishe sisi. Hiyo Rav4 iligongwa nyuma kwenye tairi ya akiba na basi la Kidia One hivyo ikasukumwa na kwenda kujigonga kwenye basi la Ester.
 
Ajali hii imeua mwalimu mstaafu ,mwanamke mwalimu Ayo, alikuwa ametoka kupata mafao yake yaliyopelekea pia kununua gari mpya.
Kwenye gari alikuwa na mwanaye wa kiume ( dereva) , akiwepo pia rafiki wa mtoto wa mwalimu ambaye ni dereva.
Gari ni mpya kabisa na imesajiriwa jana.
FB_IMG_1738427254161.jpg
 
Watu watatu wamefariki dunia papo hapo baada ya gari aina ya Toyota Rav4 waliokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na basi la abiria la Kampuni ya Ester Kuxury, mkoani Kilimanjaro leo Jumamosi Februari mosi, 2025.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoani Kilimanjaro, Jeremiah Mkomagi amesema ajali hiyo imetokea eneo la Mdawi, Wilaya ya Moshi.

"Ajali imetokea leo asubuhi eneo la Mdawi, watu watatu waliokuwa kwenye gari dogo aina ya Toyota Rav4 wamefariki dunia baada ya gari hilo kugongana uso kwa uso na basi la kampuni ya Ester Luxury lililokuwa likitokea Moshi kwenda Dar es Salaam," amesema Mkomagi.

Amesema chanzo cha ajali ni baada ya dereva wa gari dogo kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari na kwenda kugongana uso kwa uso na basi hilo.

Hata hivyo, Kamanda Mkomagi amesema hakuna majeruhi kwenye basi hilo, na miili ya marehemu waliokuwa kwenye gari dogo imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro, Mawenzi.

Qafr za mbio 2030
 
"Fatigue" huwa inaathiri sana maamuzi ya dereva unknowingly.
 
Back
Top Bottom