Freema Agyeman
JF-Expert Member
- Mar 3, 2011
- 3,666
- 3,532
Asante sana mkuu. Ndio maana nimesafiri mara tu nilipopata taarifa. Ndugu zangu wengine bado hawaamini na hawataki kuamini. Kaka alikuwa na watoto hao hao ndio walikuwa wanampa faraja baada ya mke wake kuitwa na Mungu mwezi wa pili mwaka huu.
Barabara ina lami mkeka kabisa...Ingawa sio mwenyeji lakini naona kama watu wamesimama kwenye lami, au nakosea
Hlf sasa hao madereva wanaendesha kama wamebeba gunia za viazi na si watoto... pale fire siku moja mpk trafik alimpa vitasa dereva karibu asababishe ajali aue watoto wa watuniliwahi kusema katika usafiri mbovu sana ni hizi school bus, nikaleta kisa cha school bus ya heritage school iliyokuwa imebeba wanakwaya baada ya kusimamishwa walihamaki na kumshambulia trafiki hadi kumtolea mapepo yake.
serikali ipige marufuku hizi school bus hadi zitakapokaguliwa na TRO na kuhakikishwa ni salama kubeba watu, kuna shule huku mwanza ukiikuta school bus imeegeshwa huwezi amini kama inatembeaga! Madereva wote wa school bus wapelekwe veta wafanyiwe mafunzo na kuhakikiwa upya na veko kama wanazo sifa na weledi wa kuendesha school bus.
Mkuu unahuzunisha na kuchekesha.
Umeshaenda kwa doctor kujifunza mbinu mbalimbali za kupanga jinsia ya mtoto??
Usendelee kuchepuka tafadhari
ukitaka kugombana na mtoto mkataze kwenda hizo tour sijui walimu wanawapaga nini watoto?Poleni sana wafiwa.
Binafsi huwa sipendi kabisa hizo safari za kishule maana naona zipo kibiashara zaidi. Ni kama miradi ya shule vile!
We ntakufahamu tutakuwa tunakaa mtaa mmojaNooooo jaman sitaki kuamini shule nnayoifaham na mwanang alisoma hapo kabla hajahama
Mtt wa mpangaj mwwnzang anasoma hapo ahaaa kwann lkn kifo watt wetu wapendwa mmeondoka mapema sana
Ni kweli ndugu,wiki hii tumepoteza ndugu watano wa familia moja pale Mwidu kabla ya kufika Chalinze ukitokea Moro,walikuwa na private car tairi la mbee likapasuka,ajali haichagui,ni kuomba tu Mola atusimamie.13 mega pixel ajali haichagui kuwa mko mkwenye private or public transport. Ni kumuomba Mungu aziepushe tu.
Amen ndugu yangu. Mungu ni mwema.Pole sana mkuu Mungu pekee ndio faraja yetu anayajua mawazo yetu,anaijua kesho yetu pia ni yeye pekee anayejua kwanini kaka anapitia ktk mapito magumu kiasi hichi, basi yeye akawe faraja kwenu hasa ktk kipindi hiki kigumu na akamfute kaka machozi na kumuwezesha kusimama tena na pia ampe dogo pumziko jema la milele "Amina"
pongezi kwa kutujuza na poleni sana .Nimepata habari isiyo na shaka kuwa gari aina ya coaster limeua watoto karibu wote waliokuwa wanaelekea mjini Karatu kwa ziara ya kimasomo including(joint examinations), taarifa zinasema wamebaki watoto(3) tu wengine wamefariki, shule inaitwa Lucky Vincent Nursery & Primary School ipo Arusha ni medium schools,kwa wenye updates tunaomba mtupe
Picha: Soon ntaziapload ni ajali ya mda huu
Mungu awalaze mahali pema peponi
----------------------
UPDATE: Coaster ina jumla ya abiria 30 na wote wanasadikiwa wamefariki,maiti zimepelekwa hospitalini na watu wameondoka eneo la tukio,mvua inanyesha
UPDATE: Picha zinakuja soon ripota yuko eneo la tukio..
.........................
UPDATES:Magari ya polisi yametanda kila kona na maiti zimebebwa na magari ya polisi
Tayari kuhifadhiwa
...................
UPDATES:Ni watoto wanne(3) wanasadikiwa wako hai ila wako mahututi kabisa na kuna wasi wasi vifo vikaongezeka
UPDATES:Lucky vincent nursery school bus
UPDATES:Shughuli za uokozi
UPDATES:Gari lilikuwa na abiria 30 wanafunzi 25,waalimu (4) wote wa kiume na dereva 1
................
UPDATES:Kati ya majeruhi watoto watatu(3) wawili wako mahututi kabisa na mmoja amepasuka ubongo
................
UPDATES:Maajabu ya ajali hakuna damu zozote zilizotapakaa licha ya watu wengi sana kufa!
..................
UPDATES:Majeruhi mmoja kati ya( 3) amefariki kabla ya kufikishwa hispitali,kwahy taarifa zinasema wamebaki majeruhi wawili walioko ICU
...............
UPDATES:Kuna mkanganyiko mwingi kuhusu chanzo cha ajali ila nature ya eneo la ajali ni mteremko mkali na kuna daraja,ni eneo ambalo dereva anatakiwa kuwa makini kabisa,kwa dareva asiyemwangalifu inaweza tokea lolote,hebu angalia hapo gari lilipotumbukia na haikuwa ina over take ,u can diagnose the nature of an accident
Hakika ni mtihani ila Mungu atabaki kuwa Baba naye atawapa faraja iliyo kuu.Asante sana mkuu. Ndio maana nimesafiri mara tu nilipopata taarifa. Ndugu zangu wengine bado hawaamini na hawataki kuamini. Kaka alikuwa na watoto hao hao ndio walikuwa wanampa faraja baada ya mke wake kuitwa na Mungu mwezi wa pili mwaka huu.